Uwe unasoma bila jaziba , mimi nimekuwekea Uongo wa Injili ya Luka , sisemi mimi ,
1.
- Mathayo 2:1 inasema Yesu alizaliwa wakati wa Mfalme Herode Mkuu.
- Luka 2:1-2 inataja kwamba Yesu alizaliwa wakati wa oda ya usajili chini ya Kaisari Agustusi.
Hizi taarifa zinatoa vidokezo vya kihistoria ambavyo watafiti hutumia kukadiria mwaka:
2.
- Herode alikufa mwaka wa kuanzia 4 KK au 1 KK kulingana na baadhi ya rekodi za kihistoria (Josephus).
- Ikiwa Yesu alizaliwa wakati wa Herode, hiyo inaashiria kuzaliwa kabla ya kifo cha Herode, kwa hivyo wengi wanaweka mwaka wa kuzaliwa kati ya 6–4 KK.
3.
- Luka anataja usajili wa watu wakati wa Kaisari Agustusi. Watafiti wanasema hii inaweza kuashiria mwaka karibu 6–4 KK, kulingana na rekodi za usajili wa Kiroma.
4.
- Krismasi inaadhimishwa tarehe 25 Desemba, lakini hii haimaanishi tarehe halisi ya kuzaliwa kwake. Tarehe hii ilichaguliwa karne za kwanza na za pili kuendana na sikukuu za jua za Roma (Sol Invictus).
5.
- Maoni ya Kawaida: 4–6 KK.
- Watafiti wengine: Baadhi wanasema 7 KK, kulingana na tafsiri ya rekodi za Herode na nyota ya Wamagi.
- Sababu ya tofauti: Kutokuwepo kwa maandiko ya moja kwa moja ya mwaka, na tofauti kati ya Injili za Mathayo na Luka.
Kwa kifupi,
Biblia haelezi mwaka kamili wa kuzaliwa Yesu, lakini kwa kutumia vidokezo vya kihistoria, watafiti wengi wanakisia
kati ya 6–4 kabla ya kuzaliwa kwa Kristo (KK).
Maandiko yako haya ni sahihi. Na katika maandiko haya sijauona huo uwongo wa injili ya Luka.
Unapolisoma.neno la Mungu zingatia mktadha wa andiko, na siyo vitu vidogo vidogo kama tarehe.
Fahamu yafuatayo:
1. Yesu alipoondoka hakuacha injili iliyoandikwa, injili iliachwa kwenye mafundisho aliyowapa mitume wake. Na hawa mitume, hata walipoenda maeneo ya nchi mbalimbali, walilenga zaidi kuwabadilisha watu na kuwa wakristo kwa kuzingatia maagizo ya Kristo, hawakulenga kwenda kuwasimlia watu tukio moja moja na wakati lilipofanyika. Injili katika muundo iliopo sasa, kwa mara ya kwanza ilikuwa karibia miaka 30 baadaye, ikilenga kuwajulisha watu juu ya historia ya wokovu wa mwanadamu.
Ndiyo maana injili za waandishi wote wanne, hawatofautiani kabisa kuhusu msingi wa mafundi sho ya Kristo. Wote wameandika maagizo ya Kristo:.
UPENDO
MSAMAHA
Na kisha wote wameandika kuhusu matukio makuu
KUSULIBIWA KWA KRISTO
KUFUFUKA
KUPAA MBINGUNI
Ufahamu kuwa matukio haya yalitokea wakati hii kalenda ya sasa haikuwepo, walikuwa na namna yao ya kuhesabu siku, miezi na miaka. Kuashiria kipindi fulani na siyo tarehe, walitumia zaidi vizazi, na kizazi kimoja ilikuwa ni miaka kati ya 35-40 ya sasa. Ni mara chache kwa wasomi wachache walitumia kalenda za Mesolithic Lunar calenda. Kuna kumbukumbu nyingine za simulizi ambazo hazipo ndani ya biblia, ni kwamba Yesu Kristo alisulibiwa tarehe ambayo Bikira Maria alipewa ujumbe wa kupata mimba kwa ujumbe wa malaika. Na tarehe ambayo Yesu alisulibiwa ni tarehe 14 mwezi Nisan, mwezi Nisan, ni mwezi wa March kwa sasa. Hivyo ukiongeza miezi 9, inaangukia mwezi December. Lakini bado haikupi uhakika wa 100% juu ya tarehe. Kipindi hicho cha mwezi December kinawianika na kipindi ambacho wachungaji wa mifugo walikuwa wakipeleka mifugo yao maeneo hayo.lakini cha kuzingatia ni kuwa hata kama ingekuwa ni exactly the same date, bado haimaanishi ndiyo siku aliyozaliwa, hiyo ni kumbukumbu ya tukio la miaka mingi, hivyo hakuna ubaya kama kufanya tarehe yoyote ndani ya kioindi husika.
Kuna maandiko mengine nje ya biblia, nadhani ni andiko la ushuhuda wa Yohana juu ya Bikira Maria kupaa mbinguni, Maria alipewa habari ya kupata mimba, siku ya kwanza ya juma, Yesu alizaliwa siku ya kwanza ya juma, na alifufuka siku ya kwanza ya juma.
Tarehe ambayo ipo kwenye kumbukumbu, ni tarehe ya kusulibiwa Yesu Kristo, ambayo inatajwa kuwa ni tarehe 14 mwezi Nisan, ambayo kwa sasa wanasema ni kama tarehe 3 ya mwezi March. Lakini adhimisho la tarehe ya pasaka hubadilika badilika ili kuzipata zile siku 4 muhimu: Alhamis Kuu, Ijumaa Kuu, Jumamisi, Jumapili.
NB. Soma maandiko ya imani kwa lengo la kutaka kujua Mungu anataka ufanye nini ili kuyaishi mapenzi yake. Mengine ni nyongeza kwaajili ya kukuimarisha katika kutimiza ulichoagizwa.