Uonezi katika udahili 2017, Maombi chuoni na kila chuo unalipa

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,798
71,218
Hakika Watanzania sasa tunasomeshwa namba na nashangaa wale wanaounga mkono kila kinachofanywa na serikali. Kufikia mwaka jana ili vijana wetu wasome vyuo vikuu maombi yalikuwa yanafanywa sehemu moja tuu nayo ni TCU na mzazi ilikuwa unalipa shs 50,000/ pekee ukisubiri nafasi ya kusoma kijana atapangiwa wapi.

Sasa hivi serikali inayojinasibu kujali raia wake imesema kila mtu ata apply chuo atakacho mwenyewe, sio jambo baya lakini sasa wamelifikiria hili jambo la kulipa wakati wa maombi wakati mtu hana hakika ya kupata nafasi katika chuo anachoomba?

Maana ili kujipa nafasi ya kuweza kupata chuo mwanafunzi atawajibika kuomba vyuo vingi kadiri awezavyo na hapo hapo lazima alipe application fee kila chuo kwani hana hakika kipi atapata.

Kwa hili wazazi tulikuwa tunalipa 50000/ sasa tunaweza kujikuta tunalipa hata milioni, jee huku ndio kumjali mwanachi? Kwa nini malipo yasifanywe kama admission fee kwa wale watakao chaguliwa tuu?

Haya mambo ya kutekeleza mawazo ya mtu mmoja anayokurupuka nayo na kuzoza majukwaani yanatuletea shida kubwa sana na kufanya maisha ya Watanzania kuwa ya misukosuko.
 
Tanzania watu wengi sana ni vilalamishi sana, mliikataa TCU sasa udahili wa moja kwa moja vyuoni nao mnaanza kuleta nongwa!?

Ngoja muisome namba ndiyo mtakoma.
Unayajua maisha ya Mtanzania wa kawaida au unazoza tuu? Kuna sababu gani kulipa 50000 kwa kila chuo utakachoomba? Kwa nini hiyo hela asitozwe mwanafunzi kama admission fee pale atakapokuwa kachaguliwa?
 
Hakika Watanzania sasa tunasomeshwa namba na nashangaa wale wanaounga mkono kila kinachofanywa na serikali. Kufikia mwaka jana ili vijana wetu wasome vyuo vikuu maombi yalikuwa yanafanywa sehemu moja tuu nayo ni TCU na mzazi ilikuwa unalipa shs 50,000/ pekee ukisubiri nafasi ya kusoma kijana atapangiwa wapi.

Sasa hivi serikali inayojinasibu kujali raia wake imesema kila mtu ata apply chuo atakacho mwenyewe, sio jambo baya lakini sasa wamelifikiria hili jambo la kulipa wakati wa maombi wakati mtu hana hakika ya kupata nafasi katika chuo anachoomba?

Maana ili kujipa nafasi ya kuweza kupata chuo mwanafunzi atawajibika kuomba vyuo vingi kadiri awezavyo na hapo hapo lazima alipe application fee kila chuo kwani hana hakika kipi atapata.

Kwa hili wazazi tulikuwa tunalipa 50000/ sasa tunaweza kujikuta tunalipa hata milioni, jee huku ndio kumjali mwanachi? Kwa nini malipo yasifanywe kama admission fee kwa wale watakao chaguliwa tuu?

Haya mambo ya kutekeleza mawazo ya mtu mmoja anayokurupuka nayo na kuzoza majukwaani yanatuletea shida kubwa sana na kufanya maisha ya Watanzania kuwa ya misukosuko.
Kuomba udahili siyo kamali au bahati nasibu. Mwombaji sharti awe na confidence ya course anayoiomba kwa kuwa amefaulu kusoma course hiyo. Sasa hapa habari ya kujaribu course za kila university inatoka wapi? acheni upuuzi wa kuogpa maendeleo. Maendeleo ni kazi na yana gharama; kama elimu ni ghali, jaribu ujinga!
 
Ni kweli, zamani ilikuwa una apply popote ulipo ilimradi unaweza kupata huduma ya mtandao kwa gharama ile ile elfu 50 na unaweza kuomba hata vyuo vitano.

Lakini sasa inakubidi kila chuo ulipe hiyo elfu 50, na kutokana na hali halisi inakubidi ufike mahala husika. Sasa mfano mtu yuko kigoma tusema angalau aombe vyuo vinne viwili tuseme Dar es salaam, kingine Mwanza na kingine Songea, ina maana gharama za ku apply ni laki 2. Bado gharama za usafiri kufika maeneo husika na gharama za malazi kwa siku atakazo kuwepo maeneo husika. Hizi gharama ni kubwa. Matokeo yake mtu anaweza aka apply sehemu moja au mbili na kuongeza uwezekano wa kukosa nafasi.

TCU hawakuwa wakiwapangia tu wanavyotaka, bali waliangalia wenyewe vigezo kwanza ndio wapate nafasi katika maeneo husika. Hivyo hivyo ukikosa basi wanaenda sehemu ya pili uliyoomba mpaka utapata inayokufit. Sasa hivi kuna uwezekano wa mwenye sifa zaidi kukosa sehemu akapata mwingine mwenye sifa ya chini au watu wengi kujazana sehemu moja na wengine wakakosa wakati kuna sehemu watu wachache. Chuo hakiwezi kudahili wachache kiseme kisubiri wenye sifa zaidi labda wanakuja bali watabeba tu kwani wengine ni biashara.

Waangalie utaratibu mzuri wawasaidie watoto maskini, hivi walivyofanya sasa inawaumiza na italeta kelele nyingi.
 
Kuomba udahili siyo kamali au bahati nasibu. Mwombaji sharti awe na confidence ya course anayoiomba kwa kuwa amefaulu kusoma course hiyo. Sasa hapa habari ya kujaribu course za kila university inatoka wapi? acheni upuuzi wa kuogpa maendeleo. Maendeleo ni kazi na yana gharama. Kama elimu ni ghari, jaribu ujinga!
Wewe umesoma kwel? Kozi unayoomba inanafasi ya wanafunzi 100 tuu, jee mkiomba 300? Unadhani wote mtachukuliwa kama shule za kata? Kwa hiyo uwe na confidence ya kozi uliyoomba na ukikosa hiyo nafasi unafanyaje?
Kukosa maarifa ni janga.
 
Hakika Watanzania sasa tunasomeshwa namba na nashangaa wale wanaounga mkono kila kinachofanywa na serikali. Kufikia mwaka jana ili vijana wetu wasome vyuo vikuu maombi yalikuwa yanafanywa sehemu moja tuu nayo ni TCU na mzazi ilikuwa unalipa shs 50,000/ pekee ukisubiri nafasi ya kusoma kijana atapangiwa wapi.

Sasa hivi serikali inayojinasibu kujali raia wake imesema kila mtu ata apply chuo atakacho mwenyewe, sio jambo baya lakini sasa wamelifikiria hili jambo la kulipa wakati wa maombi wakati mtu hana hakika ya kupata nafasi katika chuo anachoomba?

Maana ili kujipa nafasi ya kuweza kupata chuo mwanafunzi atawajibika kuomba vyuo vingi kadiri awezavyo na hapo hapo lazima alipe application fee kila chuo kwani hana hakika kipi atapata.

Kwa hili wazazi tulikuwa tunalipa 50000/ sasa tunaweza kujikuta tunalipa hata milioni, jee huku ndio kumjali mwanachi? Kwa nini malipo yasifanywe kama admission fee kwa wale watakao chaguliwa tuu?

Haya mambo ya kutekeleza mawazo ya mtu mmoja anayokurupuka nayo na kuzoza majukwaani yanatuletea shida kubwa sana na kufanya maisha ya Watanzania kuwa ya misukosuko.
Kama siaminiamini! Ni kweli walioapply kwa mtindo mpya wametozwa sh.elfu 50 kwa kila chuo????
 
hii system ilikuagapo miaka hiyo.

Ikaja TCU mkalalamikaaa weee kwamba mnapangiwa na Serikali vyuo vya kusoma na mkataka TCU isiwepo ili kila mtu achague anachotaka kusoma.

Kaja Rais anayewapenda ambaye anataka msipangiwe vyuo vya kusoma kawarudishia system mnayotaka ya kuapply moja kwa moja chuoni. Mnalalamika tena MNATAKA NINI JAMANI?

Sio lazima uapply vyuo vitatu kama uko confident chagua chuo kimoja unachokipenda
 
hii system ilikuagapo miaka hiyo.

Ikaja TCU mkalalamikaaa weee kwamba mnapangiwa na Serikali vyuo vya kusoma na mkataka TCU isiwepo ili kila mtu achague anachotaka kusoma.

Kaja Rais anayewapenda ambaye anataka msipangiwe vyuo vya kusoma kawarudishia system mnayotaka ya kuapply moja kwa moja chuoni. Mnalalamika tena MNATAKA NINI JAMANI?

Sio lazima uapply vyuo vitatu kama uko confident chagua chuo kimoja unachokipenda
Wabongo hatujielewi tunataka nini

Makandila
 
Back
Top Bottom