Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,320
- 33,125
Ndugu zangu wana JF na pia viongozi wa Serikali wanaohusika ningependa kuwataarifa kuwa kuna vitendo vinafanywa na baadhi ya Maofisa wa Polisi wa Upelelezi hapo uwanja wa Ndege wa kimataifa Wa Dares-Salaam.
Hawa Mapolisi wa kipelezi wakikuona unatoka nje ya nchi wanakungoja tu umalize kutoka nje ya uwanja na hukukamata mpaka kwa ofisi zao za kipelelezi na kuanza kukuhoji na pia kukuweka ndani kwa muda wanaotaka wewe bila ya kosa lolote na wanaanza kukusachi wakihisi labda wewe ubeba madawa ya kulevya na endepo hautakuwa na hayo madawa watakuachia lakini kwa masharti lazima ukae kwao uende Toilet mara 3 ndio waweze kukuachia.
Na wakikuachia wanavizuia vitu vyako ulivyokuja navyo toka nje ya nchi eti wanavichunguza kwa muda basi hata kama ndio wanavichunguza haitowezekana wewe wakuache na vitu vyako wavizuie tena sio kwa muda mchache inachukuwa hata mwezi mmoja wanavichunguza.
Sasa inakuwaje hivyo vitu vyako ulivyokuja navyo wavichunguze kwa huo muda wa mwezi na haswa ukizingatia umekuja na mabegi ya nguo, zawadi kwa ndugu zako simu ya mkononi, Computer ya Laptop na vitu vingine vidogo vidogo?
Ninachoshangazwa mimi inakuwaje hivyo vitu vyako vinazuia kwa muda wa mwezi eti kwa sababu ya kwa uchunguzi? Swali hili itabidi tumulize Kaimu kamishna mkuu wa Upelelzi ndugu Fred Nzoe inakuwaje watu wake waliopo hapo kiwanja cha ndege cha kimataifa kuwanyanyasa raia wema?
Kwa hivyo vitendo vyao vya kuzuia mizigo yao kwa huo muda wa mwezi mzima kwa kisingizio cha kuvichunguza hivyo vitu?
Hayo yametokea kwa rafiki wangu alie toka nje hivi karibuni kafanyia hivyo na kila akienda huko Kiwanja cha ndege cha kimataifa cha hapo Dares-Salaam anazungushwa mara aambiwe kuwa Mkuu wa kituo wa Polisi hayupo njoo keshokutwa na akienda hiyo kesho kutwa hurushwa tena njoo tena kesho kutwa hii kweli ndugu zangu wana JF na Viongozi wa Serikali wanaohusika tutaendelea kweli?
Kwa fikira zangu hao wanaohusika hapo Aiport inaonyesha wanataka Rushwa wapewe pesa ili wapate kumuachia huyo Rafiki yangu vitu vyake walivyovizuia bila sababu yoyote ile ya maana. Je Ndugu Wana JF Mnalichukulia vipi hilo suala na hivi karibuni Mheshimiwa ndugu Rais wa nchi yetu JM Kikwete aliwakemea maofisa wa kuzuia rushwa wawajibike kikazi sasa ikiwa Mapolisi wetu wa kipelelezi wanamzungusha huyo rafiki yangu kumpa vitu vyake sasa inapata mwezi hawajibiki, je hao aliowakemea Ndugu Rais JM Kikwete maofisa wa kuzuia Rushwa wanafanya kazi gani?
Ningeomba mnisaidie hilo tatizo langu maoni yenu ndugu wana JF wenzangu asanteni sana.
Hawa Mapolisi wa kipelezi wakikuona unatoka nje ya nchi wanakungoja tu umalize kutoka nje ya uwanja na hukukamata mpaka kwa ofisi zao za kipelelezi na kuanza kukuhoji na pia kukuweka ndani kwa muda wanaotaka wewe bila ya kosa lolote na wanaanza kukusachi wakihisi labda wewe ubeba madawa ya kulevya na endepo hautakuwa na hayo madawa watakuachia lakini kwa masharti lazima ukae kwao uende Toilet mara 3 ndio waweze kukuachia.
Na wakikuachia wanavizuia vitu vyako ulivyokuja navyo toka nje ya nchi eti wanavichunguza kwa muda basi hata kama ndio wanavichunguza haitowezekana wewe wakuache na vitu vyako wavizuie tena sio kwa muda mchache inachukuwa hata mwezi mmoja wanavichunguza.
Sasa inakuwaje hivyo vitu vyako ulivyokuja navyo wavichunguze kwa huo muda wa mwezi na haswa ukizingatia umekuja na mabegi ya nguo, zawadi kwa ndugu zako simu ya mkononi, Computer ya Laptop na vitu vingine vidogo vidogo?
Ninachoshangazwa mimi inakuwaje hivyo vitu vyako vinazuia kwa muda wa mwezi eti kwa sababu ya kwa uchunguzi? Swali hili itabidi tumulize Kaimu kamishna mkuu wa Upelelzi ndugu Fred Nzoe inakuwaje watu wake waliopo hapo kiwanja cha ndege cha kimataifa kuwanyanyasa raia wema?
Kwa hivyo vitendo vyao vya kuzuia mizigo yao kwa huo muda wa mwezi mzima kwa kisingizio cha kuvichunguza hivyo vitu?
Hayo yametokea kwa rafiki wangu alie toka nje hivi karibuni kafanyia hivyo na kila akienda huko Kiwanja cha ndege cha kimataifa cha hapo Dares-Salaam anazungushwa mara aambiwe kuwa Mkuu wa kituo wa Polisi hayupo njoo keshokutwa na akienda hiyo kesho kutwa hurushwa tena njoo tena kesho kutwa hii kweli ndugu zangu wana JF na Viongozi wa Serikali wanaohusika tutaendelea kweli?
Kwa fikira zangu hao wanaohusika hapo Aiport inaonyesha wanataka Rushwa wapewe pesa ili wapate kumuachia huyo Rafiki yangu vitu vyake walivyovizuia bila sababu yoyote ile ya maana. Je Ndugu Wana JF Mnalichukulia vipi hilo suala na hivi karibuni Mheshimiwa ndugu Rais wa nchi yetu JM Kikwete aliwakemea maofisa wa kuzuia rushwa wawajibike kikazi sasa ikiwa Mapolisi wetu wa kipelelezi wanamzungusha huyo rafiki yangu kumpa vitu vyake sasa inapata mwezi hawajibiki, je hao aliowakemea Ndugu Rais JM Kikwete maofisa wa kuzuia Rushwa wanafanya kazi gani?
Ningeomba mnisaidie hilo tatizo langu maoni yenu ndugu wana JF wenzangu asanteni sana.