Anonymous
Senior Member
- Feb 3, 2006
- 125
- 321
Ndugu ZANGU,
Mimi kimajukumu ni mchungaji wa Kanisa hapa Dar es Salaam.
Napenda kueleza uma masikitiko yangu juu ya ofisi za uhamiaji (immigration) zilizopo kurasini.
Baadhi ya maofisa wa Immigration hapo wamekuwa na vitendo vya wazi vya kuomba rushwa ili kukupatia huduma kwa wakati. Na usipo kubali basi wata hakikisha unazungushwa kupata huduma na mwishowe utajikuta umeingia gharama kubwa.
Mfano; Mimi na mke wangu tulikwenda kwaajili ya kupata pasi za kusafiria, tumezungushwa sasa mwezi mzima na hakuna sababu yeyote ya msingi. Ila kwa ujasiri afisa anakupa namba umpigie simu na nilipopiga waliomba rushwa kwa ujasiri kabisa ili nipate passport yangu.
Nilipokataa kutoa, mpaka leo ninapo andika mwezi umeisha nimeenda zaidi ya mara tatu, Kila baada ya wiki moja na sijapata passport yangu. Katika upelelezi wangu kupitia wateja wengine, ndipo niligundua huu ni mchezo wao wa rushwa ya wazi wazi kabisa.
Ningependa mamlaka husika zichukue hatua, TAKUKURU, wizara ya mambo ya ndani na Jeshi la Polisi as well .
Nilitakuwa niwe nimesafiri sijafanikiwa, ratiba imevurugika ya safari, nazidi kuingia gharama. Kila nikienda ninapigwa tarehe, njoo siku fulani, njoo siku fulani. Na nikija naambiwa tu bado bado, huku naombwa rushwa!
Tupaze Sauti zetu Kukomesha uovu huu katika ofisi za UHAMIAJI. Huduma Bora ni haki yetu , sisi ni walipa Kodi sio watoa rushwa!
Mimi kimajukumu ni mchungaji wa Kanisa hapa Dar es Salaam.
Napenda kueleza uma masikitiko yangu juu ya ofisi za uhamiaji (immigration) zilizopo kurasini.
Baadhi ya maofisa wa Immigration hapo wamekuwa na vitendo vya wazi vya kuomba rushwa ili kukupatia huduma kwa wakati. Na usipo kubali basi wata hakikisha unazungushwa kupata huduma na mwishowe utajikuta umeingia gharama kubwa.
Mfano; Mimi na mke wangu tulikwenda kwaajili ya kupata pasi za kusafiria, tumezungushwa sasa mwezi mzima na hakuna sababu yeyote ya msingi. Ila kwa ujasiri afisa anakupa namba umpigie simu na nilipopiga waliomba rushwa kwa ujasiri kabisa ili nipate passport yangu.
Nilipokataa kutoa, mpaka leo ninapo andika mwezi umeisha nimeenda zaidi ya mara tatu, Kila baada ya wiki moja na sijapata passport yangu. Katika upelelezi wangu kupitia wateja wengine, ndipo niligundua huu ni mchezo wao wa rushwa ya wazi wazi kabisa.
Ningependa mamlaka husika zichukue hatua, TAKUKURU, wizara ya mambo ya ndani na Jeshi la Polisi as well .
Nilitakuwa niwe nimesafiri sijafanikiwa, ratiba imevurugika ya safari, nazidi kuingia gharama. Kila nikienda ninapigwa tarehe, njoo siku fulani, njoo siku fulani. Na nikija naambiwa tu bado bado, huku naombwa rushwa!
Tupaze Sauti zetu Kukomesha uovu huu katika ofisi za UHAMIAJI. Huduma Bora ni haki yetu , sisi ni walipa Kodi sio watoa rushwa!