Uoga wa Serikali/CCM

Uoga wa Serikali/CCM

Hii issue ya kutokea vurugu Upanga HQ camp iliyopelekea askari MT109795 Ramadhani mlaku kuuwa kwa risasi askari aliyekua anamdhibiti asiltekeleze alilokusudia aitwae MT 79512 Sgt munyama ndio limewekwa waZi jana baada ya Ramadhani kufikishwa mahakamani
Ramadhani alidhbitiwa kwa kukanyagwa na kifaru cha dereya miguuni

Sasa tunasubiri miezi sita ijayo kuwekwa wazi kilichotokea lugalo juzi@jf where we dare speak openly

Ndio maana tunasema things are wrong somewhere let’s pray for this country
IMG_1256.JPG
IMG_1255.JPG
 
Hapo kwenye lugha naweza kubaliana nawe.
Je hauoni nia ya wataka maandamano imefikia pahala pake japo si kwa asilimia zote, nia ya maandamano ni kuvusha ujumbe hata yasipokuwepo (BUSARA ZA VIONGOZI KUSHUGHURIKIA MATATIZO YA KIFAMILIA). Sijui mnaelewaga
 
Hayo ni maandamano ya kwenye mitandao ya kijamii ila ukweli hakuna kitu kama hicho. Time will tell. Nakumbuka siku ile pale kinondoni mkuu wa maandamano alitoweka kama kivuli.
Yupi
 
Ni mara kadhaa sasa nimeona na kusikia watu wakisema kuwa eti serikali inaogopa.

Kwamba inaogopa maandamano yanayopangwa kufanyika tarehe 26 mwezi Aprili.

Watu wasemao hivyo wanasema hivyo kwa sababu wamejiaminisha kuwa kama serikali ingekuwa haiyaogopi hayo maandamano basi baadhi ya viongozi wasingeyazungumzia hata kidogo.

Si ajabu hata hapa atajitokeza mtu atayesema kuwa hata mimi nayaogopa hayo maandamano na ndo maana nimeanzisha tena uzi unaoyahusu.

Sasa jana rais Magufuli naye kazungumzia watu kuandamana. Na si mara yake ya kwanza kufanya hivyo. Keshafanya hivyo mara kadhaa huko nyuma.

Magufuli kutaja neno ‘maandamano’ hiyo jana imekuwa nongwa. Watu wanataka kutuaminisha kwamba hayo maneno ya mitandaoni huko kuhusu hayo maandamano yanamnyima raha na usingizi rais kwa sababu mpaka yeye kayazungumzia hiyo jana.

Mimi sidhani kama serikali inaogopa. Ninachokiona ni serikali yenye watu wanaojua na kutambua kinachozungumzwa kwenye mitandao ya kijamii. Kujua na kutambua huko si uoga. Si kuogopa.

Kuogopa ni pale ambapo wale waliokuwa wanapiga sana kelele za maandamano kutokujitokeza na kuandamana siku ambayo walikuwa wamepanga kuandamana. Huo ndo uoga na huko ndo kuogopa.

Maana tayari wameshaambiwa ole wao waandamane. Wataenda kusimulia yatayowapata. Sasa siku ya siku ikifika na hakuna anayeingia barabarani, huko ndo kuogopa.

Lakini mtu kusema kuwa kasikia kuna watu wamepanga kuandamana au Ngabu kuja kuanzisha nyuzi hapa kuhusu hayo maandamano, sioni uoga hapo.

Kwa hiyo, mimi nadhani na naamini kuwa wote wasemao kuwa serikali inaogopa wanasema hivyo kujipa faraja tu.

Wanajiaminisha kuwa serikali inaogopa ili wajisikie vizuri tu. Wajione na wao kelele zao dhidi ya serikali zina athari ingawa kiuhalisia sivyo hivyo.
Maandamano ni kioo ujue mapungufu yako Watu wamezibwa midomo hakuna tena Habari za kiuchunguzi Bila Habari za kiuchunguzi huwezi kujua kila kitu km Kiongozi "A Country is Not a Company"
 
Back
Top Bottom