Mikopo Consultant
JF-Expert Member
- Oct 28, 2024
- 2,287
- 4,517
Kuyaruhusu na kuyarahisisha maandamano, ndo mbinu nzuri ya kuzuia machafuko yanayotokana na maandamano.
Maandamano yakifanywa kuwa kitu cha kawaida kwa watanzania; basi ustaarabu wa kuandamana utajengeka kwa watanzania; kwa makundi mbalimbali kwenye jamii (wafanyakazi, wanafunzi, wazee, vijana, watoto, wastaafu, wafanyabiashara) kuitumia ili kutoa madukuduku yao.
Kukiwepo sheria na miongozo, maana yake itaelekeza maandamano ya kundi fulani (mfano: wafanyabiashara) kwamba kama yanahusu kodi, basi eneo la kukutania liwe TRA, na ujumbe wa maandamano utapokelewa na kiongozi wa TRA. Vivo hivyo kwa wanafunzi, walimu, wastaafu, wasani n.k; miongozo na sheria itaonesha wazi namna yatavyoratibiwa na namna upande wa serikali utavyochukua ujumbe kutoka kwenye maandamano.
Kwa sasa, japokuwa maandamano yanaruhusiwa kikatiba, ila hayana miongozo iliyowazi; matokeo yake ni yale yaliyotokea MO29; yakawa ni maandamano ambayo serikali na waandamanaji wote wakajikuta wamevunja sheria na machafuko yalitokea.
Kukiwa na sheria na miongozo ya wazi; itakuwa ngumu sana kufika hatua ya kuwa na maandamano yenye machafuko.
Na pia, ukishaweka miongozo na sheria wazi za maandamano; hiyo itaongeza uwajibikaji wa taasisi za serikali ambazo ni walengwa wa maandamano, kama: TRA, Tume ya Uchaguzi, NECTA, Halmashauri, Tume ya Wastaafu n.k kwa sababu sheria itaweka wazi kwamba: viongozi wa taasisi ambazo ni walengwa wa maandamano, wanawajibika kupokea malalamiko ya waandamanaji na kutoa ahadi ya kutatua.
Ikiwa hivo, maandamano yatakuwa ni chanzo kuzuri cha utatuzi wa kero kwenye makundi mbali mbali ya kijamii. Na hii nafikiri ndo maono makuu ya mwandishi wa katiba ya JMT. Kile kifungu cha kuandamana hakikuwekwa pale bahati mbaya.
Mbinu inayotumika sasahivi: ya kuyanajisisha na kuyaharamisha maandamano, ni kutengeneza bomu la machafuko makubwa kwa Tanzania ya kesho, na ikumbukwe kwamba Tanzania ni nchi yenye ongezeko la kasi sana la idadi ya watu, maana yake, intensity ya bomu la machafuko ya maandamano litazidi kuwa kubwa kadri muda unavyozidi kusonga mbele. Kwa sababu, utajikuta hasira za makundi mbalimbali ya kijamii, zinaungana kwa pamoja, ndo sababu utajiuliza kwa mfano, ni kwanini ofisi za TRA ambazo hazihusiki na siasa, nazo zilipigwa kiberiti ile MO29? Hiyo wazi inakueleza ilikuwa ni hasira na kero za wafanyabiashara, walioutumia mwanya wa MO29 kutoa hasira zao.
Tunakosea kuona kwamba mtunga katiba alikosea; maandamano ni haki, na ni wajibu yawekewe sheria rasmi na miongozo.
Wenu
MC
Maandamano yakifanywa kuwa kitu cha kawaida kwa watanzania; basi ustaarabu wa kuandamana utajengeka kwa watanzania; kwa makundi mbalimbali kwenye jamii (wafanyakazi, wanafunzi, wazee, vijana, watoto, wastaafu, wafanyabiashara) kuitumia ili kutoa madukuduku yao.
Kukiwepo sheria na miongozo, maana yake itaelekeza maandamano ya kundi fulani (mfano: wafanyabiashara) kwamba kama yanahusu kodi, basi eneo la kukutania liwe TRA, na ujumbe wa maandamano utapokelewa na kiongozi wa TRA. Vivo hivyo kwa wanafunzi, walimu, wastaafu, wasani n.k; miongozo na sheria itaonesha wazi namna yatavyoratibiwa na namna upande wa serikali utavyochukua ujumbe kutoka kwenye maandamano.
Kwa sasa, japokuwa maandamano yanaruhusiwa kikatiba, ila hayana miongozo iliyowazi; matokeo yake ni yale yaliyotokea MO29; yakawa ni maandamano ambayo serikali na waandamanaji wote wakajikuta wamevunja sheria na machafuko yalitokea.
Kukiwa na sheria na miongozo ya wazi; itakuwa ngumu sana kufika hatua ya kuwa na maandamano yenye machafuko.
Na pia, ukishaweka miongozo na sheria wazi za maandamano; hiyo itaongeza uwajibikaji wa taasisi za serikali ambazo ni walengwa wa maandamano, kama: TRA, Tume ya Uchaguzi, NECTA, Halmashauri, Tume ya Wastaafu n.k kwa sababu sheria itaweka wazi kwamba: viongozi wa taasisi ambazo ni walengwa wa maandamano, wanawajibika kupokea malalamiko ya waandamanaji na kutoa ahadi ya kutatua.
Ikiwa hivo, maandamano yatakuwa ni chanzo kuzuri cha utatuzi wa kero kwenye makundi mbali mbali ya kijamii. Na hii nafikiri ndo maono makuu ya mwandishi wa katiba ya JMT. Kile kifungu cha kuandamana hakikuwekwa pale bahati mbaya.
Mbinu inayotumika sasahivi: ya kuyanajisisha na kuyaharamisha maandamano, ni kutengeneza bomu la machafuko makubwa kwa Tanzania ya kesho, na ikumbukwe kwamba Tanzania ni nchi yenye ongezeko la kasi sana la idadi ya watu, maana yake, intensity ya bomu la machafuko ya maandamano litazidi kuwa kubwa kadri muda unavyozidi kusonga mbele. Kwa sababu, utajikuta hasira za makundi mbalimbali ya kijamii, zinaungana kwa pamoja, ndo sababu utajiuliza kwa mfano, ni kwanini ofisi za TRA ambazo hazihusiki na siasa, nazo zilipigwa kiberiti ile MO29? Hiyo wazi inakueleza ilikuwa ni hasira na kero za wafanyabiashara, walioutumia mwanya wa MO29 kutoa hasira zao.
Tunakosea kuona kwamba mtunga katiba alikosea; maandamano ni haki, na ni wajibu yawekewe sheria rasmi na miongozo.
Wenu
MC