Augustine Moshi
JF-Expert Member
- Apr 22, 2006
- 2,554
- 1,382
Mzee Mwanakijiji leo nitakujibu kimjini-mjini kidogo. Nitajibu baadhi tu ya hoja zako.
Wewe sasa Mzee Mwanakijiji sijui unataka nikueleweje! Yaani unataka universal college education? Bado tunataka kufikia universal secondary education. Huenda tukafikia kipindi cha elimu ya juu kupatikana kwa kila awazaye, lakini sio kila atakaye. Wengine wanataka lakini hawawezi (hazipandi).
Najua Msuya alisema "kila mtu abebe Msalaba wake" lakini mtu anapoanguka chini ya Msalaba wake inabidi Simeoni wa Kirene alazimike kubeba naye.
Migomi isiyo ya lazima ilitokea lini? Inayotokea sasa yote ni ya lazima. Kama huu wa sasa wa UDSM ulikuwa wa lazima sana. Yaani serikali ina pesa za kupeleka ndege 7 kuzika mtu mmoja halafu inakosa vijishilingi vya kuwapa wanafunzi elfu 20 ada! Mbona ukiwapa watoto elfu 20 shilingi milioni 4 kila mmoja zinafikia jumla ya shilingi bilioni 80 tu! Hizo ni chini ya kiasi kinachochotwa BoT kila mwaka!a. Migomo isiyo ya lazima isitokee
Elimu ya Juu inapatikana kwa kila atakaye
Wewe sasa Mzee Mwanakijiji sijui unataka nikueleweje! Yaani unataka universal college education? Bado tunataka kufikia universal secondary education. Huenda tukafikia kipindi cha elimu ya juu kupatikana kwa kila awazaye, lakini sio kila atakaye. Wengine wanataka lakini hawawezi (hazipandi).
Kusomesha taifa la kesho si jukumu la familia peke yake. Lazima serikali iendelee kutumia kodi zetu kusomesha watoto wote wenye uwezo. Wazazi watachangia, lakini sii jukumu lao tu. Na nakubaliana na mwenzetu aliyeshutumu tabia ya sasa ya kuchangia sherehe na mazishi tu. Lazima kuchangia elimu. Viko vikundi vya michango ya kuzikana, lakini sijasikia kikundi cha michango ya kusomesha. Kuna kosa hapo.Familia zinaweza kumudu elimu ya juu
Najua Msuya alisema "kila mtu abebe Msalaba wake" lakini mtu anapoanguka chini ya Msalaba wake inabidi Simeoni wa Kirene alazimike kubeba naye.