Undani wa John Mnyika na John Heche

Undani wa John Mnyika na John Heche

Karibu tena mkuu,
Nimependa namna ulivyojitolea kuwaelezea hawa Vijana wawili wa kisiasa ndnai ya CHADEMA.
Namimi nakuunga mkono mkuu kwamba wanatakiwa kutiwa moyo na kupewa nafasi zaidi ili wakieneze chama kwa mapana zaidi.
LAKINI MKUU,KATIKA UCHAMBUZI WAKO UMEAINISHA MAFANIKIO,CHANGA MOTO NA RAI YAKO KWA VIONGOZI WA CHADEMA.
Naomba niongeze hili katika uchambuzi wako,kwamba hawa vijana wawili wanaoonekana kushabihiana
WANAMAPUNGUFU HAYA HAPA,AMBAYO NI MUHIMU WAKAYAFANYIA KAZI

1.John Mnyika anafanya vizuri ndani ya JImbo lake kwa kiasi flani.lakini ili aweze kufanikiwa zaidi basi ni Muhimu akajitenga na siasa za kuattack watendaji wa serikali na kuwatolea amri iliwatimize shughuli za maendeleo ya jimboni mwake.
Kwa mfano>alipotoa masaa 48 maji yawe yanatoka jimboni kwake kwa watendaji wa DAWASCO hakuwa angalia kwamba yeye ni mwnasiasa na anowambia ni watendaji wa serikali.
Kwa maksudi wanaweza kumuangusha katika kufanikisha kile alicholenga kukifanya.
Pia mnyika anapaswa kuangalia namna anavyowaweka viongozi wake wa juu katika upeona upokeo wa kimatendo na kiushirikiano.Yeye ni mwanasiasa kijana sana na muda mrefu kwenye ulingo huu,basi kwa nafasi yake inatakiwa aangalie namna navyowatreat kinidhamu na kiutendaji kazi hawa viongozi wajuu wa chama.Hizi kelele tunazosikia nyuma ya pazia kwamba anatumika,au anamkubali sana mtu flani si jambo jema kwa ustawi wa chama.

2.John Heche akiwa kama wenyekiti wa BAVICHA bila kusuasua napenda kusema kunambo mengi ndani ya Baraza lake yamekwenda kombo.
John heche anatakiwa achukue hatua kuhakikisha yeye na makamu wake wanakuwa kitu kimoja.Hivi sasa nakili wazi viongozi hawa wawili wanaongea na kucheka kama binadamu lakini mioyoni mwao wanatofauti/mpasuko kubwa sana ya kiutendaji.
Heche anakambi yake(sitaki kuitaja) naye makamu mwenyekiti anawatu wake.Hii kwa uhai wa Baraza ni hatari sana,lazima Heche ajitambue kwamba yeye ni kiongozi mkubwa basi hana cha kusubiri zaidi ya kuhakikisha mambo yana kaa sawa.
Pia Heche tangu aingie madarakani kunajambo amabalo sijajua ama maksudi au kwa bahati mbaya ameamua kulitupa,kuliacha,kulitelekeza na kuto litupia macho kabisa ili hali ndio muhimili wa Vijana wasomi ndani ya chadema,Ndio shamba la kuvuna vijana wasomi wa chadema,Ndio chuo cha kuzalisha viongozi wa somi ndani ya chadema...Swala hilo ni CHASO.
CHASO-CHADEMA STUDENT ORGANIZATION imetelekezwa,haipo pamoja,inajikongoja.Karibia vyo vyote vya juu vya elimu ya kati vina vijana wa chadema ambao wamejikusanya kwa jitihada zao,wanajiongoza wanakiu ya ukombozi kupita maelezo.
Lakini baraza la vijana la chadema chini ya John Heche limeshindwa kuwaunganisha vijana hawa.hakuna uongozi wa CHASO kitaifa,Hakuna anayetambua viongozi wa chaso wanaomaliza muda wake wanakenda wapi?Heche hajui yawezekana hata idadi ya matawi ya chaso ndani ya chadema.
JOhn heche hatembelei kufungua matawi ya chaso,Heche hatembelei kuangalia Vijana hawa wa chasso kwenye matawi yao wanakabiliwa na matatizo gani.
John heche jitizame kama umekamilika kuhusu hili,CCM wanalia kuna vijana wanaharakati na wanamapinduzi wasomi wote wanakimbilia CHASO.Vijana wa chaso wanatikisa chaguzi mbalimbali za Urais vyuoni mwao.Lakini je wanaandaliwa mazingira gani ya kukua kisiasa ndani ya baraza la Vijana?
Lakini mwisho,John heche naomba tumie akili yako na ya wenzako,Kuna haja gani ya kendekeza makundi ndani ya barza la vijana?kwanini kwenye mikutano yako hutoi nafasi kwa vijana flaniflani ambao wanaonekana hawapo upande unaouamini ndani ya chama?Weweni kiongozi hutakiwi kuegamia upande wowote..Lakini kesi za kugoma kutoa maiki za kuhutubia mikutanoni kwa vijana flani zimekuwa nyingi sana.
Je kuwanyima maiki ndio suruhisho la mogogoro wako na wao?Je BAVICHA inaundwa na vijana wa upande mmoja?
asanteni.

Ni hayo tu​

Mkuu tuntemeke hivi ndivyo twajenga chama kwa hoja za kutambua udhaifu na how to fix.nakupa pongezi kwa mawazo yako ya kujenga chama na kiukombozi.
 
Mkuu,
Kwenye red hapo ndipo msimamo wangu ulipo kwamba,Kila kiongozi anamakosa yake tena hawa wa kisiasa ndio kabisaa wanamakosa mengi sana.Hivyo basi tuwakosoe kwa hoja,tuwakosoe bila kujali itikadi ya chama,maslahi ndani ya chama,Umaarufu wake kwa taifa hili.
Hapo kwenye blue nakuunga mkono matusi si fungu jema katika kusimamia jambo lolote,na sheria za JF haziruhusu.
Napinga matusi,naunga mkono hoja kwa hoja.

Mkuu nimekuelewa vema.
Thread hii ya Fmpiganaji ifungue ukurasa mpya kwa mijadala ya staha hapa JF.
Iwe mwiko kwa mwanaJF kujadili maisha binafsi ya watu hapa jamvini.Mambo hayo yabaki kule FB.Ni imani yangu tukiwakosoa viongozi kwa staha watagundua makosa yao kwani kwa hakika hakuna aliye malaika.
Mtu kama Ben anasifiwa leo hapa JF kwa heshima yake kubwa aliyojijengea kwa viongozi na wanachama wenzake.
Inatakiwa kila mtu aheshimu mchango wa mwenzake ndipo na yeye ataheshimiwa.
Again Keep in touch.
 
kama huo ndo utafiti inabidi vyuo vya utafiti vifungwe. huo ni ushabiki.

Kama alilenga kuwa analyse............nasikitika hakuweka weakness zao ili wajijienge zaid......katuwekea changamoto!!!!!!!!

Ndo maana kuna mchangiaji kahoji motive ya hoja hii
 
Ha ha hahaaaaaaaaaaaaa.watu bana.umeona jinsi hawa jamaa uliokua ukiwatukana kila siku walivyojadiliwa kwa ustaarabu ukashindwa kuvumilia

Hongera kwa kuandika busara leo.
Moderators walikuumbua juzi kwa kuunganisha ID uliyotumia kumtukana Ben,Mnyika na Heche matusi ya nguoni kwa ID ya Libasket

Jack kumbuka kuwa ili uwe mjadala chanya lazima kuweko ukinzani,tulipenda mjadala ujikite kwenye hoja na moja ya kuushinda ujinga ni kuonesha werevu.mimi nawe tulipenda tujadiliane kwa hoja na si matusi nashukuru pia mwenzetu tuntemeke amekuwa pamoja nasi na kwakweli huu ndio ukomavu wa kisiasa na demokrasia kwa ujumla.nimemuunga mkono juu ya kujadili ktk misingi ya kutambua makosa ya viongozi wetu,kuwakumbusha wajibu wao wanapojisahau na mwisho kuleta njia mbadala za kurekebisha na kujenga chama.nafahamu ili kupata mabadiliko ya kweli lazima turekebishane wenyewe ndipo tupate nguvu ya kuwabadilisha wengine na kwa hili tunakwenda vizuri.
 
Kama alilenga kuwa analyse............nasikitika hakuweka weakness zao ili wajijienge zaid......katuwekea changamoto!!!!!!!!

Ndo maana kuna mchangiaji kahoji motive ya hoja hii

Mkuu Olesaidimu
Fmpiganaji kaleta hoja jamvini.Ni kazi yetu sasa wanaJamvi kuongezea nyama.Kama kuna weakness zao unapaswa kuziweka wewe bila kumlazimisha mleta mada kuziweka,inawezekana yeye hajaziona.Pia ukifuatilia hii thread tangu jana utagundua Fmpiganaji yuko very Positive kwa kila hoja ya ziada inayoletwa na wanajamvi kuhusu mada yake.
Nadhani umenipata mkuu.Let us be GT.
 
Mkuu Molemo mtoa mada kafanya uchunguzi kwa miezi nane......he is better positioned kutoa na weakness zao na kama hwana alitakiwa aseme hawana ila kwa kusema mimi niziweke hapa si sawa sana


Mfano; nilisomsoma Ben Carson......alikuwa na weakness ya uoni hafifu alipogunduliwa na kutibiwa leo hii ni surgeon.....sasa bila ya kugundua weakness ya mtu uliyemtafiti bado kuna kazi ya kufanya ili kumjenga vizuri kwa manufaa ya umma........je hawana mapungufu??????
 
Mkuu wangu bado unataka katiba ibadilishwe ili ugombee urais? unaonekana hutaki vijana wengine ndani ya CHADEMA waibuke kama ulivyoibuka wewe.hujui wewe kutangaza nia ya urais ulichangia pia chama kupungukiwa kura?

NDIO nataka
 
Tuntemeke kwa mara ya kwanza umeonyesha ukomavu inatakiwa wote tuwe hvyo 2jadili,tutoe mapunguvu kwa hoja sio matus 2we pamoja kwa hili kw maslah ya chama na Taifa kwa ujumla
 
Ustaadh,

Asante sana.Siku zote BAVICHA ni kubwa kuliko Ben Saanane na Heche.Sote tunaongozwa na dhamira ya Chama kuchukua Dola na kusimamia mchakato wa mabadiliko.Sote tuna common Enemy.Ni lazima tukabiliane naye kwa umoja

Ni muda muafaka zaidi kwetu kubadili mtazamo na kukumbatia siasa za mazoea,hatutaki siasa za kugombani fito na kuachana na ajenda ya ujenzi.Hatutaki kumpa faida adui wa mabadiliko .Tukifanya hivyo tutakua tumejidhoofisha sisi,tumewakatisha tamaa vijana na kumpa nguvu adui yetu

Kuhusu watu wengine,Sitawajadili

Haswa huyu jamaa nyakarungu huwa naona post zake fb amekuwa ni mtu wa ajabu na inaonyesha wazi ana kitu anachokijua mwenyewe ndani ya roho yake dhidi ya mwenyekiti Heche.
 
Mkuu laiti ningejua mwalimu wako aliyekufundisha ningeomba walau anipe Tuition kidogo kuhusu Analysis.Umetisha kwa analyisis yako.

Niongeze jambo moja tu ili nisiharibu uhondo wa mada yako.Kuhusu Ben Saanane nafarijika sana kumuona jinsi alivyo mkomavu.Nimekuwa nikifuatilia Post nyingi za Ben hakika ni mtu mwenye heshima ya hali ya juu kwa viongozi wote wa CDM.Na pia ninapenda sana pale anapotetea CDM kama Taasisi na siyo makundi ya ufuasi.Ninapenda sana viongozi kukosolewa lakini siyo kumkosoa kiongozi wako kwa matusi ya nguoni kama muhuni.Kama Ben ni matunda ya Mnyika na Heche basi nawapa hongera sana na naunga mkono mada hii 100%.
Mkuu Molemo,
Asante sana kwa post yako hii.Inatia moyo sana.

JF ilikua na wachangiaji wenye hoja nzito na post za matusi kipindi hicho ukiweka hapa watu wangekushangaa.Tumeingiliwa siku za karibuni lakini naona miezi michache iliyopita mambo yamebadilika

Hii ni social forum.Imeanzishwa kwa ajili ya kuunganisha watanzania popote walipo ili kujadili mustakabali wa Taifa lao

Busara ya matumizi ya Forum hii na nyingine ni kwamba ukiona huna cha kuchangia ni bora ubakie kuwa msomaji tu

JF inasomwa na watu wengi.Hili ni soko la weledi,ni kisima cha fikra huru.

Naamini kwa mwanasiasa yeyote kijana atakayetumia jukwaa hili kuchafua viongozi au wanachama wenzake hawezi kukubalika na jamii yoyote ile.Hata CCM au vyama vingine hawataweza kukuheshimu kwa matendo kama hayo

Kuna hoja za kukosoa ili pia kupata maoni ya wengine katika kujikomaza zaidi kifikra au kutumia maoni hayo kukijenga chama chetu zaidi

Tuna wajibu wa kulinda malengo yetu ya mabadiliko.Sometimes people are so feeble,blinded by religious or sectarian bias.We should discarauge this evil spirit

Yeyote anayemtukana kiongozi wa CHADEMA au Mwanachama wake na kujifanya Mwanachadema huyo hafai.Yupo kinyume nasi

Tuendeleze mapambano yetu ya fikra.

Once,Again thank you Molemo,thanks JF family
 
Haswa huyu jamaa nyakarungu huwa naona post zake fb amekuwa ni mtu wa ajabu na inaonyesha wazi ana kitu anachokijua mwenyewe ndani ya roho yake dhidi ya mwenyekiti Heche.

Mkuu wangu Kijome

Soma Post yangu #38 imejibu hii hoja yako.
 
..........."KAZI YA KICHWA SI KUFUGA NYWELE TU".........(Jaji Werema), nikikumbuka maneno haya halafu nikifikiria na hoja za marais wajao zinavyojadiliwa humu basi huwa naheshimu sana misemo hii maana mtu anaweza kupenda mtu au chama basi akawa anatumia kichwa chake kufugia nywele...........
 
WanaJF,
Ben Saanane,kwa wanaofuatilia siasa zake watagundua kwamba ni kijana anayeonyesha uvumilivu wa hali ya juu.Ben Saanane amewahi kupata misukosuko ya kisiasa lakini alisimama imara kutetea anchoamini.Hakuwahi kukashifu viongozi wake wa chama katika uficho au kwa uwazi.Ben anaamini CDM kama taasisi imara na siyo makundi ya watu.Ninaweza kusema Ben Saanane ni matunda ya kazi nzuri za kina Mnyika na wenzake.Hata hivyo chama kiandae vijana wengi zaidi wa kufuata nyayo za kina Mnyika na Heche na siyo Ben Saanane tu...

WanaJF Karibuni kwa mjadala!

Hii nimeipenda zaidi....Hakuna kitu kikubwa katika maisha ya kijamii kama HESHIMA na UTII...
 
Tuntemeke kwa mara ya kwanza umeonyesha ukomavu inatakiwa wote tuwe hvyo 2jadili,tutoe mapunguvu kwa hoja sio matus 2we pamoja kwa hili kw maslah ya chama na Taifa kwa ujumla

Status Report inaonesha Meseji Sent and Derivered.
Hoja ndio uhai wa jukwaa.
Lakini ifahamike wazi,kumkosoa kiongozi yeyote awe wa chadema,cuf,ccm n.k kwa misingi ya kisiasa sio tusi,sio kwamba unamchukia.But amejikwaa ni lazima akosolewe.
asante.
WE CAN HAVE ELECTION WITHOUT DEMOCRACY,BUT NOT DEMOCRACY WITHOUT ELECTION
 
Status Report inaonesha Meseji Sent and Derivered.
Hoja ndio uhai wa jukwaa.
Lakini ifahamike wazi,kumkosoa kiongozi yeyote awe wa chadema,cuf,ccm n.k kwa misingi ya kisiasa sio tusi,sio kwamba unamchukia.But amejikwaa ni lazima akosolewe.
asante.
WE CAN HAVE ELECTION WITHOUT DEMOCRACY,BUT NOT DEMOCRACY WITHOUT ELECTION
Sio kuwakosoa 2 kw hoja na kuwashauri kwa hoja na kwa misingi ya kisiasa si vinginevyo
 
Mkimaliza kujadili hii,mje mtuambie kwanini katika uchaguzi uliopita wa madiwani mmeambulia kata 5 tu!,ingawa mmefanya kampeni kubwa sana kila sehemu husika,kwa kutumia fedha za mzee sabodo.

hiv wewe unaamini katika idadi ya madiwani bila kuangalia hao madiwani wenu wametoka katika kata gani na idadi ya wapiga kura na aina ya wapiga kura. Madiwani wenu wamepigiwa kura na watu mliowahongahoga kama kawaida yenu dio mkapata namba kubwa ya madiwani. Hivi kweli unaweza kupata madiwani 5 kura 20000 na zaidi kwa viti 22 kura 29000: tofauti viti 17 kura 9000: acha majigambo.
 
Mnyika & Heche wame-inspire watanzania wengi kupenda mabadiliko. Pamoja na magumu kibao,wameendelea kuonyesha ukomavu wa kisiasa,
 
Captain Green,

Sikutaka kujibu hizi post zako lakini unazidi kupotosha.

Sikuwahi kuingilia uchaguzi wenu.Kuna wagombea huko ambao walikua marafiki zangu wa Kawaida kama Felician na wengine.

Vijana tuache siasa hizi za uadui na kupanfikiziana chuki pasipo sababu

Nakushangaa unapojisifu kwamba BAVICHA haiwezi kupambana na UVCCM ya hao uliowataja bila kugusia ushiriki wako katika kugakikisha wanapita kwa Rushwa

BAVICHA ni nguzo muhimu kwa chama katika kupambana na ufisadi.Uongozi huo ni matokeo ya ufisadi utaweza vipi kusimama mbele ya vijana pale Machinga Complex na kuwahubiria vijana wajunge na UVCCM? Uongozi huo mpya ambao wewe umesimamia mchakato wa rushwa kuhakikisha wanashinda utaweza vipi kuwakemea vigogo wauza madawa ya kulevya wanaowatumia vijana? Je,hao wasomi wanaolalamikiwa na wenzao kutumika watashindwa vipi kutumika katika utungaji au utekelezaji wa sera na miradi ya kifisadi?

Je,wataweza vipi kusimamia sera ya kuwa na Baraza huruvla vijana la Taifa ambalo litakua mwiba kwa wakandamizaji wa vijana katika sekta zote?

Je,watawezaje kukosoa au kushauri sera inayopingana na utekelezaji wa kilimo kwanza kitakachowafanya vijana kuwa manamba kwenye mashamba makubwa?

Je,kipindi hiki ambacho tumegundua nishati ya Gesi,hivi kweli uongozi uliopatikana hivi utaweza kuwa objective katika utungaji wa sera ya gesi kwa manufaa ya vijana wa sasa na watoto wetu?

No,kwa maoni yangu naona vijana wa aina hii hawana ajenda za vijana bali wana ajenda za wazee wao waliolifikisha taifa hapa.

Vijana hao wamethibitisha jinsi wanavyokomazwa na Rushwa ndani ya chama chao kwa ushirikiano wa karibu kutoka kwa kaka zao na wazee ndani ya hicho chama

Ni jukumu la BAVICHA kuwaokoa vijana na hata hao vijana wa UVCCM ambao wapo ndani ya hicho chama kwa maslahi tu,tutawakomboa kifikra.Hata wewe mkuu siku moja utakuja tu CHADEMA.Tutakukomboa hata wewe kifikra

Unasema wamehongwa kwa kua mamluki wako tuliwaengua
Mbona BAVICHA hatujawasikia wakiongelea baraza huru la vijana?
Nina haki ya kujisifu nimeacha jumuiya iliyosimama.Mnyika alikuja na hoja kama hizi akiwa mwenyekiti wa vijana huko kwenu lakini kimya baada ya kuupata ubunge.Hata wewe utakua hivyo
 
Back
Top Bottom