Ben Saanane
JF-Expert Member
- Jan 18, 2007
- 14,580
- 18,222
Hapo ndipo napoanza kuamini wote ni wababaishaji tu si chama kilichoko madarakani wala vyama vya upinzani, Kama hakuna chama cha upinzani kitakachothubutu kuonyesha njia kwa vitendo,vitakuwa na umaarufu lakini haviwezi kuaminika kwa wanyonge hata siku moja, siwezi kushawishika kwamba CDM hawana uwezo wa kuonyesha utendaji kwa kuchagua mambo muhimu yanayowagusa wanyonge waliowengi na kuwasaidia, eti mpaka wasubiri waingie Ikulu wakusanye Kodi, haya ni mawazo ya Utopia!! UNAPOKUTANA NA MTU ANALIA KWA USTAARABU TU WA KAWAIDA KABISA UNATOA KITAMBAA CHAKO CHA MFUKONI UNAMPATIA AFUTE MACHOZI.." sio unamsaidia kulia.
Kwa kiwango chochote wanachopata CDM ikiwa ni ruzuku, misaada kutoka kwa chama rafiki,michango ya wanachama,harambee, michango ya wabunge na "fundrising" yote hiyo wanapaswa waanze taratibu kuchagua mambo muhimu wasaidie wananchi, wanajiandaaje kuongoza nchi hawajui kuwahudumia wananchi? Napata taabu sana kutahmini ikiwa kuna watu makini Tanzania wenye nia ya dhati na utashi wa kuwatumikia watanzania ikiwa kuna watu bado wana fikra kama zako!!
Kitendo cha kuwa shupavu na mahiri katika kulalamika na kueleza udhaifu wa chama, serikali ama mtu mwingine sio dalili ya kuwa na nia safi ama utashi wa kuwatumikia watanzania, tutahitaji tujiridhishe kwa historia yako katika kuwasaidia watanzania,na watanzania wa leo wamechoka kusikia Blah....blah....blah! ikiwa watanzania wamekata tamaa basi wewe uanayejinasibu kuwa mkombozi wao utembee katika maneno yako!! ''SIO KUHUBIRI MAJI KISHA WEWE UNAKUNYWA MAZIWA'' ni unafiki mkubwa na kamwe huwezi kuaminika hata kidogo.
Lengo la chama cha upinzani ni kukosoa na kutoa mawazo mbadala na kuonyesha wao wakichukua dola watafanya nini kizuri zaidi
Si malengo ya chama cha upinzani kubeba majukumu ya serikali inayokusanya kodi.Lengo la upinzani kuonyesha sera na mipango sahihi zaidi itakayoleta tija kwa wananchi wake
Harakati za CHADEMA hazina tofauti na harakati za TANU kumuondoa mkoloni aliyeko madarakani.Ni harakati za kumuondoa mtawala aliyebweteka na kutumia jasho la wananchi kwa maslahi ya wachache
CHADEMA kama ilivyokua TANU kina jukumu la kuwaamsha wanyonge na kuunganisha nguvu dhidi ya mfumo mbovu unaosimamiwa na watawala wasiojali raia wake kama ilivyokua kwa TANU ambayo ilikua haikusanyi kodi lakini iliunganisha nguvu kuongoza mabadiliko
TANU haikua na viongozi wenye uzoefu serikalini lakini walichukua uhuru na kuunda serikali kwa kutumia watumishi waadilifu waliokuwa wakiitumikia serikali ya kikoloni hivyo walisimamia sera na mipango chini ya serikali ya Nyerere.
Pia hoja ya uzoefu inazidi kuchuja.Chama cha The Dream huko Georgia kilianzishwa mwezi May lakini mwezi Oktoba kimechukua madaraka.Wananchi wamekiamini kutokana na elimu ya uraia
Pia hoja ya CHADEMA kupata ufadhili kutoka kwa Marafiki,kwani hujaona mradi wa maji wa Sabodo ambao CHADEMA iliombwa ipeleke mchanganuo?
Pia CHADEMA tunakoongoza halmashauri tunawaonyesha wananchi kile ambacho tutafanya tukiwa madarakani kutokana na mipango mizuri zaidi
Kazi ya CHADEMA bungeni inaeleweka na sijui kwanini unataka CHADEMA labda ijenge barabara ilihali unajua haikusanyi kodi