Undani wa John Mnyika na John Heche

Undani wa John Mnyika na John Heche

Hii nimeipenda zaidi....Hakuna kitu kikubwa katika maisha ya kijamii kama HESHIMA na UTII...

"Utii pasipo uhuru ni Utumwa. Na Uhuru pasipo Nidhamu ni Wendawazimu" J. K. Nyerere.
Ni angalizo tu mkuu!
Mungu wetu anaita!
 
"Utii pasipo uhuru ni Utumwa. Na Uhuru pasipo Nidhamu ni Wendawazimu" J. K. Nyerere.
Ni angalizo tu mkuu!
Mungu wetu anaita!

Mkuu,
Nakubaliana na wewe, lakini kwa maoni yako unadhani Utii uambatane na Mipaka? Msingi wa yote haya ni ile tabia ya vijana kutofautiana na viongozi wao na badala ya kupingana nao kwa hoja na kwenye vikao, wanakimbilia JF na FB kwa ID zao halisi au batili na kuanza kuwatukana viongozi wao. Tena matusi kabisa na kuwadhihaki na kuanza kujadili maisha yao binafsi...
 
Mkuu,
Nakubaliana na wewe, lakini kwa maoni yako unadhani Utii uambatane na Mipaka? Msingi wa yote haya ni ile tabia ya vijana kutofautiana na viongozi wao na badala ya kupingana nao kwa hoja na kwenye vikao, wanakimbilia JF na FB kwa ID zao halisi au batili na kuanza kuwatukana viongozi wao. Tena matusi kabisa na kuwadhihaki na kuanza kujadili maisha yao binafsi...

Mkuu wangu nimefurahi sana ulivyomjibu.
Unajua kitakachowaangamiza vijana wengi katika siasa ni kukosa subira na kutaka mafanikio kwa haraka haraka.Wanapokosa wanapata ghadhabu wanachanganyikiwa na kuangalia namna ya kuondoa stress zao.Sasa wanadhani kuondoa Stress ni kutukana viongozi matusi ya nguoni.Wakichoka kutukana matusi wanaanza kujadili maisha binafsi ya wenzao.
Ni wazi kwa mwendo huo vijana wa namna hiyo hawatafika.Watadhani watakimbilia vyama vingine au kuanzisha vyama lakini nawahakikishia watasambaratika kwa sababu hawataweza kukaa pamoja kwa tabia za namna hiyo.
Vujana wanapaswa kujifunza kitu kimoja,mafanikio waliyo nayo viongozi wakuu wa CDM Dr Slaa na Mbowe ni kutokana na uvumilivu wao wa kisiasa vinginevyo nao wangekuwa tu historia leo.

Vijana wanapaswa kubadilika sasa wakitaka mafanikio ya mbeleni.
 
Mkuu wangu nimefurahi sana ulivyomjibu.
Unajua kitakachowaangamiza vijana wengi katika siasa ni kukosa subira na kutaka mafanikio kwa haraka haraka.Wanapokosa wanapata ghadhabu wanachanganyikiwa na kuangalia namna ya kuondoa stress zao.Sasa wanadhani kuondoa Stress ni kutukana viongozi matusi ya nguoni.Wakichoka kutukana matusi wanaanza kujadili maisha binafsi ya wenzao.
Ni wazi kwa mwendo huo vijana wa namna hiyo hawatafika.Watadhani watakimbilia vyama vingine au kuanzisha vyama lakini nawahakikishia watasambaratika kwa sababu hawataweza kukaa pamoja kwa tabia za namna hiyo.
Vujana wanapaswa kujifunza kitu kimoja,mafanikio waliyo nayo viongozi wakuu wa CDM Dr Slaa na Mbowe ni kutokana na uvumilivu wao wa kisiasa vinginevyo nao wangekuwa tu historia leo.

Vijana wanapaswa kubadilika sasa wakitaka mafanikio ya mbeleni.

Mkuu japo umenidhania, lakini nikwambie tu, ulichosema hapo juu ndio lengo kuu la mifumo ya kudandia ovyoo ovyoo(Demokrasia)! Na usiseme vijana tu, utakuwa unaukimbia Ukweli, ni asilimia kubwa ya watu walio kwenye vyama, si wazee wala vijana, wote sawa tu!
Demokrasia ni Ushindani wa Hoja juu ya Sera na Falsafa! Ndivyo ilivyo kwa wenzetu(nje), kinachofanya waweze hilo ni "Condunssive Envirnment for Critical Thinking/Reasoning", anapokea hoja ya mtu critically, anaimeng'enya critically, mwisho anaijibu critically, aidha kwa kuipinga ama kukubaliana nayo! Ni mazingira yao yameruhusu wao kuwa hivyo! Naposema Mazingira yao namaanisha kila kitu chao, kuanzia uchumi, siasa na utamaduni wao!
MAZINGIRA HAYO HAYAPO KWETU! Mazingira yetu hayaruhusu TAFAKARI ZA KINA, ukianzia Kiuchumi, kisiasa na kitamaduni. Mfano mdogo tu: Mavyuoni, "mwanafunzi amecheleshewa posho yake kwa wiki zaidi ya 3, mama yake nyumbani mgonjwa anatarajia pesa hiyo kidogo akatibiwe(tu watoto wa mkulima), mkufunzi ametoa vitini asiyekuwa nacho haingii kwenye mtihani" mwanafunzi huyo anapoenda kuhoji, eti anajibiwa "kuwa mvumilivu tupe muda kidogo, c unajua hili na lile", akipata ghadhabu na kutukana ni kosa? Demokrasia inasema NDIO, nanyi ndiooooooo! Mama yake kesho anakufa, bado unataka ATII! Ni Wendawazimu! Mazingira yetu hayaruhusu siasa za kuvumiliana, tusingeivumilia CCM, labda leo mama wa huyu mwanafunzi angekuwa anasherehekea kuhitimu kwa mwanae!
UTII LAZIMA UWE NA MIPAKA! Haijalishi ni kwa nani, hata kwa baba na mama yako! Kuna jambo moja tu ambalo huwa halina mipaka, nalo ni MANTIKI! Halifungwi na chochote, hata damu ya mtu!
UTII kama UHURU, ni lazima uwe na MIPAKA ndugu SEBM!
Mungu wetu anaita sasa!
 
Ovyooo.hawa jamaa unaowasifia ni ovyo sana,kwanza sifa ya kiongozi mzuri anatakiwa awe intelligent,na msimamizi mzuri wa hoja.
Heche ni mtupu kichwan kasoma SAUT kwa kuungunga sana mpaka kumaliza,kama ndo hazina za cdm basi cdm nayo ni hoi kwelikweli.
 
Ovyooo.hawa jamaa unaowasifia ni ovyo sana,kwanza sifa ya kiongozi mzuri anatakiwa awe intelligent,na msimamizi mzuri wa hoja.
Heche ni mtupu kichwan kasoma SAUT kwa kuungunga sana mpaka kumaliza,kama ndo hazina za cdm basi cdm nayo ni hoi kwelikweli.

Hawa ndiyo wale watu wanaojishushia heshima na kuonekana watupu kichwani.
Mtu kaleta hoja yake wewe badala ya kujadili na kutoa hoja zenye mashiko unaleta mambo ya taarabu.Mmejikita kwa chuki binafsi bila sababu yoyote.
Kwa nini usisome tu na kukaa kimya kuliko kujidhalilisha?
 
Hivi inamsaidia nini mtu kila siku kumtaja mwenzake kwa kuzungumzia mambo yake binafsi?
Mambo binafsi ya mtu, mathalani John Mnyika ama Ben Saanane yana athari gani chanya ama hasi kwa ustawi wa Chadema?
Wasiwasi wangu ni kwamba Ben ameonyesha kupiga hatua kubwa sana kisiasa sasa kuna watu wanamuonea wivu na wanadhani njia ya kumkwamisha ni kuanza kuzungumzia mambo yake binafsi.
Mwanzoni kulikuwa na fununu mitaani kwamba vijana wote waliogombea Bavicha na kuenguliwa wameunda alliance ya kuushambulia uongozi wa Bavicha na Chadema kwa ujumla.
Kwakuwa Ben naye alienguliwa akatajwa kuwemo katika huo ushirika haramu. Kadri siku zinavyokwenda ukweli umebainika kwamba Ben hayuko nao bali amefocus kukijenga chama na si kujenga watu binafsi. Naona hii ndiyo inamletea shida kidogo lakini naona ameshaishinda hiyo vita kwani mwenye macho haambiwi tazama.

Ben hata mimi nampongeza sana mkuu kwa kushinda hiyo vita ya kuunganishwa na kina Habibu Mchange na Mwampamba, Huyu jamaa amedhihirisha usomi wake kwamba ni wa maana na Huyu jamaa ni lulu kwa taifa siyo tu kwa chama wakuu
 
Sina uhakika sana ikiwa utafiti wako hapo juu una ithibati, lakini naona nina hoja ya kuchangia,nitachepuka kidogo isipokuwa binafsi nitawachambua hao vijana kwa kujadili taasisi waliyopo (CHADEMA)

CDM kama chama kikuu cha upinzani hapa Tanzania kwa vyovyote vile lazima kikutane na changamoto lukuki katika harakati zake za kuingia ikulu, mara kadhaa nimekuwa nikimsikia Dr. Slaa akiwajibu mahasimu wake wa kisiasa (CCM) pale wanapolalama kwamba CMD muda wote wapo kuangalia mapungufu tu na kuyasema bila kutaja hata mazuri ya CCM, lakini yeye bila kumung'unya maneno alitoka na kusema wao CHADEMA hawapo kwa ajili ya kusifia mazuri ya CCM, maana kama ni mazuri hawaoni haja ya kuyataja.

Sasa kwa msingi huu, binafsi naona udhaifu mkubwa sana wa CDM kama sio wa Dr. Slaa, nafikiri huo ndo msimamo wa chama, hivyo BAVICHA ya kina Heche na wenzake wameendelea kulalamika kila kukicha kiasi kwamba kama utakuwa unafuatilia vizuri mikutano yao muda wote wanaeleza Rais kafanya nini....waziri kafanya nini..... wakati mwingine unaweza hata kubashiri mambo ambayo atakayoongea mara tu akianza.

My take: Siasa hizi zimepitwa na wakati, watanzania wamechoka kusikiliza watu wakilalamika tuuuuu! inapaswa sasa kwa uwezo mdogo walionao CDM waonyeshe kwa mfano; kama wanasema shule za kata hazina viwango, zitawaangukia wanafunzi hebu wajenge hata shule moja na wajinadi kwa kusema "Ikiwa tutaingia madarakani hizi ndo shule zenye viwango tutajenga" waseme na kutenda hivyo hivyo hata kwenye mambo kama visima vya maji, barabara za vijijini,zahati, ofisi za mitaa n.k

Kiukweli wananchi wamechoka kukusanyika kwenye mikutano wanapewa faraja ama machungu wanaporudi nyumbani kero ziko pale pale kwanza mkutano umewakawiza kwenda kutafuta kuni, kuchota maji maana ni ya shida, kwenda kutafuta vipimo zahati ya mbali,Inawezekana wanachoelezwa ni cha kweli lakini mwisho wa siku hawana jinsi zaidi ya kusubiri kipindi kingine cha uchaguzi waweze kufanya mabadiliko lakini pengine imebaki miaka 3 ndo uchaguzi mwingine sasa ndo kusema CDM wao watakuwa wakizunguka kulalamika tuuu! mi nadhani sio sahihi hebu watoke wafanye kwa mfano ndo njia peke itayowajengea imani na heshima kubwa kwa wapiga kula.

CHADEMA naweza kusema wamepanda mbegu mbaya sana kwa vijana wa kitanzania na watanzania kwa ujumla, Tabia ya kulalamika tuuuu na wengine sasa hata ukimuuliza kile acholalamika kwa kiasi gani ameona au anatambua athari zake, hajui chachote isipokuwa aliwahi kuwasikia viongozi wake wakilalamika, hii mbegu sio nzuri hata kidogo kuna wengine kabisa tunafahamu ugumu wa maisha yake sababu ni yeye mwenyewe lakini naye analalamika vijana au watu wa namna hii wapo kila kona ya nchi hii lakini ni lini hivi vyama vya upinzani vilisimama vikakemea vijana waache tabia ya kufanyiwa kila kitu? waache kukaa masikani na kusubiri maendeleo?

Kina Heche na Mnyika wamekuwa katika mkururo huo huo wa kulalamika tu kuonyesha madhaifu tu ya CCM na kusahau kuwaonyesha kwa mfano watanzania ni kipi wamefanya,najua watakuja watu wahoji juu ya fedha, lakini mi nasema wanaweza wakiamua, ujue CDM mpaka kimejipambanua kuwa ni chama kinachojengwa na matukio ni kweli kabisa!

Nilifarijika walau kwa mara ya kwanza kuona uongozi wa CDM( sikumbuki walikuwa ni wa wapi lakini sio makao makuu) walitoka na Greda kwenda kupanua nadhani mto msimbazi ili kusaidia wananchi waishio bonde la mto msimbazi wasipatwe maafa ya mafuriko, kitu kile ndo nataka iwe msimamo wa CDM Taifa na kila kiwango cha chama, mambo hayo ndo yatakayowajengea heshima kubwa na kuaminika zaidi kuliko kulalamika tu kila kukicha,mnawafundisha kitu kibaya sana watanzania kujipambanua nyie ni malaika siku ikitokea mkachukua nchi mbegu mlioipanda itawwatesa hata nyie wenyewe maana ndo mazoea! AKSANTENI.
hakuna chama cha siasa duniani chenye focus ya kufanya kazi za utekelezaji wakati hakikusanyi kodi wala hakina vyanzo vya mapato vya kiserikali ni vyema ukatumia muda wako kutafakari kuwa je ni kweli CHADEMA wanachokosoa ni kweli ama si kweli! na pia nilitarajia wewe ukazungumzia nini ambacho serikali imefanikiwa wakati chadema ikilalamika kudai haki si kulalamika utambue hilo kuikosoa serikali ni jukumu la kwanza la chadema utambue hilo pia
 
Ovyooo.hawa jamaa unaowasifia ni ovyo sana,kwanza sifa ya kiongozi mzuri anatakiwa awe intelligent,na msimamizi mzuri wa hoja.
Heche ni mtupu kichwan kasoma SAUT kwa kuungunga sana mpaka kumaliza,kama ndo hazina za cdm basi cdm nayo ni hoi kwelikweli.
inteligent ni mulugo sio pale southern hill alikuwa haungi kitu kwani heche saut alisoma miaka mingapi alipata G.P.A ya ngapi?
 
Mkuu mie sina hata la kuongeza kutokana na hii kitu yako ni kwamba nakubaliana na yote uliyoyasema kwa 100% hawa vijana wanatisha kwa anga za siasa tanzania just cheki umri wao lakini wanawapelekesha watu wenye umri mara tatu ya umri wao bila kuogopa na sio kwa kuwatukana bali kwa hoja zilizoenda shule kwani hata Pinda alikiri mwenyewe.
 
WanaJF,
Mara ya mwisho kuzungumzia undani wa wanasiasa ilikuwa mwezi January mwaka huu kwa kuwazungumzia wanasiasa mashuhuri Tanzania Freeman Mbowe na Dr Wilbroad Slaa.Niliahidi nitarudi tena na mada hii hii kuwajadili wanasiasa wengine.Na nitakuwa nikifanya hivyo mara kwa mara nipatapo nafasi bila kubagua wanasiasa kwa itikadi zao.

Leo nitaomba kuwajadili wanasiasa wengine mashuhuri katika anga la Tanzania.Wanasiasa hao ni John Mnyika-Mbunge wa Jimbo la Ubungo na John Heche-Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa.Nimewachanganya Pamoja kwa sababu wanashabihiana kwa mambo mengi lakini lamsingi likiwa Itikadi yao na misimamo yao kuhusu mambo ya msingi.

Mafanikio Misimamo yao:

-Kwanza wote hawa ni vijana na wamekuwa kama Role model kwa vijana wengi si kwa vijana wa CDM tu bali kwa vijana wa Itikadi zote.
-Ni vijana wenye misimamo isiyoyumba na wanakitetea kwa nguvu kile wanachokiamini bila kuogopa vitisho kutoka kwa yeyote.
-Kutokana na Karama za kiuongozi walizo nazo wamefanikiwa kufika nafasi za juu kabisa za uongozi kwa umri wao.John Mnyika mbali ya kuwa mbunge anayeongoza jimbo kubwa kabisa la Ubungo pia yeye ndiye msemaji mkuu wa chama chake cha CDM.John Heche ni kiongozi wa BAVICHA Taifa na mjumbe wa Kamati kuu ya chama chake CDM,chombo cha ngazi ya juu kabisa ndani ya chama chake.
-Vijana hawa wamekuwa wakifanya kazi kubwa ndani ya chama chao hasa kuimarisha chama vijijini na kukipigania chama.Mafanikio yoyote ndani ya CDM huwezi kuwakosa hawa vijana.
-Ni vijana ambao hawaamini katika siasa za makundi.Sikuzote wanaamini katika CDM Imara.Huwezi kuwakuta wakishabikia majina ya watu ndani ya chama chao bali wanashabikia sera na Itikadi ya CDM.
-Ni wanyenyekevu,watiifu na wanapenda kukosolewa.
-Vijana hawa wana heshima kubwa kwa viongozi wao ndani ya Chama na huheshimu siku zote busara za wazee.Lau wakikosoa basi hukosoa kwa staha kubwa.

Changamoto zao:

-John Heche na John Mnyika pamoja na sifa zote zilizotajwa juu bado wanachangamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwafikia vijana wengi zaidi hasa wa vijijini na kuwapa somo la Uraia hususan umuhimu wa kujiandikisha na kupiga kura kwani inaonekana vijana wengi ni wafuasi sugu wa CDM lakini hawajiandikishi wala kupiga kura.
-Kutokana na umaarufu wao wamejitokeza vijana wengine wenye chuki na mafanikio yao na kuwaandama kwa matusi na maneno ya uongo hasa kupitia mitandao ya kijamii.Hata hivyo bado vijana hawa wameonyesha subira kubwa kwa mashambulizi hayo.Hawajakata tamaa bali wanasonga mbele.

Kwa Viongozi wakuu wa CHADEMA.

-Kutokana na yote niliyoandika juu viongozi wakuu wa CDM wanapaswa kuwatia moyo vijana hawa ili wasonge mbele zaidi na wasikatishwe tamaa na maadui wa CDM.
-CDM kama chama wanapaswa kuandaa vijana wasomi wanaofuata nyayo za kina Mnyika na Heche.Hata hivyo nafarijika kuona wapo vijana ndani ya CDM wenye uwezo wa kufuata nyayo hizi.Kwa mfano yupo kijana anayeitwa Ben Saanane,kwa wanaofuatilia siasa zake watagundua kwamba ni kijana anayeonyesha uvumilivu wa hali ya juu.Ben Saanane amewahi kupata misukosuko ya kisiasa lakini alisimama imara kutetea anchoamini.Hakuwahi kukashifu viongozi wake wa chama katika uficho au kwa uwazi.Ben anaamini CDM kama taasisi imara na siyo makundi ya watu.Ninaweza kusema Ben Saanane ni matunda ya kazi nzuri za kina Mnyika na wenzake.Hata hivyo chama kiandae vijana wengi zaidi wa kufuata nyayo za kina Mnyika na Heche na siyo Ben Saanane tu...

WanaJF Karibuni kwa mjadala!

ngoja nikajiandikishe maana nimeguswa na maneno ya mtumishi muongo moja umepita bila kupiga kura yani tangu uchaguzi wa mwaka 2005 nilitakiwa kujiandikisha ila nimetambua kwamba nimefanya makosa mbele ya Mungu na wanadamu kutotizmiza haki yangu ya msingi kumchagua kiongozi nimpendae tehe teh
 
mkuu tuntemeke swala la CHASO ni muhimu kwa ajili ya kuvuna vijana wapigania mabadiliko ya kweli hapo nakuunga mkono
lakini huyu binti yetu SHONZA ameamua mwenyewe na wote tunamwona akijiandaa kusumbua baraza lao labda tumfanyie maombezi aepukane na siasa za shibuda
 
hawezi kupambana na combination ya mboni mhita na sadifa wa uvccm.kama ni shule hata sadifa ana masters na wakili anthoni mavunde mjumbe wa baraza uvccm anayo
ana kazi sana kuongoza bavicha mwakani mbele ya hawa wadomi wa uvccm.kwa bahati nzuri mamluki wake paul makonda na akina felician tuliwadhibiti uvccm .hataweza dogo huyo
kwani lazima uwe na masters ndo ujue/uweze uongozi? Umewasaau prof:j.magembe,
 
hakuna chama cha siasa duniani chenye focus ya kufanya kazi za utekelezaji wakati hakikusanyi kodi wala hakina vyanzo vya mapato vya kiserikali ni vyema ukatumia muda wako kutafakari kuwa je ni kweli CHADEMA wanachokosoa ni kweli ama si kweli! na pia nilitarajia wewe ukazungumzia nini ambacho serikali imefanikiwa wakati chadema ikilalamika kudai haki si kulalamika utambue hilo kuikosoa serikali ni jukumu la kwanza la chadema utambue hilo pia

Hapo ndipo napoanza kuamini wote ni wababaishaji tu si chama kilichoko madarakani wala vyama vya upinzani, Kama hakuna chama cha upinzani kitakachothubutu kuonyesha njia kwa vitendo,vitakuwa na umaarufu lakini haviwezi kuaminika kwa wanyonge hata siku moja, siwezi kushawishika kwamba CDM hawana uwezo wa kuonyesha utendaji kwa kuchagua mambo muhimu yanayowagusa wanyonge waliowengi na kuwasaidia, eti mpaka wasubiri waingie Ikulu wakusanye Kodi, haya ni mawazo ya Utopia!! UNAPOKUTANA NA MTU ANALIA KWA USTAARABU TU WA KAWAIDA KABISA UNATOA KITAMBAA CHAKO CHA MFUKONI UNAMPATIA AFUTE MACHOZI.." sio unamsaidia kulia.

Kwa kiwango chochote wanachopata CDM ikiwa ni ruzuku, misaada kutoka kwa chama rafiki,michango ya wanachama,harambee, michango ya wabunge na "fundrising" yote hiyo wanapaswa waanze taratibu kuchagua mambo muhimu wasaidie wananchi, wanajiandaaje kuongoza nchi hawajui kuwahudumia wananchi? Napata taabu sana kutahmini ikiwa kuna watu makini Tanzania wenye nia ya dhati na utashi wa kuwatumikia watanzania ikiwa kuna watu bado wana fikra kama zako!!

Kitendo cha kuwa shupavu na mahiri katika kulalamika na kueleza udhaifu wa chama, serikali ama mtu mwingine sio dalili ya kuwa na nia safi ama utashi wa kuwatumikia watanzania, tutahitaji tujiridhishe kwa historia yako katika kuwasaidia watanzania,na watanzania wa leo wamechoka kusikia Blah....blah....blah! ikiwa watanzania wamekata tamaa basi wewe uanayejinasibu kuwa mkombozi wao utembee katika maneno yako!! ''SIO KUHUBIRI MAJI KISHA WEWE UNAKUNYWA MAZIWA'' ni unafiki mkubwa na kamwe huwezi kuaminika hata kidogo.
 
Hapo ndipo napoanza kuamini wote ni wababaishaji tu si chama kilichoko madarakani wala vyama vya upinzani, Kama hakuna chama cha upinzani kitakachothubutu kuonyesha njia kwa vitendo,vitakuwa na umaarufu lakini haviwezi kuaminika kwa wanyonge hata siku moja, siwezi kushawishika kwamba CDM hawana uwezo wa kuonyesha utendaji kwa kuchagua mambo muhimu yanayowagusa wanyonge waliowengi na kuwasaidia, eti mpaka wasubiri waingie Ikulu wakusanye Kodi, haya ni mawazo ya Utopia!! UNAPOKUTANA NA MTU ANALIA KWA USTAARABU TU WA KAWAIDA KABISA UNATOA KITAMBAA CHAKO CHA MFUKONI UNAMPATIA AFUTE MACHOZI.." sio unamsaidia kulia.

Kwa kiwango chochote wanachopata CDM ikiwa ni ruzuku, misaada kutoka kwa chama rafiki,michango ya wanachama,harambee, michango ya wabunge na "fundrising" yote hiyo wanapaswa waanze taratibu kuchagua mambo muhimu wasaidie wananchi, wanajiandaaje kuongoza nchi hawajui kuwahudumia wananchi? Napata taabu sana kutahmini ikiwa kuna watu makini Tanzania wenye nia ya dhati na utashi wa kuwatumikia watanzania ikiwa kuna watu bado wana fikra kama zako!!

Kitendo cha kuwa shupavu na mahiri katika kulalamika na kueleza udhaifu wa chama, serikali ama mtu mwingine sio dalili ya kuwa na nia safi ama utashi wa kuwatumikia watanzania, tutahitaji tujiridhishe kwa historia yako katika kuwasaidia watanzania,na watanzania wa leo wamechoka kusikia Blah....blah....blah! ikiwa watanzania wamekata tamaa basi wewe uanayejinasibu kuwa mkombozi wao utembee katika maneno yako!! ''SIO KUHUBIRI MAJI KISHA WEWE UNAKUNYWA MAZIWA'' ni unafiki mkubwa na kamwe huwezi kuaminika hata kidogo.

Mkuu Shibalanga
Ingawa umechangia kwa jazba sana lakini ninaamini mchango wako umeongeza thamani ya andishi langu.
Nina hakika viongozi mbalimbali wa CDM wanapitia mada hii kila mara kupata mawazo ya kujenga.
 
kwani lazima uwe na masters ndo ujue/uweze uongozi? Umewasaau prof:j.magembe,

Mkuu ruhi
Inasikitisha sana kuona mpaka leo watu wanaamini kusoma sana ndiyo kigezo cha uongozi.
Wapo watu waliosoma sana lakini wameharibu sana kwenye nafasi zao na wapo wasiosoma sana ama wenye elimu ya wastani lakini wamefanya makubwa.
Mifano ipo mingi sana sina hata haja ya kuitaja.
 
Umesahau kuwa mnyika ana maumivu ya kichwa ya mara kwa mara, jee na heche pia?
 
mkuu tuntemeke swala la CHASO ni muhimu kwa ajili ya kuvuna vijana wapigania mabadiliko ya kweli hapo nakuunga mkono
lakini huyu binti yetu SHONZA ameamua mwenyewe na wote tunamwona akijiandaa kusumbua baraza lao labda tumfanyie maombezi aepukane na siasa za shibuda

Mkuu kiribo

Niseme kidogo kuhusu huyu Binti Shonza,huyu binti ni mzuri sana kiuongozi kwani namfahamu vyema tangu akiwa mwaka wa kwanza chuoni.
Tatizo lake moja tu ni kudanganywa na akadanganyika.

Unajua nilisoma siku moja makala ya Dr Kitila niliipenda sana.Dr Kitila alisema hawa vijana wanapochaguliwa nafasi za uongozi wanapaswa kupata semina za maadili ya uongozi.Wanapaswa kujua miiko ya Uongozi.

Sasa kitendo cha Shonza kwenda kwenye vyombo vya habari kumpinga Mkiti wake ilikuwa ni mbaya sana kwake.Na hii itamgharimu Shonza kisiasa maisha yake yote.

Kwa ninavyomjua Shonza naamini kuna vijana walimuingiza kwenye mtego naye akaingia mkenge.Ni vigumu sana viongozi wenzake kumuamini kwa sasa.Kwani kulikuwa na hasara gani Shonza kusubiri vikao ndipo amshambulie Mkiti wake?

Ujana bwana maji ya moto usipokuwa makini utaungua.Hata hivyo naamini Shonza amejifunza kitu.
 
ngoja nikajiandikishe maana nimeguswa na maneno ya mtumishi muongo moja umepita bila kupiga kura yani tangu uchaguzi wa mwaka 2005 nilitakiwa kujiandikisha ila nimetambua kwamba nimefanya makosa mbele ya Mungu na wanadamu kutotizmiza haki yangu ya msingi kumchagua kiongozi nimpendae tehe teh

Comrade Smallvile
Kwanza hongera kwa kuchukua hatua baada ya kusoma mada yangu.

Nimekuwa nikisisitiza siku zote umuhimu wa kujiandikisha na kupiga kura.Ndiyo maana nasema hawa akina John Mnyika,John Heche,Ben Saanane na vijana wenzao wanapaswa kujua bado wana kazi kubwa kusambaza elimu ya Uraia vijijini.Wajichimbie vijijini kuliko na idadi kubwa ya watu.

Binafsi sioni haja wala maana yoyote pale Dr Slaa anapolakiwa na msururu wa gari mia mbili na kuhutubia watu mpaka elfu kumi huko mikoani,lakini uchaguzi unapokuja chama kinapata kura chache.Bila wananchi kuelezwa umuhimu wa kujiandikisha na kupiga kura itakuwa kazi bure.

Kina Mnyika,Heche,Saanane na wenzao wanapaswa kulipa hili umuhimu mkubwa.
 
Mkuu mie sina hata la kuongeza kutokana na hii kitu yako ni kwamba nakubaliana na yote uliyoyasema kwa 100% hawa vijana wanatisha kwa anga za siasa tanzania just cheki umri wao lakini wanawapelekesha watu wenye umri mara tatu ya umri wao bila kuogopa na sio kwa kuwatukana bali kwa hoja zilizoenda shule kwani hata Pinda alikiri mwenyewe.

Mkuu Mboko

Asante sana kwa kukubali andiko langu.Nisema tu kwamba vijana hawa wanapaswa pia kupokea pongezi zako kama changamoto kwao ili wasonge mbele zaidi.
 
Back
Top Bottom