WanaJF,
Mara ya mwisho kuzungumzia undani wa wanasiasa ilikuwa mwezi January mwaka huu kwa kuwazungumzia wanasiasa mashuhuri Tanzania Freeman Mbowe na Dr Wilbroad Slaa.Niliahidi nitarudi tena na mada hii hii kuwajadili wanasiasa wengine.Na nitakuwa nikifanya hivyo mara kwa mara nipatapo nafasi bila kubagua wanasiasa kwa itikadi zao.
Leo nitaomba kuwajadili wanasiasa wengine mashuhuri katika anga la Tanzania.Wanasiasa hao ni John Mnyika-Mbunge wa Jimbo la Ubungo na John Heche-Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa.Nimewachanganya Pamoja kwa sababu wanashabihiana kwa mambo mengi lakini lamsingi likiwa Itikadi yao na misimamo yao kuhusu mambo ya msingi.
Mafanikio Misimamo yao:
-Kwanza wote hawa ni vijana na wamekuwa kama Role model kwa vijana wengi si kwa vijana wa CDM tu bali kwa vijana wa Itikadi zote.
-Ni vijana wenye misimamo isiyoyumba na wanakitetea kwa nguvu kile wanachokiamini bila kuogopa vitisho kutoka kwa yeyote.
-Kutokana na Karama za kiuongozi walizo nazo wamefanikiwa kufika nafasi za juu kabisa za uongozi kwa umri wao.John Mnyika mbali ya kuwa mbunge anayeongoza jimbo kubwa kabisa la Ubungo pia yeye ndiye msemaji mkuu wa chama chake cha CDM.John Heche ni kiongozi wa BAVICHA Taifa na mjumbe wa Kamati kuu ya chama chake CDM,chombo cha ngazi ya juu kabisa ndani ya chama chake.
-Vijana hawa wamekuwa wakifanya kazi kubwa ndani ya chama chao hasa kuimarisha chama vijijini na kukipigania chama.Mafanikio yoyote ndani ya CDM huwezi kuwakosa hawa vijana.
-Ni vijana ambao hawaamini katika siasa za makundi.Sikuzote wanaamini katika CDM Imara.Huwezi kuwakuta wakishabikia majina ya watu ndani ya chama chao bali wanashabikia sera na Itikadi ya CDM.
-Ni wanyenyekevu,watiifu na wanapenda kukosolewa.
-Vijana hawa wana heshima kubwa kwa viongozi wao ndani ya Chama na huheshimu siku zote busara za wazee.Lau wakikosoa basi hukosoa kwa staha kubwa.
Changamoto zao:
-John Heche na John Mnyika pamoja na sifa zote zilizotajwa juu bado wanachangamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwafikia vijana wengi zaidi hasa wa vijijini na kuwapa somo la Uraia hususan umuhimu wa kujiandikisha na kupiga kura kwani inaonekana vijana wengi ni wafuasi sugu wa CDM lakini hawajiandikishi wala kupiga kura.
-Kutokana na umaarufu wao wamejitokeza vijana wengine wenye chuki na mafanikio yao na kuwaandama kwa matusi na maneno ya uongo hasa kupitia mitandao ya kijamii.Hata hivyo bado vijana hawa wameonyesha subira kubwa kwa mashambulizi hayo.Hawajakata tamaa bali wanasonga mbele.
Kwa Viongozi wakuu wa CHADEMA.
-Kutokana na yote niliyoandika juu viongozi wakuu wa CDM wanapaswa kuwatia moyo vijana hawa ili wasonge mbele zaidi na wasikatishwe tamaa na maadui wa CDM.
-CDM kama chama wanapaswa kuandaa vijana wasomi wanaofuata nyayo za kina Mnyika na Heche.Hata hivyo nafarijika kuona wapo vijana ndani ya CDM wenye uwezo wa kufuata nyayo hizi.Kwa mfano yupo kijana anayeitwa Ben Saanane,kwa wanaofuatilia siasa zake watagundua kwamba ni kijana anayeonyesha uvumilivu wa hali ya juu.Ben Saanane amewahi kupata misukosuko ya kisiasa lakini alisimama imara kutetea anchoamini.Hakuwahi kukashifu viongozi wake wa chama katika uficho au kwa uwazi.Ben anaamini CDM kama taasisi imara na siyo makundi ya watu.Ninaweza kusema Ben Saanane ni matunda ya kazi nzuri za kina Mnyika na wenzake.Hata hivyo chama kiandae vijana wengi zaidi wa kufuata nyayo za kina Mnyika na Heche na siyo Ben Saanane tu...
WanaJF Karibuni kwa mjadala!
Sina uhakika sana ikiwa utafiti wako hapo juu una ithibati, lakini naona nina hoja ya kuchangia,nitachepuka kidogo isipokuwa binafsi nitawachambua hao vijana kwa kujadili taasisi waliyopo (CHADEMA)
CDM kama chama kikuu cha upinzani hapa Tanzania kwa vyovyote vile lazima kikutane na changamoto lukuki katika harakati zake za kuingia ikulu, mara kadhaa nimekuwa nikimsikia Dr. Slaa akiwajibu mahasimu wake wa kisiasa (CCM) pale wanapolalama kwamba CMD muda wote wapo kuangalia mapungufu tu na kuyasema bila kutaja hata mazuri ya CCM, lakini yeye bila kumung'unya maneno alitoka na kusema wao CHADEMA hawapo kwa ajili ya kusifia mazuri ya CCM, maana kama ni mazuri hawaoni haja ya kuyataja.
Sasa kwa msingi huu, binafsi naona udhaifu mkubwa sana wa CDM kama sio wa Dr. Slaa, nafikiri huo ndo msimamo wa chama, hivyo BAVICHA ya kina Heche na wenzake wameendelea kulalamika kila kukicha kiasi kwamba kama utakuwa unafuatilia vizuri mikutano yao muda wote wanaeleza Rais kafanya nini....waziri kafanya nini..... wakati mwingine unaweza hata kubashiri mambo ambayo atakayoongea mara tu akianza.
My take: Siasa hizi zimepitwa na wakati, watanzania wamechoka kusikiliza watu wakilalamika tuuuuu! inapaswa sasa kwa uwezo mdogo walionao CDM waonyeshe kwa mfano; kama wanasema shule za kata hazina viwango, zitawaangukia wanafunzi hebu wajenge hata shule moja na wajinadi kwa kusema "Ikiwa tutaingia madarakani hizi ndo shule zenye viwango tutajenga" waseme na kutenda hivyo hivyo hata kwenye mambo kama visima vya maji, barabara za vijijini,zahati, ofisi za mitaa n.k
Kiukweli wananchi wamechoka kukusanyika kwenye mikutano wanapewa faraja ama machungu wanaporudi nyumbani kero ziko pale pale kwanza mkutano umewakawiza kwenda kutafuta kuni, kuchota maji maana ni ya shida, kwenda kutafuta vipimo zahati ya mbali,Inawezekana wanachoelezwa ni cha kweli lakini mwisho wa siku hawana jinsi zaidi ya kusubiri kipindi kingine cha uchaguzi waweze kufanya mabadiliko lakini pengine imebaki miaka 3 ndo uchaguzi mwingine sasa ndo kusema CDM wao watakuwa wakizunguka kulalamika tuuu! mi nadhani sio sahihi hebu watoke wafanye kwa mfano ndo njia peke itayowajengea imani na heshima kubwa kwa wapiga kula.
CHADEMA naweza kusema wamepanda mbegu mbaya sana kwa vijana wa kitanzania na watanzania kwa ujumla, Tabia ya kulalamika tuuuu na wengine sasa hata ukimuuliza kile acholalamika kwa kiasi gani ameona au anatambua athari zake, hajui chachote isipokuwa aliwahi kuwasikia viongozi wake wakilalamika, hii mbegu sio nzuri hata kidogo kuna wengine kabisa tunafahamu ugumu wa maisha yake sababu ni yeye mwenyewe lakini naye analalamika vijana au watu wa namna hii wapo kila kona ya nchi hii lakini ni lini hivi vyama vya upinzani vilisimama vikakemea vijana waache tabia ya kufanyiwa kila kitu? waache kukaa masikani na kusubiri maendeleo?
Kina Heche na Mnyika wamekuwa katika mkururo huo huo wa kulalamika tu kuonyesha madhaifu tu ya CCM na kusahau kuwaonyesha kwa mfano watanzania ni kipi wamefanya,najua watakuja watu wahoji juu ya fedha, lakini mi nasema wanaweza wakiamua, ujue CDM mpaka kimejipambanua kuwa ni chama kinachojengwa na matukio ni kweli kabisa!
Nilifarijika walau kwa mara ya kwanza kuona uongozi wa CDM( sikumbuki walikuwa ni wa wapi lakini sio makao makuu) walitoka na Greda kwenda kupanua nadhani mto msimbazi ili kusaidia wananchi waishio bonde la mto msimbazi wasipatwe maafa ya mafuriko, kitu kile ndo nataka iwe msimamo wa CDM Taifa na kila kiwango cha chama, mambo hayo ndo yatakayowajengea heshima kubwa na kuaminika zaidi kuliko kulalamika tu kila kukicha,mnawafundisha kitu kibaya sana watanzania kujipambanua nyie ni malaika siku ikitokea mkachukua nchi mbegu mlioipanda itawwatesa hata nyie wenyewe maana ndo mazoea! AKSANTENI.