- Thread starter
- #181
Kumbe huo ndo undani wao? Duh!! inabidi utuambie ulitumia nyenzo gani kufanya utafiti kama huu unaoonyesha umahiri wa mnyika na henche hasa wakiwa ni wapiga POROJO wakuu wa chadema. Ujasiri na umahiri wa mtu si kelele na maneno mengi bali ni utendaji wao wa kazi za kuwaletea wananchi maendeleo. Njoo na hoja za msingi utuambie hadi sasa mnyika amewatetea na kuwasaidia vipi wananchi wake wa jimbo la Ubungo? Bado hatujaona mafanikio yao, inabidi warudi tena kwenye kile cha cha kikristo cha ujerumani (CDU) wakajifunze tena namna nzuri ya kuwabatiza watanzania.
Mkuu wangu Lali
Mtu yeyote mstaarabu akisoma hoja yako atakupuuza tu kwa sababu umeonekana ni mtupu kichwani.
Binafsi ninaogopa kukuonyesha mazuri aliyofanya Mnyika kwa sababu tayari umeshajitanabaisha wewe ni mbaguzi wa hali ya juu ambaye Mwl Nyerere tayari alishatuonya tuwaogope watu wa aina yako kama Ukoma.
Kwa mtu mwenye akili timamu kabisakabisa huwezi kusema kina Mnyika wakasomee Kubatiza watu.Mungu akusaidie upone huo ugonjwa ulio nao wa ubaguzi wa kidini.