Ben Saanane
JF-Expert Member
- Jan 18, 2007
- 14,580
- 18,222
JangalaFalsafa unachokisema ndo kitu nachokihitaji, uko sahihi kabisa, CDM au kambi ya upinzani kwa ujumla wanapaswa kujitathmini kila wakati na kujielekeza katika mambo ya msingi yatakayowaletea heshima kubwa na watanzania walio wengi kuwaamini,wasiwe na papara za kuwalazimisha watanzania kuwaamini, kitendo cha kuaminika hakilazimishwi kitakuja automatically ikiwa wananchi wataridhika na utashi wa kweli katika kuwaletea mabadiliko.
BAVICHA wanaweza wakawa mstari wa mbele katika kuwaunganisha vijana wa Tanzania na kuwaongoza katika harakati za kujiletea kipato, Nguvu ya umma isitumike katika maandamano tu watumie nguvu ya umma katika shughuli za harambee ili kuwajengea uwezo vijana na mwisho wa siku hawa ndo watakichangia chama katika harakati zenu za M4C,au anzisheni utaratibu popote pale katika nchi hii itengwe hata siku moja kila mwisho wa mwezi vijana nchi nzima wafanye shughuli za kijamii, utaratibu huu upo Rwanda, upo Burundi mtakuwa walau positive katika Taifa hili vinginevyo kuna baadhi ya watanzania wataendelea kuwaona ni watu wa fujo fujo hivi, hamna ustaarabu hamna jema katika nchi hii licha ya michango mizuri bungeni kwa bahati mbaya si watu wote wanaweza kufanya tathmini kwa kupitia bunge......
Hili la kutenga siku kwa ajili ya shughuli za kijamii tuko pamoja
Huu ni moja wapo wa mipango tuliyo nayo.