Unataka Utajiri? Njoo Tunduma haraka!

Tupo Tunduma na tumekula Christmas hapa huku tukisubiri mwaka mpya
Mambo ya Tunduma yanatisha kama sio kushangaza
Tunduma ndio sehemu pekee Tanzania kama sio Africa ambayo vijana wadogo kabisa ni matajiri wa kutisha na wengi wao hawana hata elimu ya darasa la saba
baada ya kufanya utafiti mdogo tu kuhusisha watu kama kumi tumegundua kuina jambo linaloendelea hapa Tunduma na Mbeya ambalo bado halijawekwa wazi
watu wa tunduma hasa vijana wanatumia nguvu za giza au uchawi kupata mali nyingi wanazomiliki,kuna mganga maarufu hapa ambaye anafuga jogoo mkubwa sana mwenye afya ya kutosha
ukitaka utajiri unaenda kwa huyu mganga halafu anabashiri siku zako za kuishi duniani zimebakia ngapi
akishakupa idadi ya siku zako zilizobakia duniani anamleta jogoo wake mwenye afya tele
anarusha mahindi sawasawa na idadi ya miaka yako iliyobakia duniani.jogoo anaruhusiwa kudonoa mahindi yale,
kama miaka yako ya kuishi duniani ilibakia 10,mahindi kumi yanarushiwa jogoo,anadonoa na kula baadhi ya mahindi,akila mahindi matano ina maana utapewa utajiri na utaishi miaka mitano baada ya hapo utakufa
ile miaka mitano iliyobaki utaenda kuwatumikia wakubwa waliokupa huo utajiri,kuna mahimbo ya madini Congo DRC ndiko unakopelekwa
tulipoulizia maisha ya huko machimboni tuliambiwa kule unakunywa maji kila siku huku ukipiga kazi masaa 24
hiyo ndio taarifa ya Tunduma mji uliojaa vijana waliokata tamaa na kuamua kujitoa mhanga
hii taarifa ni ya kweli na tumefanya utafiti wa kutosha

Hii kitu ni kweli iko Tunduma na hata Mbeya mjini. Wenyewe ambao wanafurahia huo utajiri wanasema kila kitu kinawezekana 'ujasiri wako tu'. Sasa kuhusu hizo sentensi nilizoweka red, mimi nilipata maelezo tofauti kidogo;
1. Jogoo akichagua mahindi kadhaa, ina maana sawa kuwa utakuwa tajiri wa kufa mtu kwa kipindi hicho. Tofauti inayobaki ni kuwa unafanywa msukule. Muda wa kutumika msukule ukiisha, then unauawa moja kwa moja
2. Kipindi kile ukiwa msukule, wanasema unapewa 'rejesho' unalotakiwa kurudisha kila siku. Hii inatokana na 'matajiri wapya' waliopo kwenye mng'aro ambao wewe unakuwa unawatumikia. Ni kwamba wakati wewe ulipokuwa ukifaidi utajiri ni kuwa kuna watu waliofanywa misukule ndio walikuwa wanakuletea mali, hivyo sasa inakuwa zamu yako kuwatumikia wengine
3. Huo msukule kazi unazofanya ni kuiba kimazingara fedha na vitu vya thamani toka nyumbani kwake i.e. kuchota ule utajiri wake alioucha na kuupeleka kwa mganga ili awagawie 'matajiri wapya'. Na kama haujitoshelezi basi unahamia kuiba kwa ndugu na jamaa zako.
4. Inasemekana pia ukishindwa kufikisha 'rejesho' la muda uliopewa basi unapata viboko vya haja. Kwa hivyo salama yako iwe kuwa 'rejesho' ni dogo kuliko uwezo wa wewe kurejesha, la sivyo kila siku unalalia fimbo
 
Matthew 16:26 KJV

For what is a man profited, if he shall gain the whole world, and lose his own soul? or what shall a man give in exchange for his soul?

ndo ushangae sasa,hata mtu awe na mabilioni atakufa atayaacha,ni upuuzi mtupu.
 
Tajirika mwenyewe umalize ndugu zako wote,wenzio tuna chapa kazi ili tupate kihalali
 
dalili za kukata tamaa na athari za kunywa VIROBA kwa wingi,.......wenye hela ni washirikina!
umenifurahisha sana mkuu,Tanzania ukiwa na hela kama sio fisadi basi watakuita mchawi.hawaamini katika kufanya kazi kwa bidii. Ndio maana hata maofisini anaejituma kazini lazima aundiwe zengwe kwamba anamajungu au anajipendekeza kwa bosi...wabongo tufanye kazi kwa bidii fursa zipo nyingi tutatajirika tu.!
Kama
 
Tanzania ni nchi ya ajabu sana!nadhan ni miongoni mwa nchi chache ambazo matajiri hawana elimu ya kutosha ht ya fomu four hakuna!lakin nchi za wenzetu zlizoendelea ni vigumu sana kukuta mtu mwenyewe elimu dogo kawa tajiri kama ilivo tanzania!anachosema mtoa mada ni kwel kabisa!

Unasahau kuwa watanzania tunaishi kama kuku wa kienyeji, kila mtu anajihangaikia mwenyewe. Ndio maana maskini wanakua na hela sababu wanajua hayupo wa kumsaidia zaidi ya nguvu zake.
 
...Huu upo nje nje tu, wala sio hadithi...
Kuna utajiri gani huko si tungewasikia au kuwaona km huko Mirerani, Geita au wangetoa matajiri wanaohesabika km kina Rostam, EL, MENGI, Bakhresa lakini wapi wote huko unaambiwa wamewaweka watoto au wazazi wao Misukule
Utajiri wa Tunduma ni wa Mipakani km Tarakea, Namanga nk kuwa na makaratasi mengi (Noti) mifukoni
 
watanzania bwana! hebu badilikeni jamani, unatumia muda mwingi kujadili mambo ya kusadikika, and then, mwisho wa siku unatoa povu kwa kulalamikia serikali? badilikeni jamani, maji hufuata mkondo, na kizazi chenu kitafuata nyayo zenu hizo hizo.
 
Nilidhani jogoo anawekewa punje za mahindi kwenye kinyeo cha kijana kisha anadonoa ili kumfanya kijana awe lijali
 
Hii kitu ni kweli iko Tunduma na hata Mbeya mjini. Wenyewe ambao wanafurahia huo utajiri wanasema kila kitu kinawezekana 'ujasiri wako tu'. Sasa kuhusu hizo sentensi nilizoweka red, mimi nilipata maelezo tofauti kidogo;
1. Jogoo akichagua mahindi kadhaa, ina maana sawa kuwa utakuwa tajiri wa kufa mtu kwa kipindi hicho. Tofauti inayobaki ni kuwa unafanywa msukule. Muda wa kutumika msukule ukiisha, then unauawa moja kwa moja
2. Kipindi kile ukiwa msukule, wanasema unapewa 'rejesho' unalotakiwa kurudisha kila siku. Hii inatokana na 'matajiri wapya' waliopo kwenye mng'aro ambao wewe unakuwa unawatumikia. Ni kwamba wakati wewe ulipokuwa ukifaidi utajiri ni kuwa kuna watu waliofanywa misukule ndio walikuwa wanakuletea mali, hivyo sasa inakuwa zamu yako kuwatumikia wengine
3. Huo msukule kazi unazofanya ni kuiba kimazingara fedha na vitu vya thamani toka nyumbani kwake i.e. kuchota ule utajiri wake alioucha na kuupeleka kwa mganga ili awagawie 'matajiri wapya'. Na kama haujitoshelezi basi unahamia kuiba kwa ndugu na jamaa zako.
4. Inasemekana pia ukishindwa kufikisha 'rejesho' la muda uliopewa basi unapata viboko vya haja. Kwa hivyo salama yako iwe kuwa 'rejesho' ni dogo kuliko uwezo wa wewe kurejesha, la sivyo kila siku unalalia fimbo

.
Halafu kibaya zaidi asilimia kama 99 ya maduka ya Tunduma yanapiga nyimbo za injili(kwaya).
.
 
Tunduma bana kwa mambo ya ushirikina sikatai maana kuna siku (wiki tatu zimelizopita) nilikuwa hapo mchana kulitanda bonge la wingu radi zinapiga hatari mwenyej wetu akasema hii mvua hainyeshi cz wafanyabiashara wameanika mazao yao na kweli haikunyesha ila mm binafsi nilishannua mpk mwamvuli

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Utajiri wa punje,mambo ya wakinga hayo, watoto wa mwakipande hao.
 
Hivi ni ukweli haya Mambo? Na kwa mfano huyo mganga anaekupa masharti akifa inakuaje? Na ukifa utajiri unabaki ili familia iuendeleze?
 
umechanganya madesa. mwakipande alikuwa anaishi makete tarafa ya lupila. kawatajirisha sana wakinga...kwa sasa ni marehemu. but huo utajiri wa tunduma hiyo ni kweli na unajulikana sana kwa jina la utajiri wa mkataba.infact wewe hutaufaidi but ndugu zako ndo wanaenjoy....
Mkuu haya Mambo umejuaje
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom