Kwa kawaida dawa/ supplements hua zinahitaji mtu akiwa anakula awe anafanya mazoezi haswa akilegea legea ndiyo unakuta mtu ni baunsa wa klabu na ananyanyua uzito lakini ana kitambi na matako makubwa hii ni kwa Tanzania.
Wenzetu kwakua wana hadi dawa za kufanya wawe na miili iliyokata ndiyo unakuta bodybuilder ana kitambi lakini kina six packs
View attachment 470604.
Madhara mengine yanasemwa kua ni hasira za hapa na pale mfano Bodybuilder Titus alipoua mtu ilisemekana kua ni kutokana na matumizi ya steroids.
Lakini kuna bodybuilders kama Flex Wheeler na Paul Dillet ambao wameonesha kua steroids siyo nzuri kwa afya kutokana na madhara waliyoyapata baada ya kuachana na bodybuilding.
Magonjwa kama ya moyo, ini, mapafu na kansa hua yanawasumbua sana bodybuilders ambao walikua wakitumia hizi dawa.