Unataka kuijua CHADEMA? Angalia hapa

Unataka kuijua CHADEMA? Angalia hapa

Mjinga kweli, kwani hata kama wanapewa support kutoka nje, Ukipata maisha bora shida iko wapi?
Hata tukiendeshwa na mzungu ila tuwe na Good life ubaya uko wapi? Si bora hiyo kuliko ujinga unaoendelea sa hvi humu nchini! Tatizo unashabikia chama na si maendeleo... Nyie ndo ambao bado mnarudisha hii nchi nyuma.. Wewe na fisadi yeyote aliye bungeni hamna tofauti....
 
Annael,
Pole sana kwa matusi yanayozidi kuwa utamaduni wa kawaida wa hapa JF (lakini ni baadhi ya mashabiki wa chama fulani), itabidi uyazoee.
Laiti JF tungejitahidi kuujadili ukweli kama ulivyo, pengine tungekuwa na mchango wa kulielekeza taifa letu katika suluhu. Huko kutofautiana kwa Mwalimu na Mzee Mtei ni kweli kulitokea (Soma kitabu cha Mtei mwenyewe; From Goatherd to Governor). Katika kitabu hicho Mtei anaeleza hilo suala la masharti ya IMF. Hao jamaa walitaka fedha ya Tanzania ishushwe thamani, viwanda na mashirika ya umma tuuze, tupunguze pesa tunazotumia katika sekta ya elimu, n.k. Mtei akakubaliana nao, maana wakati huo uchumi wa nchi ulikuwa unayumba si pole pole, na ili IMF watupe msaada wa kifedha 'kutuokoa' (bailout) ndio wakaja na masharti hayo. Mtei akayakubali, ila yeye alikuwa waziri tu wa fedha, ikabidi aende kwa mkuu wa kaya, ambaye aliwatolea nje, na akamwambia Mtei, 'Tanzania haitatawaliwa kutokea Washington, na hela yetu hatushushi ... over my deadbody' Kesho yake Mtei akajiuzulu.
Lakini hali ya uchumi ikaendelea kuwa ovyo, hatimaye Mwalimu akang'atuka. Akaja Mzee ruksa, asijue afanye nini na hiyo hali, ndipo ikabidi awakubalie IMF, tena kwa namna fulani akamtumia huyo huyo mzee Mtei kwa kumtuma awe mwakilishi wa Tanzania katika makao ya IMF Marekani. Kwa hiyo sera za kubinafsisha zilianzia hapo, Mkapa alikuja kuintensify tu. (Hapa utaelewa kwa nini watu wanasema CCM halisi, ile ya kijamaa iliondoka na Mwalimu)
Hatimaye Mzee Mtei akiwa amekwishashiba mambo ya IMF na Benki ya Dunia, na akiwa anajua fika matatizo yetu kiuchumi yalikoanzia, uliporuhusiwa mfumo wa vyama vingi nchini, ndipo yeye na wenzake wakaanzisha chama chenye mtazamo huo uliousema.
Turejee nyuma kidogo, kwa nini uchumi uliyumba hadi ikabidi IMF waje kutuwekea 'dhamana'? Sababu ni nyingi; 1. Vita vya Kagera (tumlaumu Mwalimu?) 2. Kupanda kwa bei ya mafuta ulimwenguni (tulaumu mfumo wa uchumi wa dunia?) 3. Ufisadi wa waliopewa dhamana ya kuendesha mashirika ya umma (hapa tujilaumu sisi wenyewe watanzania kwa tabia ya kutafuna kama mchwa, na kutothamini bidhaa zetu wenyewe).
Jambo jingine tujiulize; je, dhamana ya IMF imesaidia? Hata kidogo, tena ndio imefanya mambo yakawa mabaya zaidi.
Ndio maana nikasema, kama JF yaweza kuwa jukwaa la msaada kwa Tanzania, inabidi iwe sehemu ya kutafuta njia ya tunachomokaje katika udhaifu wa nchi kiuchumi ambao wahuni wa magharibi wameutumia kwa kutulaghai kwamba wanatusaidia kumbe ndio wanatuharibia zaidi.

waridi umejaribu kueleza vizuri,kama umefatilia vizuri utajua fika we na mtoa mada mnatofautiana kabisa hata jinsi ya kufikiri,unamzidi mbali kabisa hapa na washington.

Mtoa mada ana lugha za kashfa na za kichochezi, yan ana tumia lugha inayo mfanya mtu hapandwe na hasira kwasababu ana anzisha uzi ili kukera watu sio kutafuta majibu.

Mimi siungi mkono matusi hila mtoa mada anaonekana kupenda matusi,mada yake hiko wazi kabisa kwani hakuna chama kisicho cha kibepari nchini kwani ata nchi yenyewe ni ya kibepari.

Mtoa mada alitaka kupima hisia za wana cdm,kwenye mada yake hakuna asichokijua hapo.
 
Chadema ni chama kilichoanzishwa kwa mfumo wa kibepari. Kwahiyo Msingi mkuu wa chadema ni ubepari.
Mwanzilishi wa Chadema ni Mzee Mtei ambaye alitofautiana na baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Tofauti yao ni kuhusu sera za IMF Mtei alikuwa anaunga mkono bali Nyerere alikataa sera za kibepari.

Kwahiyo Sera za kibepari msingi wake mkuu ni mtaji (Pesa).
Kimekuwa kikipata misaada ya chini chini kutoka katika nchi za magharibi kama Uholanzi na zingine, kitendo ambocho kinanipa mashaka kuwa vipi pesa hizo zitalipwa. Ninadhani kuna makubaliano ya chini kwa chini ambayo watu wengi hatuyajui.

CHADEMA kimejitahidi sana kuwafundisha wanachama wake kutohoji mapato na matumzi ya chama. Hii ni mbinu ambayo imetumiwa na CHADEMA kuwaaminisha wanachama dhidi ya viongozi kuwa wao hawana doa.

na hii ni hatari sana.

Bora hayati baba wa taifa angeukubali ubepari ile wote tuwe mabepari wa longtime kuliko makaburu ambao tunao sasa hivi ambao wachache ndo wenye navyo. Wazazi wangu walikuwa maskini kwa sababu ili tusome na kulitumikia taifa kwa uadilifu halafu leo hiii wale mliosomeshwa kwa sacrifice ya wazazi wangu leo hii ndiyo nyie mabepari na watoto wenu. Bora tungeuanza mapema ungekuta na mimi ni bepari. To hell. Tunadanganywa na Socialism, eti hata kwenye katiba ya sasa ipo wakati wameshatengua ujamaa na azimio la Zanzibar. To hell!!! Mtei ana akili sana na ndiyo maana CDM ni makini!!!
 
Duh...........! Haya maongeziiiii.............! Ngoja nipime upepo kwanza.
 
Hebu tupe hivi CCM wanaendesha mfumo upi? Mbona mwenye nacho ndiyo anapeleka watoto wake shule nzuri, hospiatali nzuri watoto wa hao wakubwa ndiyo wanakuwa wakubwa pia JE HUU NI MFUMO GANI UBEPARI USIOUPENDA AU UJAMAA? TAFAKARI KWA MAKINI
Ubepari tatizo lake ni kwamba mwenyenacho ndie anayepata na siye nacho ataendelea kuwa mnyonge.

Ni tofauti kabisa na mfumo wa kijamaa.
Jaribu kujikumbusha Uraia au siasa darasa la tatu shule ya msingi.
 
waridi umejaribu kueleza vizuri,kama umefatilia vizuri utajua fika we na mtoa mada mnatofautiana kabisa hata jinsi ya kufikiri,unamzidi mbali kabisa hapa na washington.

Mtoa mada ana lugha za kashfa na za kichochezi, yan ana tumia lugha inayo mfanya mtu hapandwe na hasira kwasababu ana anzisha uzi ili kukera watu sio kutafuta majibu.

Mimi siungi mkono matusi hila mtoa mada anaonekana kupenda matusi,mada yake hiko wazi kabisa kwani hakuna chama kisicho cha kibepari nchini kwani ata nchi yenyewe ni ya kibepari.

Mtoa mada alitaka kupima hisia za wana cdm,kwenye mada yake hakuna asichokijua hapo.

Ni sawa Ruttashobolwa, hata mimi napinga kwa nguvu zote huu utamaduni wa kila atakayeisema CHADEMA au kila kikitajwa chama kingine basi linafunguliwa 'box la Lusinde'. JF ni majukwaa ya GTs, lusindeism inaharibu hadhi hiyo.
 
Kwa hiyo unataka kusema mtei alikuwa ana uwezo wa kufikiria kuliko baba wa taifa?maanake alishindwa kupambana na dudu ubepari,kwa kuwa hakuna wa kulizuia.....kwa hoja yako mtei aliona mbali,maana aliona haiwezekani kujitenga na ifm,,,
 
hujaeleza historia ya chama, ila umeeleza ubaya wa chama, mimi sijakuelewa kabisa
 
Ninaendelea kutafakari ni kwa kiasi gani katika nchi zilizotawaliwa na mkoloni, na hususan zinazoendelea kuwa katika umaskini kama wa Tanzania, vyama vya siasa vina jeuri ya kuchagua kwa hakika mifumo ya kiuchumi na itikadi za kisiasa.
 
mkubwa! Annael unakumbuka vizur nilikwambia wewe ni mwana magamba,tena damudamu na mpenzi wa CCM? nakumbuka ulikuja juu sana na kukana kuwa wewe si mwanaCCM,na nikawa nakuliza kwanini unajificha?
Sasa naomba leo uniambie kutokana na Thead yako hii utakanusha kuwa wewe ni adui wa CHADEMA na upo hapa jamvini kwa posho ilimladi kuizushia uongo CDM?Naomba majibu tafadhari kwa kila swali langu
anaeli kichwa kimejaa majivu,hana tofauti na nape.
 
Mimi sija sema hakina uhalali kisheria hapa ni mfumo wake jinsi ulivyo.

1. Ninataka ulete historia ya chadema na utendaji wake wa kazi.
2. Ni kwanini Nyerere na Mtei walikorofishana na ikapelekea Mtei ahame na kuanzisha CHADEMA?
3. Nieleze kwanini Kaburu alihama CHADEMA na kurudi CCM?
4. Nchi kama ya china si ya kibepari lakini ndio sasa inayo tisha kiuchumi duniani. So sisi watanzania hatutaki Kuwa na UTAWALA BORA bali UONGOZI BORA, hii ndio MSINGI MKUU WA CCM.

CCM wamejikwaa sasa wanarejea mwanzo.


Nikuulize swali na unijibu usikwepe. Msingi mkuu wa CHADEMA ni nini?

Ndugu inaelekea umeamua kuchagua kutokuelewa hoja zako wala hazina mashiko lakini ngoja nikufahamishe kuwa Mzee Mtei alikorofishana na Julius Nyerere miaka mingi kabla ya chadema kuanzishwa, na msingi wa ugomvi wao ni Nyerere kukataa ushauri wa Mzee Mtei kukubali masharti ya IMF, na Mzee mtei ni mtaalam wa uchumi na alikuwa na fact za kumshauri mzee Nyerere lakini mzee wetu yule kwa kiburi tu na kuchukia kwake ubepari alikataa na madhara ya ubishi wake sote tunayajua nikukumbushe tu ni sukari, chumvi unga, sabuni, majani ya chai vyote hivi vilikuwa kwa foleni! baada ya Kuona amechemsha na kwa kuwa hakutaka kulamba matapishi yake ndio mzee Nyerere alipojiuzulu na kumpisha Alhaji Mwinyi ambaye alifungua milango kwa ubepari na the rest unajua! kuhusu Kaborou kuhama chadema ni kwa kuwa alikuwa hakubaliki ndani ya chama na damu yake ilikuwa ni ya kifisadi kama magamba ndio maana akatoka! hahaha umenena vyema kuwa watanzania hatutaki kuwa na utawala bora bali uongozi bora na ndicho hasa chadema wanachofanya, labda nikukumbushe CCM huwa wanajiita chama tawala, sasa si chama tawala hutoa watawala au sivyo! lakini CDM kinajulikana kama chama Kiongozi cha upinzani, sasa chama kiongozi hutoa viongozi!
 
hujaeleza historia ya chama, ila umeeleza ubaya wa chama, mimi sijakuelewa kabisa
Katokumbi,
Pengine ili kukijua chama vizuri, historia yake, mazuri na mabaya yake, malengo yake ya wazi na yaliyofichika vyote ni muhimu.
 
Kama huna hoja kaaa kimya mbona haya yameishaongelewa mara hamsini kasoro moja hapa!
 
hadanganyiki mtu upepo unaondoka na nyumaba nzima si paa tu mpende msipende halali mtu CHADEMA ndilo tumaiini pekee
 
Ubepari tatizo lake ni kwamba mwenyenacho ndie anayepata na siye nacho ataendelea kuwa mnyonge.

Ni tofauti kabisa na mfumo wa kijamaa.
Jaribu kujikumbusha Uraia au siasa darasa la tatu shule ya msingi.

Sio ndo sera ya magamba! au?
 
Ni sawa Ruttashobolwa, hata mimi napinga kwa nguvu zote huu utamaduni wa kila atakayeisema CHADEMA au kila kikitajwa chama kingine basi linafunguliwa 'box la Lusinde'. JF ni majukwaa ya GTs, lusindeism inaharibu hadhi hiyo.
Nimefurahia upembuzi wako.

Tatizo la mtoa mada hakuja kwa kujifunza, ila kutetea kile anachokiamini bila kuwa na hoja wala falsafa anayosimamia. Na hivyo ndivyo mashabiki wa siasa yetu wote walivyo, si chadema, cuf wala ccm. 85% to 90% ya wanachama na mashabiki wa siasa katika nchi za kiafrika. Hawapo tayari kuumiza vichwa kupembua mambo, wanapenda personality ya watu, wanapenda hadi majina ya vyama, pasi kujali sera na falsafa zao. Leo chadema wakisema ni kinaamini ujamaa mashabiki wake watakandia ubepari, kesho kikibadilika na kuamini ubepari mashabiki walewale watakandia ujamaa. Tupo tupo tu. Ndio maana nasema "Demokrasia sio mfumo sahihi kwa Afrika, bado sana" UBUNIFU HAUJAWAI KUFIKA MWISHO, NAFASI TUNAYO NA TUNAWEZA. Nguvu yetu ni UMOJA na KUTHUBUTU.
Mungu wetu anaita.
 
Chadema ni chama kilichoanzishwa kwa mfumo wa kibepari. Kwahiyo Msingi mkuu wa chadema ni ubepari.
Mwanzilishi wa Chadema ni Mzee Mtei ambaye alitofautiana na baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Tofauti yao ni kuhusu sera za IMF Mtei alikuwa anaunga mkono bali Nyerere alikataa sera za kibepari.

Kwahiyo Sera za kibepari msingi wake mkuu ni mtaji (Pesa).
Kimekuwa kikipata misaada ya chini chini kutoka katika nchi za magharibi kama Uholanzi na zingine, kitendo ambocho kinanipa mashaka kuwa vipi pesa hizo zitalipwa. Ninadhani kuna makubaliano ya chini kwa chini ambayo watu wengi hatuyajui.

CHADEMA kimejitahidi sana kuwafundisha wanachama wake kutohoji mapato na matumzi ya chama. Hii ni mbinu ambayo imetumiwa na CHADEMA kuwaaminisha wanachama dhidi ya viongozi kuwa wao hawana doa.

na hii ni hatari sana.

mbona ccm na mkewe cuf wanapata mipesa kutoka iran na oman na nchi mbalimbali za mashariki ya kati?? sasa angalia ukiwasikiliza watu wa ulaya hata kama watakuibia uchumi wako utakuwa kama wa RSA, Botswana, Kenya, Mauritius nk Lakini ukijawa ngebe ukawasikiliza jamaa wa mashariki ya kati hata kama hawatakuibia uchumi wako utakuwa kama wa Somalia, Eritrea nk na jamii yako itajaa malumbano yasiyokoma, mtagawanyika, mtachomeana makazi, mtanyimana ajira, kila kitu kitakuwa ni kati ya sisi na wao halafu twiga wenu watapandishwa ndege bila hiari zao, swala wenu watawindwa kikatili na wake zenu watajificha uso mitaani hata kama kuna jua la kuchemsha maji. Uchaguzi ni wako kusuka ama kunyoa!!!!
 
Back
Top Bottom