Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,371
- 39,186
Nimefanya kautafiti ka haraka haraka na kugundua kuwa Watanzania wanashukuru kwa namna tofauti kwa kufuata jinsia zao. Na hasa pale ambapo wanajibu shukrani zinazotelewa kwao kwa kiingereza au kwa kiswahili. Hawa hasa wale walioko nje ya nchi.
Kina Dada:
Ukimwambia dada wa Kiswahili "Thank you" anajibu kwa Kiingereza "You are welcome".
Ukimwambie dada huyo huyo "asante" yeye anajibu "Karibu" (akitafsiri 'you are welcome')
Kina kaka.
Ukimwambia kaka wa Kiswahili "thank you" atajibu aidha "you are welcome" au "no problem man/hun.etc"
Ukimwambia kaka huyo huyo kwa Kiswahili "asante" yeye atasema "hamna neno, pouwa," au atajibu kwa kiingereza "anytime man, no problem" lakini hasemi "you are welcome" - ni nadra au hasemi kabisa "karibu".
Lakini ukienda kwetu kule Usukumani ukimwambia mtu "wabecha" jibu utakalolipata bila kujali jinsia ni "wabecha kulumba". Sasa siku hizi wakazi wengi wa maeneo ya Usukumani na labda imeanza kuenea maeneo mengine ya Tanzania ukiwaambia kwa kiswahili "asante" wanasema "Asante kushukuru" wakitafsiri "wabecha kulumba".
Sasa:
Mtu anapokushukuru kikwenu, jibu lake linaendena kwa ukaribu na "you are welcome" au linaendana kwa ukaribu na "asante kushukuru"?
Unafiriki kwa lugha yetu, ili ni jibu sahihi mtu anapokushukuru kwa Kiswahili na kusema "asante"? Na ipi inapaswa kufaa?
Kina Dada:
Ukimwambia dada wa Kiswahili "Thank you" anajibu kwa Kiingereza "You are welcome".
Ukimwambie dada huyo huyo "asante" yeye anajibu "Karibu" (akitafsiri 'you are welcome')
Kina kaka.
Ukimwambia kaka wa Kiswahili "thank you" atajibu aidha "you are welcome" au "no problem man/hun.etc"
Ukimwambia kaka huyo huyo kwa Kiswahili "asante" yeye atasema "hamna neno, pouwa," au atajibu kwa kiingereza "anytime man, no problem" lakini hasemi "you are welcome" - ni nadra au hasemi kabisa "karibu".
Lakini ukienda kwetu kule Usukumani ukimwambia mtu "wabecha" jibu utakalolipata bila kujali jinsia ni "wabecha kulumba". Sasa siku hizi wakazi wengi wa maeneo ya Usukumani na labda imeanza kuenea maeneo mengine ya Tanzania ukiwaambia kwa kiswahili "asante" wanasema "Asante kushukuru" wakitafsiri "wabecha kulumba".
Sasa:
Mtu anapokushukuru kikwenu, jibu lake linaendena kwa ukaribu na "you are welcome" au linaendana kwa ukaribu na "asante kushukuru"?
Unafiriki kwa lugha yetu, ili ni jibu sahihi mtu anapokushukuru kwa Kiswahili na kusema "asante"? Na ipi inapaswa kufaa?