Unavutiwa kua na mtoto /watoto?
Watoto wako wamebadili nini kwenye maisha yako?
Wameongeza nini kwenye maisha yako?
Mara nyingi mtoto akiwa mchanga huvutia sana
Namna alivyo na sura yake ya upole anaporusha miguu na mikono huku akikutazama huwa ni jambo la kupendeza sana kuangalia🤗
Mtoto akifika hatua ya kukaa chini, kucheka na kuonyesha yale mapengo yake madogo ya meno, huwa anavutia mno
Watoto wa umri huo wana namna ya kugusa moyo, especially anapokushika shavu na kutabasamu☺️
Na anapoanza kujifunza kutembea, vile anavyotembea, kuanguka kisha kuinuka tena, huwa ni raha kubwa sana kumuona
Kuna happiness ya kipekee ndani yake
Pia kuna feeling nzuri sana pale mtoto anapoanza kuita mama baba dada au jina lako
Kusikia mtoto anakutambua na kujua wewe ni nani kwake, huwa kunagusa moyo sana
Mimi binafsi hupenda sana kumbeba mtoto, kumkumbatia na kumbusu
Hali hiyo hunipa amani, utulivu na furaha ya ndani yaan nahisi msisimko ajabu
Mara nyingi nikimuona mtoto mdogo akiimba au akifanya kitu kizuri, huwa najikuta nikipata furaha mpaka machozi kunilenga
Kwa kifupi, napenda watoto sana
Huwa nawaona kama malaika wenye kuleta upendo, amani na utulivu
Dear children🥰 nyie ni kama maua yanavyochanua ndani ya bustani, like the sun rising and setting with its own beautiful light
Tabasamu lenu wakati mwingine huponya nafsi zilizochoka na kuleta peace ndani ya mioyo ya watu
I truly love children😍
Mna nafasi kubwa sana ndani ya moyo wangu 🤍
Wewe unapenda watoto?
Unatamani kupata watoto wengi?
Au huvutiwi kabisa na watoto?