Unapenda watoto?

Unapenda watoto?

ShesRise_1

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2025
Posts
8,711
Reaction score
20,957
Unavutiwa kua na mtoto /watoto?

Watoto wako wamebadili nini kwenye maisha yako?

Wameongeza nini kwenye maisha yako?

Mara nyingi mtoto akiwa mchanga huvutia sana
Namna alivyo na sura yake ya upole anaporusha miguu na mikono huku akikutazama huwa ni jambo la kupendeza sana kuangaliašŸ¤—

Mtoto akifika hatua ya kukaa chini, kucheka na kuonyesha yale mapengo yake madogo ya meno, huwa anavutia mno

Watoto wa umri huo wana namna ya kugusa moyo, especially anapokushika shavu na kutabasamuā˜ŗļø

Na anapoanza kujifunza kutembea, vile anavyotembea, kuanguka kisha kuinuka tena, huwa ni raha kubwa sana kumuona

Kuna happiness ya kipekee ndani yake

Pia kuna feeling nzuri sana pale mtoto anapoanza kuita mama baba dada au jina lako

Kusikia mtoto anakutambua na kujua wewe ni nani kwake, huwa kunagusa moyo sana

Mimi binafsi hupenda sana kumbeba mtoto, kumkumbatia na kumbusu
Hali hiyo hunipa amani, utulivu na furaha ya ndani yaan nahisi msisimko ajabu

Mara nyingi nikimuona mtoto mdogo akiimba au akifanya kitu kizuri, huwa najikuta nikipata furaha mpaka machozi kunilenga
Kwa kifupi, napenda watoto sana
Huwa nawaona kama malaika wenye kuleta upendo, amani na utulivu

Dear children🄰 nyie ni kama maua yanavyochanua ndani ya bustani, like the sun rising and setting with its own beautiful light

Tabasamu lenu wakati mwingine huponya nafsi zilizochoka na kuleta peace ndani ya mioyo ya watu
I truly love childrenšŸ˜
Mna nafasi kubwa sana ndani ya moyo wangu šŸ¤

Wewe unapenda watoto?
Unatamani kupata watoto wengi?
Au huvutiwi kabisa na watoto?
 

Attachments

  • file_00000000a37c720b98b0eb57eb836d8f.png
    file_00000000a37c720b98b0eb57eb836d8f.png
    2.3 MB · Views: 15
Yaani we acha tu..
Hapo ndio unaanza kujua kuna viumbe wengine unaishi nao, na kuwa mpole tu maana utajipa kesi mahakamani ukiwa mapepe....
Kuna watoto ni pasua kicwa aisee mimi mama aliniambia nilikuaga pasua kicwa
Japo siamini🤣
na kwakumbuku zangu nilivyoonza kujitambua nimechapwa aiseee mom alikua mkalii moto
 
Back
Top Bottom