Unamkumbuka Dk. Leakey Abdallah?

Unamkumbuka Dk. Leakey Abdallah?

Huyu ndio alitakiwa kuwa mwalimu wa wachambuzi yani uwezi kuona kasoro.
Leo baba levo naye ni mchambuzi
Halafu kuna wale watu wa TV3uchambuzi wao huwa unanishangaza sana. Pia kuna Kitenge, yeye hafichi mapenzi yake kwa Yanga, na hafichi CHUKI yake kwa Simba. Hii fani imevamiwa!
Miaka ile ndiyo nilimfahamu Haji Manara. Mpira na historia yake, anajua sana. Pia, kipindi hicho, wakajitokeza huyu 'MWANAHARAKATI HURU' Musiba, akiwa na huyu aliyekuwa Katibu Mkuu msaidizi Zanzibar, CHADEMA Salim Mwalim, pale Channel Ten!
 
Sitamsahau alichambua final ya Arsenal vs Barcelona 2006.
Akasema Arsenal atafungiwa 2_1
Na Arsenal atapata red card na kweli Aluminia alipata red card
Wale wenye jicho la mpira wanaona kabla mechi haijachezwa kutokana na tabia za wachezaji.Mfano unajua kabisa beki za yanga zitasababisha penalty kumkaba Mpanzu au Kibu hivyo mashabiki wao wanaanza kampeni ya propaganda eti Simba anapata penalty za mchongo
 
2006 fainali ni kati ya Italy na France sio Germany.

Tukio maarufu ni red card ya Zidane kufuatia kumtwika kichwa Gattuso.

Recheck your facts.
😂😂Gatutuso!! Afu unamlazimisha mwenzio acheki facts zake🙌🙌🚶
 
Wakati huo mi mdogo.

Anapanga logic vizuri na reference za kutosha.

Kuna kipindi walidai kuna kampuni ya kubet imemuajiri kisa kawapiga sana. Sijajua usahihi wa hii kitu.

Ila baada ya kuijua internet nikajua ukiachilia maarifa na mapenzi yake ya mpira inawezekana alikua step ahead kwa kukisoma anachotakiwa kukichambua ndiyo sababu alikua vizuri mno.
 
Back
Top Bottom