Dah niko hoi kwa kucheka..unanikumbusha mbali watu walivyokuwa wanakimbizwa mabwawa saba..haaa beach kidimbwi lol jamani tumetoka mbali..
Rest in Peace my "fiancee wa kitoto toto....Mary Abonike,nikikumbuka haya mambo ya chinjachinja sijui nyonya damu namkumbuka sana Mary wangu,1991 tukiwa Mwadui A Primary School,tunapita pembezeni mwa barabara ya boidi,mara mwanafunzi mmoja akatushitua kuwa mnyonya damu wa kijiji cha Utemini anakuja...katika harakati za kukimbia tukajichomeka kwenye barabar...Gari aina ya Peugot ukatupitia...nilivunjika mkono na mguu...lakini mwenzangu Mary alifia Hospitali ya Misheni pale Mipa...
Alikuwa jirani na "mchumba" wangu wa kombolela na mchezo wa chekecha...darasani hadi kanisani pamoja..tukapewa kipaimara na Askofu Castor Sekwa(R.I.P) Parokia ya Msalaba Mtakatifu-Mwadui...sijawahi kumsahau wala kulisahau tukio la kumkimbia Mnyonya damu...picha za kipaimara na mazishi ninazo...hunipa kumbukumbu ya rafiki wa utotoni niliompoteza kwa vitisho ambavyo leo nakuja kujua havikuwepo....R.I.P MARY ABONIKE
Pia unakumbuka ukimuona mlemavu ngozi kwa mbali unatemea mate kifuani
Rest in Peace my "fiancee wa kitoto toto....Mary Abonike,nikikumbuka haya mambo ya chinjachinja sijui nyonya damu namkumbuka sana Mary wangu,1991 tukiwa Mwadui A Primary School,tunapita pembezeni mwa barabara ya boidi,mara mwanafunzi mmoja akatushitua kuwa mnyonya damu wa kijiji cha Utemini anakuja...katika harakati za kukimbia tukajichomeka kwenye barabar...Gari aina ya Peugot ukatupitia...nilivunjika mkono na mguu...lakini mwenzangu Mary alifia Hospitali ya Misheni pale Mipa...
Alikuwa jirani na "mchumba" wangu wa kombolela na mchezo wa chekecha...darasani hadi kanisani pamoja..tukapewa kipaimara na Askofu Castor Sekwa(R.I.P) Parokia ya Msalaba Mtakatifu-Mwadui...sijawahi kumsahau wala kulisahau tukio la kumkimbia Mnyonya damu...picha za kipaimara na mazishi ninazo...hunipa kumbukumbu ya rafiki wa utotoni niliompoteza kwa vitisho ambavyo leo nakuja kujua havikuwepo....R.I.P MARY ABONIKE
Hivi jamani hili suala ni nani alikuwa analianzisha ?maana katika miaka yangu yote 7 ya primary school sijawahi kuwashuhudia though story zilikuwa haziishi..siku nyingine tunanusurika na kuumia kisa mmoja kalianzisha kaona wanyonya damu.je ni kweli walikuwepo ama ilikuwa ni imani tu
Hahahaaaa.....Ware wa kure kwetu enzi za primary, ilikuwa inasemekana kuwa kuna watu wanaiba watoto na kwenda kutoa KAFARA migodin...
Enzi hizo alivuma mzee mmoja kwa jina MALEMBERA ambaye alikuwa anamiliki mashimo kadhaa ya Dhahabu NYAMONGO, Sasa wakawa wanasema huyo mzee alikuwa akipiga hizo issue....Basi mtoto ukitishiwa tu... "Malembera huyo yuaja...mbiooooooo, au hata kama kuna kitu umezuiwa kufanya hutofanya ukihofia utapelekwa kwa huyo Mzee.....
Aione: Think pad, Mwita Maranya na platozoom...
Malembera alivuma si kidogo, nasikia kwenye harusi yeye alikuwa wa mwisho kutaja zawadi kwa Wanaharusi, ilikuwa balaa. Kuna wakati aliweka rekodi ya mtu aliyeuza dhahabu nyingi kwa NBC Bank.
Ila hivi sasa nasikia yuko hoi kifedha!!
ilikuwa mwaka .1994 nipo la tano mwalimu mkuu alienda mjini hukunyuma ikazuka kaenda kuchukua wanyonya damu wee shuleni hapakutosha!
Umeona ee!
Mie yule mlinzi babu wa pale Tahfif alikuwa ananikeraga na mikwara bubu yake.
Cathedral Book Shop pale.
Nakumbuka siku moja wakati wa mapumziko tulienda pale TTCL kuchezea lifti, tusikwame nini, tulilia...ilibidi mwl mkuu Fadhil aje kututambua kama sisi ni wnfnz wake baada ya kunasuliwa.
Tulipofika skuli tukaambiwa tunaitiwa nyonya damu ili watunyonye...mama weee...nilivyomponyoka mwl ni mbio mpaka ofsn kwa dad (r.i.p).
Jamani utoto...hasa wa kimjini, raha sana.
Heheheheh usinikumbushe
Wakati niko darasa la pili
Kida lilikuja gari jekundu sijui nani akatangaza kuwa ni la wanyonya damu
Ilikuwa patashika shule nzima
class letu lilikuwa halina madirisha ya nyavu wala hakuna frem..ni kama boma, basi ukisikia tu 'manyonya' unachomoka ktk uwazi wa dirisha home hapo hadi kesho....... kimsingi sijawahi kuwaona ila nimekimbia mara nyingi
morogoro hiyo!Kinondoni?
Aisee kumbe we mtata tangu utoto yani orijinaly mpk ofice za ttcl@ Madame B....mlikua darasa la ngapi hapo...tahfif kuna watu walikua wanaibaga sometimes achaaa
Mitaa hiyo tulikuwa hatukatizi tukija kuokota maembe chuo kikuu hahaha.
Yani we acha tu.
Nilikuwa mtata mwisho.
TTCL mama alikuwa anafanya kazi, basi nakwambia twachukuana haooo...
Ni panda shuka...panda shuka.
Hapo niko drs la 3.
Tukitoka hapo twaenda Snow Cream.
Dereva wa home akitufata ye ndio akatuchukulie mabegi ya Dino shule,unayakumbuka?
Tahfif tumedokoa sana vipenseli, viufutio...