Unakumbuka wanyonya damu mashuleni?

Unakumbuka wanyonya damu mashuleni?

Ablessed, hapo kwa red umechapia! Enzi hizo, mifuko ya rambo haikuwepo, ilikuwepo mifuko ya karatasi pia mifuko ya nguo, kitambaa cha khaki-ngumu.
Hapana ilikuwepo mifuko ya nailoni lbd kama nimekosea jina lkn ilikuwepo hapo nazungumzia miaka ya 82-89 hapo katikati sikumbuki ilianza kuwepo mwaka gani hasa tena ilikua ya blue hivi.
 
enzi hizo haina cha mtoto wa tajiri wala nini,sote tunasoma shule moja tu.
Ilikua raha sana watoto wa wakubwa tulikua nao class moja . Nakumbuka ukichaguliwa kwenda sec huko ndio unakutana nao wengi tu na wote mnaheshimiana na kuishi kwa upendo. Tena shule za sec za serikari hapa dar zilikua chache sana so walilazimika kwenda boarding hasa walipofika high school. Kulikua na shule moja tu yenye mchepuo wa science kama pcb ilikua jangwani tu so ni lazima high school uende boarding sasa huko mkifika maskini watoto wa wakubwa hawawezi kushika jembe lkn walilishika na wote mlikimbia mchaka mchaka. Kwa sasa kuna matabaka sana kati ya wenye nacho na wasio nacho.
 
Mnakumbuka mazingaombwe eti mtu anazaa chura. Pia kuikua na uhaba wa uniform basi tukawa tunavaa sketi nyeupe wanaita marudufu kama sikosei. Enzi zile zilikua na raha yake sisi watoto wa wakulima nakumbuka tulikua tunabeba mifuko ya Rambo au karatasi au kama wazazi wakiweza unashonewa mfuko wa nguo. Vipi viazi mbatata vilivyokua vinapikwa shule tunauziwa senti 20 kwa kipande na mchuzi wa Nazi basi mtamegeana hadi basi.

mifuko ya nguo hasa kalenda za kiwanda cha urafiki, kiltex, tanganyika textile etc........
 
hii thread imenifurshisha sana na kuondoa stress zoote mungu awabariki sana... inanikumbusha enzi hizo vingunguti B primary school
 
Huyu sekeni alikuwa ni mafia balaa, maarufu kama chinja chinja.
Huyu mi namfahamu alikuwa maarufu sana pande za ndiwili,watu kibao washauliwa
jamaa lilikuwa na midevu afu miguuni halivai kitu,ukipewa lifti tu ujue gari haisimami hadi kusikoeleweka !!
 
Umenikumbusha Forodhani Primary.
Enzi hzo tuko drs la 3.
Kuna gari flani la Red Cross liliingia pale shule kwa minajiri ya kugawa First Aid Kit kwa mwl mkuu Bw. Saiwad.
Sasa pata picha kilichotokea...afu sasa yule baba mhindi alikuwa amevaa gloves na nguo nyeupe, akaja moja kwa moja kule juu darasani.
Kama si busara za masista siku hiyo...sijui kama mngemjua Madame B.
Tulipagawa mpaka wengine tulizima chali.
madam B nakufananisha au ndio wewe
 
Rest in Peace my "fiancee“ wa kitoto toto....Mary Abonike,nikikumbuka haya mambo ya chinjachinja sijui nyonya damu namkumbuka sana Mary wangu,1991 tukiwa Mwadui “A“ Primary School,tunapita pembezeni mwa barabara ya boidi,mara mwanafunzi mmoja akatushitua kuwa mnyonya damu wa kijiji cha Utemini anakuja...katika harakati za kukimbia tukajichomeka kwenye barabar...Gari aina ya Peugot ukatupitia...nilivunjika mkono na mguu...lakini mwenzangu Mary alifia Hospitali ya Misheni pale Mipa...
Alikuwa jirani na "mchumba" wangu wa kombolela na mchezo wa chekecha...darasani hadi kanisani pamoja..tukapewa kipaimara na Askofu Castor Sekwa(R.I.P) Parokia ya Msalaba Mtakatifu-Mwadui...sijawahi kumsahau wala kulisahau tukio la kumkimbia Mnyonya damu...picha za kipaimara na mazishi ninazo...hunipa kumbukumbu ya rafiki wa utotoni niliompoteza kwa vitisho ambavyo leo nakuja kujua havikuwepo....R.I.P MARY ABONIKE

dah! Pole sana kaka kwa ulimbukeni wetu.
 
utoto raha jamani na mtu unaamini kabisa.gari likiwa tinted ni la wanyonya damu.kkh enzi za shule unanunua kitu unakitemea mate ili usiombwe,maana kitu kidogo utaombwa wee kila mtu umkatie.ukinunua soda na chipsi yaani wewe ni mtu mwenye hela
 
Best ilikuwa tu imani ile ya watu
Hivi jamani hili suala ni nani alikuwa analianzisha ?maana katika miaka yangu yote 7 ya primary school sijawahi kuwashuhudia though story zilikuwa haziishi..siku nyingine tunanusurika na kuumia kisa mmoja kalianzisha kaona wanyonya damu.je ni kweli walikuwepo ama ilikuwa ni imani tu
 
zamani watu wengi waliokuwa na uwezo ktk jamii walihusishwa sana na hili swala, zama hizi ukifanikiwa kimaisha utaskia "jamaa fliimaason" kama siyo freemason basi utazushiwa kuwa unauza sembe.
 
Back
Top Bottom