Unakumbuka wanyonya damu mashuleni?

Unakumbuka wanyonya damu mashuleni?

class letu lilikuwa halina madirisha ya nyavu wala hakuna frem..ni kama boma, basi ukisikia tu 'manyonya' unachomoka ktk uwazi wa dirisha home hapo hadi kesho....... kimsingi sijawahi kuwaona ila nimekimbia mara nyingi
 
class letu lilikuwa halina madirisha ya nyavu wala hakuna frem..ni kama boma, basi ukisikia tu 'manyonya' unachomoka ktk uwazi wa dirisha home hapo hadi kesho....... kimsingi sijawahi kuwaona ila nimekimbia mara nyingi
hahahaha kweli ni wengi sana tumekimbia tena marathon haswaaaa but akuna aliyewahi kushikwa hata mkono na mkimbizaji lol
 
Umenikumbusha Forodhani Primary.
Enzi hzo tuko drs la 3.
Kuna gari flani la Red Cross liliingia pale shule kwa minajiri ya kugawa First Aid Kit kwa mwl mkuu Bw. Saiwad.
Sasa pata picha kilichotokea...afu sasa yule baba mhindi alikuwa amevaa gloves na nguo nyeupe, akaja moja kwa moja kule juu darasani.
Kama si busara za masista siku hiyo...sijui kama mngemjua Madame B.
Tulipagawa mpaka wengine tulizima chali.
 
Last edited by a moderator:
unataka nibanwe lini?

Mtondojogoo na nataka ubanwe na mavi na mkojo kwa mpigo ili nikuchezeshe kindumbwendumbwe.

Kindumbwendumbwe chalia
Kikojozi kakojoa na nguo kazinyea
Kikojozi nani huyo
Kikojozi Mwajuma huyo
 
Mtondojogoo na nataka ubanwe na mavi na mkojo kwa mpigo ili nikuchezeshe kindumbwendumbwe.

Kindumbwendumbwe chalia
Kikojozi kakojoa na nguo kazinyea
Kikojozi nani huyo
Kikojozi Mwajuma huyo

utantapisha vyuku vyangu ujue. khaaa! halafu inaonesha ulikuwa unajikojolea sana utotoni.
 
Chemwali umenikumbusha mbali.sisi kwetu kuna baba mpaka amekufa tunaamini alikuwa mnyonya damu.

Haaahahaahaa🙂 Tulikuwa tunawaita MUMIANI-hadi le0 sijui jina lilit0kea wapi!
 
Dah! hii ni moja ya 'hoax' ambazo zilishika hatamu miaka hiyo tukiwa bado makinda...

Nakumbuka nikiwa Mbeya kuna jina la Msekwa(sio Pius Msekwa) lilikuwa maarufu sana...

Na kipindi kile mji haukuwa umejengwa sana kwani kulikuwa bado na ule uoto wa misitu ya mikaratusi...

Sasa ilikuwa inasemekana huyu bwana ni nyonya damu na anatembelea kibito chekundu na hakitoi mlio...

Suala la kwenda shule asubuhi na mapema au kurudi nyumbani kigiza kikiwa kimeingia ilikuwa tafrani sana...

Dah! Huyu msekwa alivuma sana mkoan Tanga, korogwe na handen alitisha watu tulikuwa hatuchezi mbali na nyumban
 
Tena walikua wanasema nyonya damu anakunyonya damu halafu anakuachia damu hadi ya kukufikisha nyumbani na kama ukiwa home unatakiwa unywe chai ya rangi nyingi yenye majani mengi bila ya sukari eti ndo utapona na kurudisha damu
 
Back
Top Bottom