Unajisikiaje ukikutana na Rafiki zako mliosoma wote kipindi hicho, wako mbali sana kimaisha

Habari za Jumapili wanajukwaa,Pia poleni na majukumu ya kutafuta mkate wa kila siku.Niende kwenye mada husika hapo juu hivi huwa unajisikiaje hasa pale unapokutana na rafiki zako mliosoma wote kipindi hicho wako mbali sana kimaisha kuliko wewe?

Kwa Upande wangu hii imenikuta wakati natoka Kanisani na stress nyingi zimejaa kwenye kichwa ghafla napigiwa honi na Gari nyeusi aina ya BMW X5 nikashituka kuona linapaki pembeni na Mtu anashuka ananiita jina langu la Ukoo! Nikamkubuka ni rafiki yangu tuliyesoma wote.
Advance Level ila yeye Alibahatika baada ya kutoka mujibu wa sheria alijiunga na Taasisi nyeti, hapa nchini kwa sasa ni Afisa mkubwa.

Kwa upande wangu akaniuliza "ndugu kwa sasa unapiga mishe gani?", ikabidi niwe muwazi nikamwambia kwangu bado mambo hayajakaa sawa japo,nilijisikia Aibu kidogo yaani niliyekuwa nampita class,namfundisha kila siku,tunakesha wote kwenye madesa kashanizidi ilihali mimi bado sioni mwanga.

Nikajisemea Moyoni "basi mpaka pale zamu yangu itakapo fika niendele kuwapigia wenzangu makofi kwa tabasamu na upendo."
Nashukuru akanipa lift mpaka home maana nilikuwa sijawahi panda hizi BMW aisee kuna utofauti mkubwa sana na hizi IST. Naishia hapo wakuu Mungu atubariki sote Jumapili njema.
Mim yuko mmoja nilikuwa na mzidi class na mfundisha mno lakin kwakweli amefanikiwa sana tunawasiliana sana hajawai kunidharau tunashirikiana mno tho mwanzo niliumia mno,lakin ajabu mungu akaleta lottery paa aisee. Kweli maisha ya mwanadamu yapo mikononi mwa mungu.ila sitamsahau alijua kunibeba mno nilipokwamwa
 
Mim yuko mmoja nilikuwa na mzidi class na mfundisha mno lakin kwakweli amefanikiwa sana tunawasiliana sana hajawai kunidharau tunashirikiana mno tho mwanzo niliumia mno,lakin ajabu mungu akaleta lottery paa aisee. Kweli maisha ya mwanadamu yapo mikononi mwa mungu.ila sitamsahau alijua kunibeba mno nilipokwamwa
Hongera mkuu
 
Mkuu,hayuko mbali kimaisha bali anamiliki IST na wewe unamiliki miguu yako unafanya mazoezi.Kuwa mbali kimaisha ni zaidi ya kumiliki gari na kuwa na pesa na kazi nzuri.Hivo ni vitu rahisi na vidogo sana.Ukiwa navyo hutaona kama ni issue.Wewe kwa sasa unaona ni issue kwa sababu tu huna.ILA kiukuweli hayuko mbali kimaisha na wewe.Maisha na haya haya na mziki tunaocheza ni mmoja.
 
Back
Top Bottom