Unajifunza nini kuhusu tukio hili

Unajifunza nini kuhusu tukio hili

Mwili umenisisimka ghafla.

Kisha nimeingiwa na simanzi ya ghafla.

Kwa kweli nimeguswa sana na tukio la huyu Dogo
 
Wakati ukihuzunika huna kandambili kuna watu hawana miguu na wanamshukuru Mungu kwa uhai!!
Mungu ni Mwema sana kila kitu anatupa kwa sababu!! Ni ubinadamu tu unatufanya tushindwe kumwambia ASANTE!
Hakika.

Kila Siku tunalalamika Maisha magumu, Mambo hayaendi sawa, na mifano mingine mingi sana ya manung'uniko.

Tujiulize?!

Je mara ya mwisho ni lini tulikaa kitako, tulipiga magoti, tulichuchumaa, kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa zile Neema alizotujalia?

Kuna wangapi tunawafahamu, tunaowafahamu, hivi sasa tunavyoongea wapo Vitandani mwao hawawezi hata kujinyanyua?

Kuna wangapi tunawafahamu, tunaowafahamu, hivi sasa tunavyoongea wanatembelea Magongo, wakati mwanzoni hawakuwa wanatembelea Magongo?

Mifano ni mingi sana.

Tuwe na utaratibu wa KUSHUKURU, kwa kila jambo na kwa kila hali yoyote itakayotukumba/tutakayokutana nayo Kimaisha.

Waungwana Mungu ni mwema sana
 
Dogo kanitia simanzi sana.
Wakati nasoma hii mada nimeshangaa mtoa mada kutoa angalizo...nilijisemea "Habari sensitive kama hii kuna mtu anaweza kuibeza kweli?"
Sijaamini macho yangu kwa comments za baadhi ya members humu.

Aliyenishangaza zaidi ni aliyesema hili tukio limepangwa mpigaji picha alijuaje hili litatokea?

Hivi mbona huwa tunaona picha za ajali,wapiga picha huwa wanapanga ajali zitokee?
Sasa mtu apange tukio kama hili ili iweje?
Dah kweli ubinadamu kazi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom