Unajifunza nini kuhusu tukio hili

Unajifunza nini kuhusu tukio hili

Kajolijo

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2016
Posts
3,364
Reaction score
4,619
Hebu tusaidiane na toa mchango wako juu ya hili, Mtoto alijikuta anatokwa machozi baada ya kugundua kuwa aliyekuwa anataka kumuomba msaada wa hela kwenye gari amewekewa mitambo ya oksjeni imsaidie kupumua,... karibu uchangie ulichojifunza.

NB: mihemuko, matusi na mapovu ni ruksa kwa wale wenye tabia hizo.
1481262784670.jpg
1481262792398.jpg
 
Hebu tusaidiane na toa mchango wako juu ya hili, Mtoto alijikuta anatokwa machozi baada ya kugundua kuwa aliyekuwa anataka kumuomba msaada wa hela kwenye gari amewekewa mitambo ya oksjeni imsaidie kupumua,... karibu uchangie ulichojifunza.

NB: mihemuko, matusi na mapovu ni ruksa kwa wale wenye tabia hizo.View attachment 444156View attachment 444157
Dogo anatafuta hela ya kula wakati mwenzake anapigania uhai wake,

Ukijiona una matatizo kuna waenye matatizo zaidi yako.
 
Hivi kwa umri wa huyo mtoto "Ombaomba" anaweza kua na akili iliyokamaa ya kuguswa na jambo hilo mpaka kutokwa machozi? Nawaza tu.
 
Shetani anawatesa sana watu hapa Duniani ila tusijali kwasababu muda ukifika Mungu atairudisha Dunia ile ya kwenye bustani ya Eden.
Mkuu ni kama sijakuelewa vile! Una maanisha kuumwa kwa huyo mtoto ni kazi ya Shetani?...!!
 
Kuna nyakati zinafika unaona mwenzangu ana hitaji kubwa kuliko la kwangu, huyu mtoto ameona anahitaji pesa kisha kuna mtu anaihitaji oksijeni, kitu cha bure ambacho mwenzangu anakilipia.

Ulimwengu unahitaji idadi ya watu wa hivi waongezeke, haswa haswa viongozi wa nchi zetu.
 
Hivi kwa umri wa huyo mtoto "Ombaomba" anaweza kua na akili iliyokamaa ya kuguswa na jambo hilo mpaka kutokwa machozi? Nawaza tu.
Kwamba hili tukio linaweza kua 'staged' kama kutua kwa vyombo vya NASA kwenye mwezi?
 
Hayo maneno wayasema wewe... lakini hizo picha ahziongei hayo.
 
Yaliyomkumba huyo mtoto pia yalimkumba mtoto mmoja aliyekuwa akimsumbua sana baba yake amnunulie viatu.Siku moja huyo mtoto akakutana na mtoto mwingine ambaye hakuwa na mguu!
Baba hakusumbuliwa tena juu ya viatu kamwe!
 
Tukio la kupangwa.. Kwa akili za mi chokolaa zilivyo hapo dogo angetoka anamcheka mgonjwa ama kumzomea kabisa.. Naijua vizuri hiyo mitoto
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom