Habarini za wakati huu wanajamvi.
Kuna suala hapa la rafiki yangu ambaye yeye ni muajiriwa wa serikalini, lakini kuna suala ambalo linanishangaza sana kila ninapozungumza naye, wakati mwingi yeye anakua anadai kwamba pamoja na hayo yote aliyonayo ila moyo wake unapenda sana kulitumikia taifa katika idara ya usalama. na kwamba ndio kazi ya kwanza anayoipenda sana kuliko zote maishani mwake, na anaipenda kiasi cha kutaka kuwafuata hadi ofisi zao zilipo kwaajili ya kuweza kuzungumza nao kinaga ubaga. na yeye ni muhandisi katika serikalini.
nimeshindwa kumshauri kwakua sielewi kwa kuanzia, na ndio maana nikalileta hili suala mbele yenu.