Kuna watu hawajipendi kabisa, unakuta mtu unamheshimu vizuri tu lakini hajui kuzingatia usafi wake wa mwili. Mtu mzima, unanukaje mdomo, kwapa, miguu, masikio, au pua?
Mf: mambo ya faragha, ukutane na mwanamke na harufu za ajabu-ajabu lol… inakata sana! Kwa wanaume pia inakata asalaleeeee🙌
Hivi shida hua nini? Mfano, mtu kufuga msitu wa Amazon sehemu za siri? 😳 Huoni unakua kero kwa mwenzi wako?
Kuna ugumu gani kuosha kwapa vizuri ili lisiwe shombo? Sugulia hata limao basi 😏
Unakuta mtu akivua viatu… tafrani akhaaa !
Soks, unaiva wiki nzima mfurulizo. Ebooo!
Mdomo, kinywa… yeuwiiiiiiiiii 😬
hiii sehemu ikinuka ina haribu shughuli nzima usisahau kusugua ulimi!
Kama una matatizo ya mdomo tibiwa
Usafi wa sehemu nyeti wewe unafanyaje?
Wax, wembe, jivu, remove hair, mkasi, kipande cha chupa, kunyofoa…?
Karibuni tuzogoe 🫣👌