Unadhani hawajisikii vibaya?

Unadhani hawajisikii vibaya?

Ndio maana tunamlilia Mzee Mengi.Hata kama unakipato na unajua kabisa unaweza anzisha jambo kwa kuajiri vijana wawili au watatu fanya hivyo.Waamini na amini tu japo kuna zile changamoto za hapa na pale.Tupunguze ubinafsi wa roho na tamaa za kutowatazama wengine vibaya.
Ukipata nafasi ya kushauri mtu juu ya kitu cha maendeleo funguka tuache tabia za kuficha ficha mambo ya kimaendeleo.Vijana tunapswa ku share habari njema sana za maendeleo tupunguze vitu vya ajabu ajabu vya kupoteza muda.
Hongera kwa wale walioamua kuwa wakulima wa mboga mboga,Matunda .Wasambaza chakula maofsini na wajasilia amali woote waliamua kupigana na adha hii ya ajira.Sisi tunaoletewa hizo huduma na vijana wenzetu tupunguze Dharau,majivuno na kuwaona watu wajinga wajinga,hasa humu maofisini.Watu wanahangaika kama mlioajiriwa pia.
Wenye nafasi ya kutoa semina na mafunzo mbalimbali basi yalenge kusaidia na si kukamuana.Tuelekezana mambo hasa ya uzalishaji kuendana na wakati huu uliopo na ujao.Vitu vipo vingi na mpo mlio bahatika kuvipitia.Ni vyema tukawa na mioyo wa kusaidiana.
 
 
[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]nakuombea.. Pambana usikate tamaa siku hazigandi
Hii thread ni bonge la thread Aisee, nimeisoma umenipa uchungu kwa sababu Mimi mwenyewe ni msaka ajira kila Siku kukosa

Jr[emoji769]
 
[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]nakuombea.. Pambana usikate tamaa siku hazigandi

Jr[emoji769]
Asante mkuu mshana Jr, huku mtaani vijana wenye degree, diploma, masters tunadhararuliwa sana na wenzetu wale walioshia form four halafu wametoboa!
 
Saveya wasikukatishe tamaa ngoja nikupe kisa changu cha kweli
Nilimaliza chuo mwaka 1993.. Sisi ndio intake ya kwanza ambayo haikukwenda jeshini kwa ajili ya ukata wa serikali, hivyo tukakaa mwaka mzima na zaidi wa 1993/94
Hicho ndio kipindi cha Mwinyi akikaribia kumkabidhi Mkapa kijiti.... Pesa ilikuwa nje nje... Baada ya kusotea sana ajira bila mafanikio nikaamua kuomba kazi kwa wajenzi kama saidia FUNDI... Siwezi kusahau yale manyanyaso na masimango na kejeli
Wale mafundi walikuwa seven leaver.. Lakini kutokana na kupata kazi nyingi za ujenzi walikuwa vizuri kiasi chake... Wakatucheka sana wasomi tulioenda kupoteza muda shuleni.... Nikaifanya ile kazi kwa uvumilivu mkubwa
Lakini bwana asikwambie mtu ukiwa umesoma umesoma tu.. Siku isiyo na jina tajiri akaja na kuniona... Akanihoji Maswali mengi akagundua mimi ni msomi
Siku iliyofuata nikapewa kitengo cha msaidizi wa fundi mkuu upande wa manunuzi na baada ya mwezi nikakabidhiwa kusimamia miradi yote ya mzee... Unaweza ku guess wale ma boss wangu wa kwanza walivyokuwa wakinuna... NIKAWA BOSS WAO
Asante mkuu mshana Jr, huku mtaani vijana wenye degree, diploma, masters tunadhararuliwa sana na wenzetu wale walioshia form four halafu wametoboa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
View attachment 411685
Ni asubuhi ya siku nyingine tena, harakati zimeshaanza na nyingi Zikiwa ni kuwahi kazini au mishemishe pamoja na uchovu wa jana lakini huna budi kuamka na kujiandaa ili uwahi kazini

Ni katika kipindi hiki kwenye hizi harakati za kuwahi kibaruani kuna mtu yuko kitandani muda huu si kwa kupenda la hasha! Anaumia hana kazi naye angetamani muda huu awe anapasi nguo za kazini au yuko barabarani kuwahi

View attachment 411686
Anaumia sana akikumbuka alivyosoma kwa tabu na sasa ni mwaka wa tatu huu hana ajira huku washkaji zake wakipeta(mawazo mabaya huanzia hapa)kwanini na si mimi?kwanini wao wapate na mimi nikose? Kwani tunatofautiana nini? INAUMIZA SANA

Huwezi kuendelea kulala siku nzima utaumwa unaamua kutoka uende kijiweni au ukajaribu bahati yako popote lakini du mfukoni huna hata mia!inauma sana.

Siku yako inapita hivyo hivyo kimungu Mungu na jioni inapokaribia unaanza kuwaona watu wakirudi toka makazini, kwenye magari yao na wengine kwenye usafiri wa jumuiya wengine wamechoka wengine wanapiga story inaumiza mno unatamani na wewe ungekuwa mmoja wao

Unavuta picha jinsi ulivyochomekea na tai yako jinsi ulivyohudumia wateja wako kazini changamoto ulizokutana nazo..unajikuta kabisa ukitumika na kuhudumia kwa furaha unapotelea kabisa mawazoni mpaka unatabasamu, na ghafla unashtuka kumbe uko kijiweni honi ya mshikaji uliyesoma naye inakushtua yuko kwenye altezza anatoka job INAUMIZA SANA
View attachment 411684

tatizo la ajira ni la dunia nzima lakini hii isiwe kisingizio cha serikali...kila mwaka vijana wetu wanamaliza elimu zao wakitegemea kupata ajira...na idadi inaongezeka kila mwaka.. ! Hili linapaswa kuangaliwa kwa umakini zaidi hali ni mbaya sana mitaani
Nice idea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kujiajiri sio dhana rahisi kama inavyochukuliwa na wanasiasa...imagine wewe ni fresh graduate huna mbele huna nyuma huna chochote unaambiwa sio lazima kuajiriwa unaweza kujiajiri
Unapozungumzia kujiajiri unahitaji mtaji , nenda kakope bank uone
Kujiajiri hapa Tanzania inataka mtaji kama huna kitu utabaki kuota.

TRA wanakukadilia kodi mpaka unaogopa bado Brela. Hawa wadau walinifanya niache hata wazo la project yangu, Uganda, Comoro njia nyeupe kufanya biashara unakadiriwa kawaida.

Saizi nimebaki na escape plan ya kwenda kwa Mandela mitaa ya Waterfront, Port Elizabeth na Robin Island nikachezee boti za mkaburu iwe kwa spana au kuendesha.
 
IMG_20200531_072737_186.jpg


Jr[emoji769]
 
Back
Top Bottom