"Una malengo gani na Mimi?"

"Una malengo gani na Mimi?"

Hakuna Swali napata shida kulijibu kama hili.

Mdada(Demu), ambae nimemfuata kwa ajili ya uhusiano wa muda anaponiuliza swali hili huwa nashindwa nijibu nini.

Naogopa kumwambia ukweli, na naogopa kumwambia kitu ambacho anapenda( ndoa).

Pongezi kwa wadada(mademu) ambao huwa hawaulizi swali hili. Huwa wanajiongeza wenyewe.
ukiwa na mtu muite mahali ukiwa serious muulize una mpango gani namimi? Akisita kujibu piga chini, ndo fomula natumia hadi leo
 
Ni swali zuri kimsingi lakini pia linakupa picha umekutana na sampuli ya aina gani ya mwanamke.

Mwanamke mjuaji atakuuliza hilo swali sababu kwenye akili yake ni tayari anawaza ni namna gani hajakuelewa na hajui unamipango gani ambayo kwake inafaida binafsi. Kwa kifupi anataka kujua yeye atafaidika vipi na huo uhusiano.

Sasa kwa mimi hilo swali lingejibiwa na swali. Nitamuuliza hapa tulipo hadi saa hii mimi ni mwanaume ambaye upo tayari kuachana na wazazi wako uje kwangu tuyajenge maisha, katika hali yoyote ya ugumu na mafanikio, magonjwa na afya, kwenye hofu na faraja, shibe na njaa, usiku na mchana, na kusimama katika misingi ya MUNGU?

Ajibu tu ndio au hapana then basi mjadala uishe. Sababu haimake sense mtu ambaye anakuamini anakukubali halafu akuulize swali kama hilo it means hajui yeye amesimama wapi na wewe.
Swali zuri sana hili..
 
Ukiulizwa ni bora useme, hata kama unataka kumchezea ukiulizwa sema..

Mi nikimuuliza mwanaume hilo swali akishindwa kujibu basi safari inaishia hapo
Seriously, unamwambia mdada wa watu, "Nataka kukuchezea". , atakayekubali na aliyekubaliwa wote ni wendawazimu.
 
A genuine man would tell her right away, the genuine mans way.

Japo ndoa ndio ideal lakini sio kila mwanamke anaitaka! Kuwa real hata nguvu za kiume zitakuwa dhatiti maana wasiwasi na wiziwizi(kuuibia mwili wako) itakuwa hamna tena.

Kama mi namuambia tu nnachokitaka kweli. Kama hawezi kuuhandle ukweli basi hanifai iwe ni kwa muda au kwa kudumu damn it.
Ukitumia hizo swaga za u-genuine utachezea vibuti sana mwanamke usipomdanganya kumpata ni ngumu sana, ni wanawake wachache sana utawapata kwa kutumia ukweli
 
Wanaume wengi wasiojitambua hua wanajibu NDOA..

Binafsi ukiniuliza hivo lazima nikufokee seems lyk unataka kunishika sharubu au unanitishia kuachana....
Nahili ndio jibu sahihi, ninani aliekwambia kuwa ukijibiwa kuwa nataka ndoa basi lazima mwisho wa siku lazima itokee ndoa. Au ukiambiwa urafiki basi mwisho wa siku mnaweza msioane, mnakuwa kama mnayaishi maisha ya hadithi za kufikirika kana kwamba matukio ya maisha unayapanga wewe. Msichana ambaye hajakuwa ndio atauliza hilo swali, laasivyo ambaye yupo desperate na ndoa kana kwamba kaumizwa huko mpaka sasa njia aliyobakiwa nayo kujikinga asiumizwe ni kuuliza hilo swali akidhani ndio hata chezewa.
 
Seriously, unamwambia mdada wa watu, "Nataka kukuchezea". , atakayekubali na aliyekubaliwa wote ni wendawazimu.
No si lazima useme nataka kukuchezea direct kuna lugha nyingi za kutumika mbona

Kama ambavyo nyie mkiangalia mnasema huyu napiga ila kuoa hapana na sisi kuna watu tunasema i can date him ila kuolewa nae hapana
 
No si lazima useme nataka kukuchezea direct kuna lugha nyingi za kutumika mbona

Kama ambavyo nyie mkiangalia mnasema huyu napiga ila kuoa hapana na sisi kuna watu tunasema i can date him ila kuolewa nae hapana
Sasa sisi wengine lugha hizo hatuzijui, ni direct answer bila kupindisha. Kuweka jibu gumu liwela sukari ni kipaji.
 
No si lazima useme nataka kukuchezea direct kuna lugha nyingi za kutumika mbona

Kama ambavyo nyie mkiangalia mnasema huyu napiga ila kuoa hapana na sisi kuna watu tunasema i can date him ila kuolewa nae hapana
Sasa sisi wengine lugha hizo hatuzijui, ni direct answer bila kupindisha. Kuweka jibu gumu liwela sukari ni kipaji.
Hao wadangaji ndo utawambia direct answer na watakua comfortable
 
Back
Top Bottom