Una kipawa gani?

Una kipawa gani?

Kila mtu ana kitu kile ambacho mwenzake hana na kila mmoja anatumia kipawa chake kwa usahihi kabisa kuliko mwenzake.

Kipawa na uwezo wa kufanya kitu chochote kile ambacho kinaweza kuwa kigumu kwa baadhi ya watu/mtu (Kipaji)

Naamini kila mmoja anajua kipawa chake hadi sasa kama huna kipawa basi pole sana na Mungu akuoneshe kipawa chako na jinsi ya kukitumia.

Kwangu mimi nina kipawa cha USHAWISHI nasema hili kwa uhakika sana ninaweza kushawishi pande mbili kuwa sawa au pale ambapo hakuna amani kukawa na amani, naweza kubadilisha mtu mawazo yake na akaenda vile navyotaka kwa muda mfupi sana.

Kwangu mimi Najivunia sana kuwa na kipawa hiki wote ambao wamekuwa na mimi wamejikuta wanapita njia yangu, marafiki, wapenzi, ndugu na jamaa.

Kwako wewe una kipi unachoweza kushukuru Mungu kuwa amekupa kitu cha kipekee kuliko yeyote?

Karibu.



Thibitisha mkuu hapo nilipo bold
 
Mimi nadhani kujisimamia. Huwa siyumbishwi hata kidogo katika misimamo yangu hata kama ulimwengu mzima unapingana nami...

Kingine ni kudai. Aisee najua kudai duh! Hata uwe bingwa namna gani kwenye dhuluma, mimi utanilipa tu! Halafu huwa natumia steps ambazo nazipanga kuendana na mdaiwa.
Naomba nkukabidhi mdeni wangu anapiga chenga kunilipa deni langu[emoji22]
 
Kuogelea ni kipawa!? Au mtu unajifunza labda sijaelewa! Kwamfano mtoto anakua amezaliwa na kipawa cha kuimba tangu utotoni yeye anaimba tu akianza kupata akili anaanza kutunga nyimbo! Ndio mm najua hivyo
 
Huruma sijui ndo kujali maana mtu akiwa na shida naumia nakosa amani[emoji27]
 
Ushawishi wa face2face unamaanisha, wa kwenye maandishi huwezi ama?
Naweza sasa kw swali lako kusema nithibitishe hilo siwezi kuthibitisha kwa kitu ambacho hakipo, ina maana kuwa ushawishi utadhihirika pale utakapo nipa jukumu la ushawishi ila hii ya kusema nithibitishe inaniwia ugumu kuthibitisha kitu ambacho hakipo.

Ni kitu kinachoenda na vitendo mkuu.
 
Naweza sasa kw swali lako kusema nithibitishe hilo siwezi kuthibitisha kwa kitu ambacho hakipo, ina maana kuwa ushawishi utadhihirika pale utakapo nipa jukumu la ushawishi ila hii ya kusema nithibitishe inaniwia ugumu kuthibitisha kitu ambacho hakipo.

Ni kitu kinachoenda na vitendo mkuu.
poa sana mkuu
 
Kipawa changu umbea tu, This is not good tho,but ndio kipawa
 
Back
Top Bottom