bless on
JF-Expert Member
- May 22, 2026
- 702
- 1,649
INTELLIGENCE vs KNOWLEDGE! (UFAHAMU DHIDI YA AKILI
Ufahamu (au intelligence) ni kitu ambacho mtu au mnyama au kiumbe hai yeyote anazaliwa nacho, hafundishwi na yeyote.
Intelligence ni tofauti na akili.
Akili ni yale maarifa aliyo nayo mtu kwa kufundishwa.
Akili ni zao la jamii iliyokuzunguka.
Huwezi kuwa na akili zaidi ya jamii iliyokuzunguka, lakini unaweza kuwa na Intelligence kuliko jamii iliyokuzunguka kwa sababu Intelligence unazaliwa nayo, ni kipawa chako, lakini akili unaingiziwa.
Kama ukiondoa kichwani mwako mambo yote ulofundishwa na wazazi, waalimu, jamii yako nk., kile utakachobakia nacho ni intelligence, yaani ufahamu wako ambao ndio wewe mwenyewe halisi.
Intelligence ni kitu ambacho kinamsaidia mtu kuishi katika mazingira yake.
Hata mti una intelligence, ukiona maji yamepungua, unapukutisha majani. Bila kufanya hivyo, hautaweza kuishi, utakufa!
Wanyama hawana akili, lakini wana Intelligence.
Kile kitendo cha mnyama dume kunusa mkojo wa jike na kutambua kwamba jike lipo tayari kupandwa, hiyo ni intelligence, sio akili.
Ndio maana Intelligence ni bora kuliko Akili.
Kwa hiyo, Intelligence unazaliwa nayo, haufundishwi na mtu; kinachofundishwa ni elimu ambayo huwa tunaiita knowledge.
Hiyo knowledge ndio akili yenyewe.
Mfano, umeme ukizima ghafla nyumbani wakati mnaangalia mpira pale sebuleni, lazima mtaulizana pale kama kuna mtu yeyote kati yenu mwenye AKILI ya kurekebisha hali hiyo.
Akitokea mtu 'akakorokochoa' vitu pale na umeme ukawaka, tunasema ana akili kwa sababu ya ile KNOWLEDGE fulani aliyowahi kuipata mahali kuhusiana na suala zima la Elimu ya umeme, iwe formal au informal.
Hii knowledge ni elimu na ndiyo hufundishwa.
Kwa hiyo usichanganye kati ya intelligence na knowledge/ akili (maarifa)
Knowledge huzaliwi nayo, bali unafundishwa, lakini intelligence unazaliwa nayo.
Kwa kadiri unavyoongeza knowledge, ndivyo unavyopoteza au kudumaza intelligence yako.
Wasomi karibu wote wanatumia knowledge (elimu) ili kufanikiwa, wakati wale ambao hawajaenda shule kabisa wanatumia intelligence ili kufanikiwa.
Wengi wa wasioenda shule wana nafasi kubwa ya kufanikiwa kuliko wale walioenda shule kwa sababu Intelligence ni bora kuliko Knowledge.
Ukiondoa ajira asilimia kubwa ya wasomi watakufa kwa presha, lakini wasiosoma wataendelea kupeta kama kawaida kwa sababu wao maisha yao hayategemei knowledge, yanategemea Intelligence!
Hata hivyo, wasomi (wenye elimu) na wasiosoma (wasio na elimu), tatizo lao wote ni moja.
Msomi knowledge yake imeharibiwa na EGO na huyu ambaye hajasoma intelligence yake naye imeharibiwa na EGO pia.
Kumbuka kwamba EGO ni mafundisho ya jamii inayomzunguka msomi na ambaye hajasoma.
Wote hawapo salama dhidi ya EGO.
Wote wameharibiwa na EGO.
Ingawa wale ambao hawajasoma EGO yao ni ndogo, wasomi EGO yao ni kubwa zaidi.
Ufahamu (au intelligence) ni kitu ambacho mtu au mnyama au kiumbe hai yeyote anazaliwa nacho, hafundishwi na yeyote.
Intelligence ni tofauti na akili.
Akili ni yale maarifa aliyo nayo mtu kwa kufundishwa.
Akili ni zao la jamii iliyokuzunguka.
Huwezi kuwa na akili zaidi ya jamii iliyokuzunguka, lakini unaweza kuwa na Intelligence kuliko jamii iliyokuzunguka kwa sababu Intelligence unazaliwa nayo, ni kipawa chako, lakini akili unaingiziwa.
Kama ukiondoa kichwani mwako mambo yote ulofundishwa na wazazi, waalimu, jamii yako nk., kile utakachobakia nacho ni intelligence, yaani ufahamu wako ambao ndio wewe mwenyewe halisi.
Intelligence ni kitu ambacho kinamsaidia mtu kuishi katika mazingira yake.
Hata mti una intelligence, ukiona maji yamepungua, unapukutisha majani. Bila kufanya hivyo, hautaweza kuishi, utakufa!
Wanyama hawana akili, lakini wana Intelligence.
Kile kitendo cha mnyama dume kunusa mkojo wa jike na kutambua kwamba jike lipo tayari kupandwa, hiyo ni intelligence, sio akili.
Ndio maana Intelligence ni bora kuliko Akili.
Kwa hiyo, Intelligence unazaliwa nayo, haufundishwi na mtu; kinachofundishwa ni elimu ambayo huwa tunaiita knowledge.
Hiyo knowledge ndio akili yenyewe.
Mfano, umeme ukizima ghafla nyumbani wakati mnaangalia mpira pale sebuleni, lazima mtaulizana pale kama kuna mtu yeyote kati yenu mwenye AKILI ya kurekebisha hali hiyo.
Akitokea mtu 'akakorokochoa' vitu pale na umeme ukawaka, tunasema ana akili kwa sababu ya ile KNOWLEDGE fulani aliyowahi kuipata mahali kuhusiana na suala zima la Elimu ya umeme, iwe formal au informal.
Hii knowledge ni elimu na ndiyo hufundishwa.
Kwa hiyo usichanganye kati ya intelligence na knowledge/ akili (maarifa)
Knowledge huzaliwi nayo, bali unafundishwa, lakini intelligence unazaliwa nayo.
Kwa kadiri unavyoongeza knowledge, ndivyo unavyopoteza au kudumaza intelligence yako.
Wasomi karibu wote wanatumia knowledge (elimu) ili kufanikiwa, wakati wale ambao hawajaenda shule kabisa wanatumia intelligence ili kufanikiwa.
Wengi wa wasioenda shule wana nafasi kubwa ya kufanikiwa kuliko wale walioenda shule kwa sababu Intelligence ni bora kuliko Knowledge.
Ukiondoa ajira asilimia kubwa ya wasomi watakufa kwa presha, lakini wasiosoma wataendelea kupeta kama kawaida kwa sababu wao maisha yao hayategemei knowledge, yanategemea Intelligence!
Hata hivyo, wasomi (wenye elimu) na wasiosoma (wasio na elimu), tatizo lao wote ni moja.
Msomi knowledge yake imeharibiwa na EGO na huyu ambaye hajasoma intelligence yake naye imeharibiwa na EGO pia.
Kumbuka kwamba EGO ni mafundisho ya jamii inayomzunguka msomi na ambaye hajasoma.
Wote hawapo salama dhidi ya EGO.
Wote wameharibiwa na EGO.
Ingawa wale ambao hawajasoma EGO yao ni ndogo, wasomi EGO yao ni kubwa zaidi.