Una aina ipi ya hasira kati ya hizi?

Una aina ipi ya hasira kati ya hizi?

Pindi unapokosewa ni kipi kati ya hivi hutawala hasira zako

1.KUKAA KIMYA / KUMCHUNIA / KUTOMUONGELESHA ALIEKUKOSEA
2.KUSHOUT / KUGOMBA / KUTUKANA
3. KUONDOKA UKIKOSEWA / KUSEPA / KUMFUKUZA ALIEKUKOSEA
4.KULIA MACHOZI
5. VITENDO / KUMPIGA ALIEKUKOSEA / KUVUNJA VITU
Namba 3 ila hasira ikipoa na nikabahatika kirudi aisee omba sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Me nalala zangu, pia kama Nina hasira nikisoma kitu ndy naelewa sana yan.
 
Mimi nikiwa na hasira kali huwa siwezi kuongea vzr na huwa natetemeka, hivyo basi huwa naamua kukaa kimya au kuondoka eneo la Tukio

Asanteni
Najiona mimi kabisa, when I was too young, nikiwa na hasira sana, nilikuwa nahisi baridi kali, hadi natetemeka, nashindwa kuongea naishia tu kumuangalia aliyenikosea. Hasira sio kitu chema, tunatakiwa tu balance sana.
 
Pindi unapokosewa ni kipi kati ya hivi hutawala hasira zako

1.KUKAA KIMYA / KUMCHUNIA / KUTOMUONGELESHA ALIEKUKOSEA
2.KUSHOUT / KUGOMBA / KUTUKANA
3. KUONDOKA UKIKOSEWA / KUSEPA / KUMFUKUZA ALIEKUKOSEA
4.KULIA MACHOZI
5. VITENDO / KUMPIGA ALIEKUKOSEA / KUVUNJA VITU
1
2
3
4
5
Yote yanawezekana kutegemeana na situation.
 
anatwanga mtu ndoo

Eehh!! Bibie maana mie mdomoni sina maneno mengi nikikasirika! Siwezi kabisa kubwabwaja! Mie nataka nikae chini tuzungumze! Hata km nimekosea sio mtu kunikoromea au kunibwatiza! Ndio kuepusha haya huwa najiondokea tu! Laa sivyo napiga mtu ndoo nzito!! Bichwa la boyka🤣
 
Kama mnaandika kiswahili kwanini msiandike tu kiswahili moja kwa moja, ukizingatia mada imeletwa kwa kiswahili.
Au nyie kiswahili akipandi vyema?
Hili ni jukwaa huru hata ukiamua kuongea kichini kuna wachina wamo humu ndani wanajua kiswahili,
We hata ukiamua kuzungumza kizigua zungumza tu..
Kikubwa toa maoni yako ya hekima na busara...

Shing shang Juan cons
 
Inategemea na sehemu yenyewe, mimi siwezi kuongea wala kugombana na mtu kama nikikasirika kwenye maisha halisi huwa navuta pumzi ndefu alafu nitakaa kimya au naondoka eneo la tukio, alafu hasira zinakwisha,
ila ukinikasirisha kupitia simu au chochote kile ili mradi tusionane, nahakikisha naandika kila kilichopo moyoni mpaka viishe vyote kwa bahati mbaya huwa haviishi vinatoka tu,

usiombee niwe nimekamata pc, kwani nitaandika kitabu kizima ndani ya dk 15.
 
Namba 1 hii ikishindikana nahamia namba 3 kuondoka au kumtimua mtu machoni kwangu. Napenda kuwa na amani.
 
Pindi unapokosewa ni kipi kati ya hivi hutawala hasira zako

1.KUKAA KIMYA / KUMCHUNIA / KUTOMUONGELESHA ALIEKUKOSEA

2.KUSHOUT / KUGOMBA / KUTUKANA

3. KUONDOKA UKIKOSEWA / KUSEPA / KUMFUKUZA ALIEKUKOSEA

4.KULIA MACHOZI

5. VITENDO / KUMPIGA ALIEKUKOSEA / KUVUNJA VITU

6. KUNYWA BIA / SEX / KULA / KULALA
Huwa naenda Kilingeni Msata kufanya yangu

Jr
 
Pindi unapokosewa ni kipi kati ya hivi hutawala hasira zako

1.KUKAA KIMYA / KUMCHUNIA / KUTOMUONGELESHA ALIEKUKOSEA

2.KUSHOUT / KUGOMBA / KUTUKANA

3. KUONDOKA UKIKOSEWA / KUSEPA / KUMFUKUZA ALIEKUKOSEA

4.KULIA MACHOZI

5. VITENDO / KUMPIGA ALIEKUKOSEA / KUVUNJA VITU

6. KUNYWA BIA / SEX / KULA / KULALA
Mimi nimejifunza na ninajitahidi sana kuishi namba 1&3. Namba 1&3 ni bora sana, ninamshauri kila mmoja ajaribu ku-practice maishani. Ukiweza itakuepusha sana na mengi. Ila mtoa mada namba 3 mwishoni pale nadhani umechanganya- hii ya kumfukuza aliyekukosea ikae sehemu nyingine
 
basi km ndiyo hivyo mi utaniua kwa ndoo maana nikiona unajishusha ndiyo nazidi kuongea nitalalamika mpaka
Eehh!! Bibie maana mie mdomoni sina maneno mengi nikikasirika! Siwezi kabisa kubwabwaja! Mie nataka nikae chini tuzungumze! Hata km nimekosea sio mtu kunikoromea au kunibwatiza! Ndio kuepusha haya huwa najiondokea tu! Laa sivyo napiga mtu ndoo nzito!! Bichwa la boyka
 
Namba moja. Nikiwa na hasira huwa siwezi kabisa kuongea. Na vile nina historia ya kuwa na kigugumizi utotoni, ndo kabisa.
 
Mm namba 5., huwa simuachi mtu salama


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Nikiwa na hasira napiga au kuvunja vitu hovyo hovyo mfano ndoo,chupa n.k
 
Back
Top Bottom