Umuhimu wa Kumbi za Starehe kuaanza kukagua Vitambulisho vya wateja Nchini

Wild Flower

Member
Jul 20, 2023
80
96
Siku hizi idadi ya watoto wanaokwenda kumbi za starehe ni wengi mno. Na utawakuta wanakunywa pombe, kutumia madawa ya kulevya, kujiuza, kuvuta sigara, kufanya biashara haramu na mambo mengine yanayokiuka jamii.

Tatizo hili tunaweza tusione madhara yake sasa hivi lakini ndo tunavyokuza kizazi cha baadae.

Ni wakati sasa mamlaka husika kuchukua hatua za kudhibiti tatizo hili kwa kuanzisha utaratibu wa kuangalia vitambulisho vya wateja wanaohudhuria sehemu hizi kama nchi mbalimbali duniani zinavofanya. Na vitambulisho hivyo viwe na picha na umri ili kuthibitisha taarifa za kweli znazotolewa na mteja.

Hatua hii itasaidia kuhakikisha kuwa mazingira ya starehe yanabaki salama kwa wote wanaohudhuria na kuzuia uwepo wa watoto chini ya umri wa 18 ambao hawaruhusiwi kisheria kuingia katika maeneo hayo.
 
Umeongea jambo ambalo ni la msingi sana.

Kuna mahala nilikuepo jana, ni local swimming pool ipo Kibangu uko, kuna vitoto kama sio 16yrs basi less, vibakunywa beer na kuvuta fegi ni hatari.

Ata ishu ya kumtuma mtoto akakununulie sigara dukani au bia, wenzetu hiyo hawana. Maana sometimes haujui ni muda gani ametumwa au anatumia mwenyewe.
 
Siku hizi idadi ya watoto wanaokwenda kumbi za starehe ni wengi mno. Na utawakuta wanakunywa pombe, kutumia madawa ya kulevya, kujiuza, kuvuta sigara, kufanya biashara haramu na mambo mengine yanayokiuka jamii.

Tatizo hili tunaweza tusione madhara yake sasa hivi lakini ndo tunavyokuza kizazi cha baadae.

Ni wakati sasa mamlaka husika kuchukua hatua za kudhibiti tatizo hili kwa kuanzisha utaratibu wa kuangalia vitambulisho vya wateja wanaohudhuria sehemu hizi kama nchi mbalimbali duniani zinavofanya. Na vitambulisho hivyo viwe na picha na umri ili kuthibitisha taarifa za kweli znazotolewa na mteja.

Hatua hii itasaidia kuhakikisha kuwa mazingira ya starehe yanabaki salama kwa wote wanaohudhuria na kuzuia uwepo wa watoto chini ya umri wa 18 ambao hawaruhusiwi kisheria kuingia katika maeneo hayo.
Mtoto wa mwenzio ni mkubwa mwenzako
 
Umeongea jambo ambalo ni la msingi sana.

Kuna mahala nilikuepo jana, ni local swimming pool ipo Kibangu uko, kuna vitoto kama sio 16yrs basi less, vibakunywa beer na kuvuta fegi ni hatari.

Ata ishu ya kumtuma mtoto akakununulie sigara dukani au bia, wenzetu hiyo hawana. Maana sometimes haujui ni muda gani ametumwa au anatumia mwenyewe.
Hili jambo linatakiwa ifikapo 2025 litiwe mkazo zaidi maana kipindi hiko watanzania wengi watakua na NIDA kama sio ID basi atakua na Namba
 
Hamna mtoto sehemu ya starehe sikuhizi akkitokea mmoja. Haoo wote over 18. Nao watakua kama ww katika age uliyonayo maana wte mmekutana sehemu yenu pendwa...only if you are there for research.
 
Back
Top Bottom