Umri gani ni sahihi kumtahiri mtoto wa kiume?

Habari.
Nina jambo linanitatiza kidogo la ki-utabibu. Kipindi cha likizo ya mwisho wa mwaka (December 2010), nilipanga kumtahiri mwanangu. Lakini tatizo lilikuja kutoka kwa wazazi na baadhi ya ndugu wa karibu wakati naulizia ni hospitali gani nitapata huduma hiyo. Kila mmoja alikuwa anasisitiza kuwa hakikuwa kipindi kizuri kumtahiri sababu ni kipindi cha joto, hivyo nisubiri mpaka wakati wa baridi.

Ikabidi tu niwe mpole ingawa nikifikiria kipindi cha baridi ni huko mwezi April on wards naona kama kijana nae anazidi kukua na utundu unaongezeka. Nikaona kupitia safu hii niulizie uhalisia na uhusiano wa joto na huko kutahiri mtoto cuz I understand nchi zenye joto pia huwa wanatahiri watoto wao. kama kuna mtu mwenye utaalamu wa sekta hii tafadhali anaomba mawazo au ushauri wa kitaalam.
 
Mi si mtaalamu sana ila kwa uzoefu mdogo nilionao watoto wadogo wa kiume wa ndugu zangu wote huwa wanatahiriwa kipindi cha baridi. Wazee wanasema kuwa kipindi cha joto ni kizuri maana kidonda kinapona haraka du. Wataalam watakuambia zaidi.
 
Sisi wengine huwa atuangalii misimu ya hali ya hewa, mtoto akishafikisha siku saba tangia kuzaliwa tu basi anaingizwa sunna (anatahiriwa). Huwa atusubiri mpaka afikie umri wa kwenda shule, kwa sababu umri huo mtoto ashaanza kukomaa na kuwa mtundu...! na huwezekano wa kujitonesha tonesha ni mkubwa sana.

Kama mtoto wako keshaanza shule basi mpeleke hospitali kutahiriwa kipindi chocote cha likizo, haswa zile likizo ndefu. Kwa ufupi kupona kwa kidonda hakutegemei hali ya hewa, watoto wote miili yao ina uwezo wa kujiponyesha kwa haraka sana kuliko watu wazima.
 
hata mie nilivyokuwa natoga sikio nilishauriwa kipindi cha baridi ndio kizuri coz yanapona haraka tho naona haimaanishi kipindi cha joto ndio kidonda hakiponi
 
Hapana bado hajafikia umri wa shule, ana miezi mitano!

Mkuu mwaka jana nilikua na shughuli kama hiyo ya kutahiri, lakini kabla niliona nililete mbele ya wadau wanishauri, na baada ya maoni nilipata njia sahihi na nzuri nakushauri tumia hiyo.
Njia nzuri ambayo haijalisha joto wala baridi ni kumtahiri kwa njia ya plastiki, tena kwa umri huo ndio mahala pake ni siku 5 kwisha maneno.
Njia hii nikwamba anavalishwa kiplastiki ndani kwa juu ktk kichwa na juu ya ganda panafungwa na kitu kama waya hivi, kisha inaachwa baada ya kuanzia siku 4 hadi 7 utakuta kiplastiki na ganda vimeanguka vyenyewe.
Na njia hii haina maumivu na kidonda chake ni chadakika kadhaa na mara nyingi haina maambukizi, pia kuanzia siku ya kwanza mtoto anaoga kama kawa na kaptula anavaa tu.
Sikushauri utumie njia ya kukata na kushona utamtesa sana mwanao kwa maumivu makubwa.
kwa ushauri zaidi cheki na thread hii
https://www.jamiiforums.com/jf-doctor/65133-umri-gani-ni-sahihi-kumtahiri-mtoto-wa-kiume.html
 
Thanks a lot kwa somo mkuu paulss

Nimeelimika vya kutosha, na mwanangu ana siku 49 mpaka leo.

Inabidi nimtahiri wiki hii hii.

Japo uzi ni wa muda kidogo lakini umenisaidia kujua mambo mengine.
 
Last edited by a moderator:
Mtoto kupata UTI ni kutokuwa makini kumbadilisha anapojisaidia. wanangu siwatahiri chini ya miaka miwili na hawajawahi kuugua UTI. Na kama mtu hauko makini utashangaa mtoto katahiriwa na bado anasumbuliwa na UTI.

Baada ya mimi kukosa jibu la kitaalamu kuhusu lini mtoto anapaswa kutahiriwa niliamua kuamini tu ushauri wa kitaani kuwa kutahiri mtoto mchanga kunamfanya awe na kibamia.

Mwanangu nimemtahiri na miaka miwili na alipona in a week. Tena nilinfanyia pale Regency wana wataalamu wazuri kuanzia wa nusu kaputi, doctor wa watoto na bingwa wa operation; hivyo hakuna mistake anakuwa amezungukwa na wataalamu.

Tena hakuwahi kuvaa kanga kama wengi niwaonavyo...yani doctor kanambia mvalishe kaptula kama kawaida...na hakulia hata kidogo zaidi ya kulia sindano ya nusu kaputi...katoka hapo kaendelea na mishe mishe zake za michezo. Baada ya wiki tukatoa nyuzi.
 
mie hili swala bado linanchanganya kwa kweli, nina jiran yangu hapa milango inaangaliana, ana mwanae saa hz anakaribia miaka miwili, huyu mtoto alitahiriwa kwa njia hyo cjui ya plastic akiwa na miez mitatu, sasa bac yaan huyu mtoto jaman ni ana alama ya pe...., tena kakisimamandio kanachomoza kidogo, akiwa kawaida yaan ni hamna kitu ana mwili mzur, kila ki2 kinakua vzur icpokuwa pale pako hvo hvo sasa cjui ni huko kutahr au ndivyo alivyozaliwa,,,,
ningeweka hapa pic ya kidushe chake ila sio poa

so jaman kuwen makin aiseee
 
Mtoto kupata UTI ni kutokuwa makini kumbadilisha anapojisaidia. wanangu siwatahiri chini ya miaka miwili na hawajawahi kuugua UTI. Na kama mtu hauko makini utashangaa mtoto katahiriwa na bado anasumbuliwa na UTI.

Baada ya mimi kukosa jibu la kitaalamu kuhusu lini mtoto anapaswa kutahiriwa niliamua kuamini tu ushauri wa kitaani kuwa kutahiri mtoto mchanga kunamfanya awe na kibamia.

Mwanangu nimemtahiri na miaka miwili na alipona in a week. Tena nilinfanyia pale Regency wana wataalamu wazuri kuanzia wa nusu kaputi, doctor wa watoto na bingwa wa operation; hivyo hakuna mistake anakuwa amezungukwa na wataalamu.

Tena hakuwahi kuvaa kanga kama wengi niwaonavyo...yani doctor kanambia mvalishe kaptula kama kawaida...na hakulia hata kidogo zaidi ya kulia sindano ya nusu kaputi...katoka hapo kaendelea na mishe mishe zake za michezo. Baada ya wiki tukatoa nyuzi.

Mkuu Regency wanacharge sh. ngapi kwa operation hiyo?
 
Dah...... Uzi umerudi tena
Anyway napenda kuthibitisha kuwa baada ya kupata maoni anuai ya wataalamu hapa JF na kwa DRs njia sahihi na salama zaidi ya kumtahiri mtoto katika dunia yetu ya leo ni ya plastick
Kama atafungwa vizuri njia hii inatoa maumivu na kuuguza kidonda kwa sailimia 99
Haihitaji uangalizi mkubwa kama ya kukata na kushona kunakopelekea kidonda kuuguzwa na kusafishwa mara kwa mara kunako msababishia mtahiriwa mateso makubwa
ya maumivu.

Kuhusu umri hili swala ni mtambuka, nionavyo mimi umri mzuri ni akiwa mdogo inapendeza zaidi na salama zaidi kwa kupona haraka
Dhana ya kibamia ni maneno ya mitaani tu na haishauriwi kutahiriwa ukiwa umebalehe maana utaathiri baadhi ya mishipa ambayo imekomaa na kusababisha kupunguza ufanisi wa shughuli
Pia kutahiri ukiwa umebalehe ni tatizo kwa uponaji wa kidonda maana kila mara uume ukisimama utasababisha kutanuka na kusumbua jeraha hasa wakati wa asubuhi au pindi usikiapo muwasho wa kidonda husababisha uume kusimama mara kwa kwa mara.

Tujitahidi kuwatahiri watoto mapema ndani ya mwaka mmoja na tutumie njia ya kufunga plastick ambayo ni salama zaidi
, inga pia kama hutajali kumpunguzia mateso ya kuuguza kidonda na kuvaa kanga mwanao waweza tumia njia ya kukata
 
Wakwangu alitahiriwa baada ya siku 8 tu tangu azaliwe, na hakupata na wala sijaona madhara yoyote hadi leo
 
Re: Umri gani ni sahihi kumtahiri mtoto wa kiume?

By
quote_icon.png
chrispin
mhashamu baba/mama askofu, ni umri gani sahihi wa kumtahiri mtoto wa kike?

WW WATU WANAONGEA MAMBO YA KUELIMISHA, NA WEWE UNAKUJA NA ZA KUBOMOA,TOHARA KWA WANAWAKE NI DHAMBI HATA KWA MUNGU



 
Paulss, wale mapacha wako ni kiume au wakike?

Dah...... Uzi umerudi tena
Anyway napenda kuthibitisha kuwa baada ya kupata maoni anuai ya wataalamu hapa JF na kwa DRs njia sahihi na salama zaidi ya kumtahiri mtoto katika dunia yetu ya leo ni ya plastick
Kama atafungwa vizuri njia hii inatoa maumivu na kuuguza kidonda kwa sailimia 99
Haihitaji uangalizi mkubwa kama ya kukata na kushona kunakopelekea kidonda kuuguzwa na kusafishwa mara kwa mara kunako msababishia mtahiriwa mateso makubwa
ya maumivu.

Kuhusu umri hili swala ni mtambuka, nionavyo mimi umri mzuri ni akiwa mdogo inapendeza zaidi na salama zaidi kwa kupona haraka
Dhana ya kibamia ni maneno ya mitaani tu na haishauriwi kutahiriwa ukiwa umebalehe maana utaathiri baadhi ya mishipa ambayo imekomaa na kusababisha kupunguza ufanisi wa shughuli
Pia kutahiri ukiwa umebalehe ni tatizo kwa uponaji wa kidonda maana kila mara uume ukisimama utasababisha kutanuka na kusumbua jeraha hasa wakati wa asubuhi au pindi usikiapo muwasho wa kidonda husababisha uume kusimama mara kwa kwa mara.

Tujitahidi kuwatahiri watoto mapema ndani ya mwaka mmoja na tutumie njia ya kufunga plastick ambayo ni salama zaidi
, inga pia kama hutajali kumpunguzia mateso ya kuuguza kidonda na kuvaa kanga mwanao waweza tumia njia ya kukata
 
Wana JF lets share experience, biologicaly uume ni kama ndizi (banana) yaani ina layers tatu na kimsingi kutahiri ni kuondoa layer ya juu sehem ya mbele, kwa mantiki hii basi kama ambavyo ndizi ikiwa changa si rahisi kutenganisha ganda na ndizi yenyewe(ile sehemu tunayokula) ndo maana mtu akimenya ndizi ambayo haijakomaa anajikuta anatoa na sehemu ya ndizi yenyewe kwenye ganda, tukiwianisha mfano huu utaona kwamba kumtahiri mtoto mchanga sana (0-10) days ni delicate kwa kua ni rahisi sana kukata tissues laini ambazo kwa sababu ya udogo wa kiungo hicho si rahisi kutenganisha nyama na ngozi, endapo mtoto akikua kiasi cha miaka 2 ukiangalia uume wake utaona kisehemu cha mbele automatikali kinaonyesha mbinuko na ile round tunayo tahiri inaonekana wazi kwa wakati huu maana yake ni kama ndizi iliyo anza kuiva ambayo kuimenya bila kuathiri nyama ni rahisi, kwa ushauri wangu huu ndio muda muafaka kwa kua inapunguza chances za kumjeruhi mtoto, zamani watu walikua wanachelewa kutahiri ndo maana pamoja na madhara ya magonjwa lakini uume ulikua unakua vizuri (full length) kwa kua misuli ilikua ina grow freely, utaratibu wa sasa wa kutahiri vichanga ndo umepelekea kuathiri ukuaji wa nanihii zetu matokeo yake ndo haya tunalazimika kutumia stimulant ila ku paform vizuri na kuongeza ukubwa maana misuli ikiumizwa haikui vizuri ndo kidude kinakua kidooogo. suala la utiai (UTI) ni usafi tu wala siyo ishu maana hata mtu mzima usipofanya usafi wa kutosha utapata UTI, kwa kuongezea mi naona njia ya kiplastic (ring) ni nzuri sana maana hawashoni hivyo kidide cha mtotot hakitobolewi ili kushikiza uzi kwa maana kwamba unaendelea kupunguza chances za kuiumiza dudu, halafu inapona fasta na inakua rahisi kihudumia kidonda, thats my contribution.
 
umri mzuri zaidi ni pale anapokuwa bado mdogo, kwasababu akishakua mtu mzima huwa wanapata tabu sana kupona kidonda. Angalau kabla hajafikisha miaka saba awe tayari kafanyiwa tohara

mtoto wa ndg yangu alitahiriwa akiwa na cku 3 kutokana na mtoto kuwa na maumbile madogo sana yalitokea makosa ktk shughuli hiyo matokeo yake mtoto alianza kutokwa na mikojo mpaka juzi akiwa darasa la nne imebidi afanyiwe operation ndogo ndo imemsaidia kwa ujumla si vizuri kutahili mtoto akiwa mchanga sana umri mzuri ni angalau miaka miwili
 
Back
Top Bottom