masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 18,625
- 14,591
Nilipokuwa kijana wa CCM tuliwahi kuwa na kile kitu kinaitwa kiburi ya chama, kunywa maji ya bendera, na kutetea kwa hali yoyote nchi na chama.
Hizo ndo siku chama kilikuwa chama.
Tuliandamana miaka hiyo kutetea ukombozi kusini mwa Afrika na walioshirikiana na makaburu tuliwapasha kisawasawa.
Nakumbuka Ufaransa ikishirikiana na makaburu, waziri wao wa mambo ya nje alikuja Tanzania kutoa misaada.
Vijana tulimwambia "Go home". Yule waziri akatoa shinikizo Serikali imwombe radhi. Serikali ikakataa, Jamaa akaondoka. Hiyo ndo ilikuwa jeuri ya vijana wa chama.
Kwa leo Nape naweza kumuinguza kuwa ni kati ya vijana wachache wenye uthubutu wa si tu kuelewa, bali kutetea chama na itikadi yake.
Sasa leo tunaona vijana toka vyama mbali mbali wakitimkia CCM.
HATUJUI misimamo yao, hatujui itikadi zao.
Tunawapokea na kuwapa vyeo, na kuwaacha walio sota na chama.
Watu wanaohamia CCM zaidi sana ni wachumia tumbo, na tunawaenzi sasa.
Naunga mkono msimamo kama ule wa Nape.
Hakika tutavuna tunachopanda. Hatuwezi kupanda michongoma, halafu tuvune maembe.
Kidumu Chama Cha Mapinduzi.
Hizo ndo siku chama kilikuwa chama.
Tuliandamana miaka hiyo kutetea ukombozi kusini mwa Afrika na walioshirikiana na makaburu tuliwapasha kisawasawa.
Nakumbuka Ufaransa ikishirikiana na makaburu, waziri wao wa mambo ya nje alikuja Tanzania kutoa misaada.
Vijana tulimwambia "Go home". Yule waziri akatoa shinikizo Serikali imwombe radhi. Serikali ikakataa, Jamaa akaondoka. Hiyo ndo ilikuwa jeuri ya vijana wa chama.
Kwa leo Nape naweza kumuinguza kuwa ni kati ya vijana wachache wenye uthubutu wa si tu kuelewa, bali kutetea chama na itikadi yake.
Sasa leo tunaona vijana toka vyama mbali mbali wakitimkia CCM.
HATUJUI misimamo yao, hatujui itikadi zao.
Tunawapokea na kuwapa vyeo, na kuwaacha walio sota na chama.
Watu wanaohamia CCM zaidi sana ni wachumia tumbo, na tunawaenzi sasa.
Naunga mkono msimamo kama ule wa Nape.
Hakika tutavuna tunachopanda. Hatuwezi kupanda michongoma, halafu tuvune maembe.
Kidumu Chama Cha Mapinduzi.