Sikirimimimasikini
JF-Expert Member
- Dec 27, 2019
- 2,921
- 15,612
Baada ya Russia kuivamia kijeshi Ukraine, Russia imewekewa vikwazo kadhaa na nchi mbali mbali zikiwemo US, UK na nchi kadhaa zinazounda Umoja wa Ulaya (EU). Ktk vikwazo vya hivi karibuni zaidi ni vikwazo vilivyotangazwa na US dhidi ya nchi hiyo kununua mafuta ya Russia na ikaahidi kutangaza vikwazo vingine dhidi ya nishati nyinginezo za Russia ikiwemo gesi huko mbeleni.
Kwa upande wa Umoja wa Ulaya, fikra ya kuweka vikwazo dhidi ya mafuta na gesi ya Russia imezua mtafaruku mkubwa kutokana na utegemezi mkubwa wa nchi za EU kwa bidhaa hizo za Russia kiasi kwamba vikwazo hivyo wakivipitisha vitawaathiri vibaya wao wenyewe. Ktk mjadala wa kuweka vikwazo hivyo, Umoja wa Ulaya umegawanyika ktk mafungu matatu yafuatayo:
1) Wanaosapoti vikwazo hivyo: Poland, France, Spain
Poland ndiye kinara anayetaka kila aina ya vikwazo viwekwe dhidi ya Russia hata kama vikwazo hivyo vitaathiri uchumi wa nchi za Ulaya. Pamoja na kuwa nchi hiyo inawezaathirika na maamuzi ya vikwazo hivyo, Poland yaamini kuwa imejiandaa vizuri kutokana na ongezeko lake la kununua gesi asilia toka US, pamoja na ujenzi wa bomba la kuingiza gesi ya Norway kwenye nchi hiyo (Poland).
2) Wapingaji wa vikwazo hivyo: Ujerumani, Hungary, Bulgaria na Finland
Ujerumani, mtumiaji mkubwavwa mafuta ya Russia kwa Ulaya, anapinga vikali tena moja kwa moja vikwazo vyovyote vitavyowekwa dhidi ya nishati za Russia. Vice-chancellor Robert Habeck alionya kuwa vikwazo hivyo vitahatarisha utulivu wa raia wa Ujerumani na kuhatarisha upungufu mkubwa wa nishati ktk sekta kadhaa nchini.
Bulgaria, Waziri Mkuu Kiril Petkov amesema serikali yake inasapoti vikwazo vyote dhidi ya Russia lakini vikwazo hivyo visiwe tu ktk mafuta na gesi za Russia. Waziri huyo akaongezea kuwa "Hatuna mbadala wa nishati hizo kwa sasa, tunategemea zaidi (mafuta na gesi za Russia)"
Nchi hizo zimeamua kukalia kimya mjadala huo, na pia zategemea nishati toka Russia. Mfano:
Kwa upande wa Umoja wa Ulaya, fikra ya kuweka vikwazo dhidi ya mafuta na gesi ya Russia imezua mtafaruku mkubwa kutokana na utegemezi mkubwa wa nchi za EU kwa bidhaa hizo za Russia kiasi kwamba vikwazo hivyo wakivipitisha vitawaathiri vibaya wao wenyewe. Ktk mjadala wa kuweka vikwazo hivyo, Umoja wa Ulaya umegawanyika ktk mafungu matatu yafuatayo:
1) Wanaosapoti vikwazo hivyo: Poland, France, Spain
Poland ndiye kinara anayetaka kila aina ya vikwazo viwekwe dhidi ya Russia hata kama vikwazo hivyo vitaathiri uchumi wa nchi za Ulaya. Pamoja na kuwa nchi hiyo inawezaathirika na maamuzi ya vikwazo hivyo, Poland yaamini kuwa imejiandaa vizuri kutokana na ongezeko lake la kununua gesi asilia toka US, pamoja na ujenzi wa bomba la kuingiza gesi ya Norway kwenye nchi hiyo (Poland).
- Mwaka jana, 2021, Poland ilinunua tani milioni 8.3 za makaa ya mawe toka Russia, yenye thamani ya zaidi ya Euro milioni 625most of
- Mwaka 2019, 61.5% ya mafuta yote nchini Poland yalinunuliwa toka Russia.
- 55% ya gasi itumikayo Poland hununuliwa toka Russia.
- 17% ya gesi yote itumikayo Ufaransa hununuliwa toka Russia
- 7% ya mafuta yatumikayo Ufaransa hununuliwa toka Russia.
- 30.2% ya makaa ya mawe yatumikayo Ufaransa hununuliwa toka Russia.
2) Wapingaji wa vikwazo hivyo: Ujerumani, Hungary, Bulgaria na Finland
Ujerumani, mtumiaji mkubwavwa mafuta ya Russia kwa Ulaya, anapinga vikali tena moja kwa moja vikwazo vyovyote vitavyowekwa dhidi ya nishati za Russia. Vice-chancellor Robert Habeck alionya kuwa vikwazo hivyo vitahatarisha utulivu wa raia wa Ujerumani na kuhatarisha upungufu mkubwa wa nishati ktk sekta kadhaa nchini.
- Mwaka 2021 Germany ilinunua 55% ya gesi yake toka Russia, ambayo ni takribani mita za ujazo bilioni 140.
- 35% ya mafuta ghafi yake na 50% ya makaa yake ya mawe hutegemea toka Russia.
Bulgaria, Waziri Mkuu Kiril Petkov amesema serikali yake inasapoti vikwazo vyote dhidi ya Russia lakini vikwazo hivyo visiwe tu ktk mafuta na gesi za Russia. Waziri huyo akaongezea kuwa "Hatuna mbadala wa nishati hizo kwa sasa, tunategemea zaidi (mafuta na gesi za Russia)"
- 70% ya gesi nchini Bulgaria hutoka Russia
- 60% ya mafuta yatumikayo Bulgaria hutoka Russia
- Bulgaria inaitegemea Russia kwa 100% ktk nishati ya nyuklia (nuclear fuel)
- 50% ya makaa ya mawe yatumikayo Finland hutoka Russia
- Zaidi ya 60% ya gesi itumikayo Finland hutoka Russi
- Zaidi ya 60% ya mafuta yatumikayo Finland hutoka Russia
Nchi hizo zimeamua kukalia kimya mjadala huo, na pia zategemea nishati toka Russia. Mfano:
- 90% ya gesi asilia itumikayo Czechia hutoka Russia
- 50% ya mafuta nchini Czechia hutoka Russia
NETWORK ROUNDUP: EU split on Russian oil and gas ban
Germany and Hungary are the most vocal opponents of an EU import ban on Russian energy, which is staunchly supported by Poland, while France and others sit on the fence.
www.euractiv.com