King Jody
JF-Expert Member
- Oct 8, 2022
- 914
- 1,704
Habari zenu waungwana,
Katika ulimwengu wa sasa ni nadra sana kupata rafiki wa kweli ambaye unaweza kumuamini,
Nakumbuka miaka kadhaa nyuma niliwahi kuwa na rafiki, huyu alikuwa ni zaidi ya ndugu, tulielewana sana.
Tulishirikiana kwa kila jambo, Popote alipo nami nilikuwepo, jamaa alikuwa mpambanaji sana,
hakuchagua kazi ya kufanya ili mradi apate pesa,
Katika harakati za upambanaji, mimi nilibahatika kupata kazi kwenye kampuni moja ya utalii iliyopo mjini Arusha, yeye alienda mererani kwenye machimbo ya Tanzanite. Tuliendelea kuwasiliana huku tukiwa na mipango mingi,
Kuna siku mvua ilinyesha kubwa mno, maji yakajaa kwenye mashimo huko Mererani, watu wengi walipoteza maisha akiwepo rafiki yangu, ilikuwa siku ya huzuni sana kwangu, nikiri sijawahi kuwa na rafiki wa kweli kama huyu.😢😢
Mwenyezi Mungu ailaze pema roho ya marehemu Amen🙏🙏,
Kazi ya MUNGU haina makosa. R.I.P Rafiki wa kweli.
Je wewe umewahi kubahatika kuwa na rafiki wa kweli?
Katika ulimwengu wa sasa ni nadra sana kupata rafiki wa kweli ambaye unaweza kumuamini,
Nakumbuka miaka kadhaa nyuma niliwahi kuwa na rafiki, huyu alikuwa ni zaidi ya ndugu, tulielewana sana.
Tulishirikiana kwa kila jambo, Popote alipo nami nilikuwepo, jamaa alikuwa mpambanaji sana,
hakuchagua kazi ya kufanya ili mradi apate pesa,
Katika harakati za upambanaji, mimi nilibahatika kupata kazi kwenye kampuni moja ya utalii iliyopo mjini Arusha, yeye alienda mererani kwenye machimbo ya Tanzanite. Tuliendelea kuwasiliana huku tukiwa na mipango mingi,
Kuna siku mvua ilinyesha kubwa mno, maji yakajaa kwenye mashimo huko Mererani, watu wengi walipoteza maisha akiwepo rafiki yangu, ilikuwa siku ya huzuni sana kwangu, nikiri sijawahi kuwa na rafiki wa kweli kama huyu.😢😢
Mwenyezi Mungu ailaze pema roho ya marehemu Amen🙏🙏,
Kazi ya MUNGU haina makosa. R.I.P Rafiki wa kweli.
Je wewe umewahi kubahatika kuwa na rafiki wa kweli?