Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,599
Nimepewa hadithi hii na jamaa yangu anayefanya kazi ya kuwahudumia watoto yatima na wale wanaoishi katika mazingira hatarishi (orphaned and vulnerable children, OVC) katika mji mmoja hapa Tz. Watu wengi wanaowahudumia ni wahanga wa VVU/UKIMWI (victims of HIV/AIDS). Siku moja walimtembelea bibi mmoja mzee mwenye umri wa karibia miaka 70. Anaishi na binti yake mmoja mwenye VVU/UKIMWI na wajukuu karibia 10. Watoto wake wengine 5 walishakufa kutokana na VVU/UKIMWI. Huyo mgonjwa alikuwa anaumwa sana na anatoa harufu kali. Waliamua kumpeleka zahanati ambapo iligundulika kuwa sehemu zake nyeti zimeoza. Alipewa huduma kwa gharama za shirikia (la huyo jamaa yangu) na kuanzishiwa dawa za kurefusha maisha. Kwa sasa hali yake ni nzuri kiasi.
Tatizo jingine ni kuwa hii familia haikuwa na nyumba. Nyumba yao ya mbavu za mbwa ilianguka na walikuwa wanalala nchini ya mti karibu na ilipokuwa nyumba yao. Hawakuwa na uhakika wa chakula, walitegemea wajukuu wawili wa huyo bibi (ambao walikuwa darasa la 7) wafanye vibarua na kupata pesa ya unga na dagaa. Maisha yalikuwa magumu kweli kweli.
Shirikia liliamua kuwajengea nyumba ndogo ya bati na kuta za udongo. Pia walianza kuwapatia chakula kila wiki. Na yule bibi alipewa godoro. Wakati anakabidhiwa vitu hivyo, bibi alilia sana. Akawambiwa wanfayakazi wa lile shirika kuwa, ameishi umri wake wote, hakuwahi kula chakula kizuri na mbali ya hayo hakujua kuwa siku moja anaweza kulalia godoro. Yule rafiki yangu naye alitokwa na machozi na kupata hisia za ajabu. Anasema kuwa kwa muda mfupi tu alijihisi kama alimwona Mungu amezungukwa na malaika.
Tatizo jingine ni kuwa hii familia haikuwa na nyumba. Nyumba yao ya mbavu za mbwa ilianguka na walikuwa wanalala nchini ya mti karibu na ilipokuwa nyumba yao. Hawakuwa na uhakika wa chakula, walitegemea wajukuu wawili wa huyo bibi (ambao walikuwa darasa la 7) wafanye vibarua na kupata pesa ya unga na dagaa. Maisha yalikuwa magumu kweli kweli.
Shirikia liliamua kuwajengea nyumba ndogo ya bati na kuta za udongo. Pia walianza kuwapatia chakula kila wiki. Na yule bibi alipewa godoro. Wakati anakabidhiwa vitu hivyo, bibi alilia sana. Akawambiwa wanfayakazi wa lile shirika kuwa, ameishi umri wake wote, hakuwahi kula chakula kizuri na mbali ya hayo hakujua kuwa siku moja anaweza kulalia godoro. Yule rafiki yangu naye alitokwa na machozi na kupata hisia za ajabu. Anasema kuwa kwa muda mfupi tu alijihisi kama alimwona Mungu amezungukwa na malaika.