Umewahi Kuchunguza kwanini Nyoka hamdhuru Mtoto!?

Umewahi Kuchunguza kwanini Nyoka hamdhuru Mtoto!?

[Inasemekana adrenaline hormone inayozalishwa pale mtu anaposhtuka kwa kumuona nyoka ndio inasababisha ang'atwe kwani nyoka anahisi hatari inayomkabili na anajihami mapema. Na ndio maana inasemekana kama hujamuona nyoka na yeye kakuona hawezi kukudhuru, kwa kuwa hakuna adrenaline inayozalishwa. Wataalamu wanasema nyoka inahisi adrenaline inayozalishwa katika mwili wa binadamu.
Kwa watoto nadhani hiyo ishu ya adrenaline hormone ina-apply, kwa sababu hawajui hatari ya nyoka.]

mkuu katati nakubaliana na wewe, mie niliyekulia kijijini nimeshaona hii, nilienda kujisaidia porini, nilipomaliza kukata gogo nachukua majani nicha... natizama chini pale niliposhusha gogo namuona kifutu katulia, kwa kweli nilitoka mbio kama jogoo anavyokuza mtetea, sikuamini nilivyopona, manake ningekuwa sipo na jamii forum wala nisingeijua
 
[Inasemekana adrenaline hormone inayozalishwa pale mtu anaposhtuka kwa kumuona nyoka ndio inasababisha ang'atwe kwani nyoka anahisi hatari inayomkabili na anajihami mapema. Na ndio maana inasemekana kama hujamuona nyoka na yeye kakuona hawezi kukudhuru, kwa kuwa hakuna adrenaline inayozalishwa. Wataalamu wanasema nyoka inahisi adrenaline inayozalishwa katika mwili wa binadamu.
Kwa watoto nadhani hiyo ishu ya adrenaline hormone ina-apply, kwa sababu hawajui hatari ya nyoka.]

mkuu katati nakubaliana na wewe, mie niliyekulia kijijini nimeshaona hii, nilienda kujisaidia porini, nilipomaliza kukata gogo nachukua majani nicha... natizama chini pale niliposhusha gogo namuona kifutu katulia, kwa kweli nilitoka mbio kama jogoo anavyofukuza mtetea, sikuamini nilivyopona, manake ningekuwa sipo na jamii forum wala nisingeijua
 
[ Sio nyoka tu,wanyama wengi hawawadhuru watoto,ni Mungu tu anawalinda kama anavyowalinda na magonjwa mbalimbali hata wale uchafu kiasi gani]

mwachie fisi uone, sikubaliani na hii kauli
 
mtoto mdogo hana dhambi ndo maana snake hujifeel guilty sana akimdhuru,lakini sisi wakubwa ni mazinzi,malevi,maongo,machoyo,machawi,majizi ndo maana snake akitudhuru ni lawfull hata kwa sir God!
 
Nje ya mada kidogo, Naomba kujuzwa nimewahi kusikia mara nyingi watu wakisimulia Mbwa akikutana na Chatu hana ujanja anamfuata mwenyewe hadi anakamatwa nakuliwa.Je ni sababu zipi za kisanyansi au kienyeji zinazopelekea Mbwa kuwa -----/Mjinga mbele ya Chatu.
 
Kwa kweli there're somethings which are exeptional, mimi nimemshuhudia mtu mzima kabisa mwenye wajukuu hadhuriwi na nyoka wa aina yoyote ile, Yule mzee alikuwa pacha na inasemekana tangu utotoni walikuwa na hiyo hali na nyoka, Yeye nyoka akimuona anakuwa mpole kama nini anashindwa hata ku move, Kuna incident moja tulienda kuvuna mahindi shambani kwake, wakati wa kula kule shambani mzee alivua saa yake akaiweka juu ya kisiki akaisahau akakumbuka tumefika nyumbani, akawasha pikipiki tukairudia tukakuta bonge la nyoka aina ya kifutu ameizunguka ile saa, mzee akamchukua nyoka akamning'iniza shingoni akawasha pikipiki baada ya umbali flani akamtua na kumwacha aende zake, Kwa wale waliokuwa wanamfahamu amefanya kazi kama afisa elimu takwimu Mbozi baadae.Mbarali in late 1990s now ni Marehemu. Hii makitu ipo ingawa nimekuwa impressed na maelezo ya kibailojia about Adrenaline hormone.
 
[Inasemekana adrenaline hormone inayozalishwa pale mtu anaposhtuka kwa kumuona nyoka ndio inasababisha angle'atwe kwani nyoka anahisi hatari inayomkabili na anajihami mapema. Na ndio maana inasemekana kama hujamuona nyoka na yeye kakuona hawezi kukudhuru, kwa kuwa hakuna adrenaline inayozalishwa. Wataalamu wanasema nyoka inahisi adrenaline inayozalishwa katika mwili wa binadamu.
Kwa watoto nadhani hiyo ishu ya adrenaline hormone ina-apply, kwa sababu hawajui hatari ya nyoka.]

mkuu katati nakubaliana na wewe, mie niliyekulia kijijini nimeshaona hii, nilienda kujisaidia porini, nilipomaliza kukata gogo nachukua majani nicha... natizama chini pale niliposhusha gogo namuona kifutu katulia, kwa kweli nilitoka mbio kama jogoo anavyofukuza mtetea, sikuamini nilivyopona, manake ningekuwa sipo na jamii forum wala nisingeijua

Daaah...haahaa haaaaaaàaaaaaaaaa...kinyeo kilikoswakoswa
 
Wakuu hivi ndo unamkuta dogo anacheza na nyoka.Utatumia mbinu gani kumuokoa?Au utampotezea?Lets be honest
 
Nimeona kule Tanga mtu akimwona nyoka anapita, basi yeye anajishika kwenye wrist na nyoka anabakia palepale haendi mbele wala nyuma hadi anauawa, nilipouliza wanatumia dawa gani wakasema hamna dawa nikashindwa kuelewa nguvu gani ipo baina ya binadam na nyoka, nadhani hata JF kuna watu walishapata kuona hiyo kitu
 
Mtoto ni malaika.
Siri ni moja, japo siwezi kukumbuka aya za mnaandika matakatifu....."waacheni watoto wadogo waje kwangu, maana ufalme wa mbingu ni wao...."

Pia mtakumbuka baada ya nyoka kumlaghai mama yetu wa kwanza Eva/Hawa, MUNGU alikasirika na kumwambia nyoka......"umelaaniwa wewe. Nitaweka uadui Kati yako na uzao wa mwanamke huyu. Yeye atakuponda kichwa, nawe utamgonga kisigino......."
 
smartapartments Sio nyoka tu,wanyama wengi hawawadhuru watoto,ni Mungu tu anawalinda kama anavyowalinda na magonjwa mbalimbali hata wale uchafu kiasi gani

kweli mkuu nilishuhudia tembo akiua watu wawili na kumpapasa mtoto mdogo kwa mkonga wake kisha kupita pembeni na kuondoka zake huku mtoto akimkimbilia na tembo akimgeukia kwa huruma
 
Binafsi nadhani, nyoka nae ana uelewa endapo anakua katika mazingira hatarishi (yaani akutanapo na mtu mzima anajua hatari inamnyemelea, purukushani za mtu huyo ni dalili tosha kua anaweza dhurika) ila anapokutana na mtoto, kunakua hakuna dalili yoyoye ya mazingira hatarishi kwake na ndio maana anajiachia ila anaposhtuliwa, anapata dalili za mazingira hatarishi ndio maana anaweza kumdhuru mtoto endapo atashtuliwa..
 
kweli mkuu nilishuhudia tembo akiua watu wawili na kumpapasa mtoto mdogo kwa mkonga wake kisha kupita pembeni na kuondoka zake huku mtoto akimkimbilia na tembo akimgeukia kwa huruma

mbona we ulibaki? ama we ndo huyo dogo?
 
Back
Top Bottom