Umewahi Kuchunguza kwanini Nyoka hamdhuru Mtoto!?

Umewahi Kuchunguza kwanini Nyoka hamdhuru Mtoto!?

Kwa hiyo na sisi ni MALAIKA TULIOZEEKA?

Old_Angel_by_jujano.jpg
 
The answer is simple: Law of Love applies. When you act lovely towards anything the reaction you receive is love. Unapomwona nyoka ukahamaki the impression he receives is that you've considered him a threat therefore anakuona wewe ni threat kwake vile vile, lazima ajihami.

Kumbe nyoka anatumia "he"
 
Kuna wakati jf kuna mada nzuri sana za kuelimisha. Kuhusu hili, mimi nimemshuhudia mdogo wangu aitwaye doto akicheza na nyoka, tena akicheka kwelikweli. Mimi na mama tulishitushwa na kicheko.tulitaharuki, tukatulia. Hatimaye yule nyoka akaondoka zake.
 
Mungu wetu ni wa upendo ivyo mtt tunaambiwa ni Malaika, pia tujifunze kwakua nyoka nae anaelewa....zaidi badae
 
Hallo Wana JF, Naomba kujua kutoka kwa yeyote yule Mwenye kujua kwa nn Nyoka hawadhuru Watoto.

Kutia ndani chatu?

Akanambia kuwa vivyo hivyo nikimuona Nyoka akila Chakula kilichoachwa wazi au nikimuona Nyoka amekwea PiPa la Mbege huku akinywa Mvinyo ndani ya Pipa Basi Usije ukamshtua, kwani ukimshtua,hukasirika na kutemea huko Sumu.

Do, hii sikuijua. Nyoka wa Moshi wanakunywa mbege?
 
Inasemekana adrenaline hormone inayozalishwa pale mtu anaposhtuka kwa kumuona nyoka ndio inasababisha ang'atwe kwani nyoka anahisi hatari inayomkabili na anajihami mapema. Na ndio maana inasemekana kama hujamuona nyoka na yeye kakuona hawezi kukudhuru, kwa kuwa hakuna adrenaline inayozalishwa. Wataalamu wanasema nyoka inahisi adrenaline inayozalishwa katika mwili wa binadamu.
Kwa watoto nadhani hiyo ishu ya adrenaline hormone ina-apply, kwa sababu hawajui hatari ya nyoka.
makes sense..
 
Hallo Wana JF,

Naomba kujua kutoka kwa yeyote yule Mwenye kujua kwa nn Nyoka hawadhuru Watoto.

Bibi yangu aliwahi kunisimulia visa Vingi vya Nyoka kukutwa akicheza na Mtoto. Na hakuna hata Mara Moja imeonyesha Mtoto kudhuriwa na Nyoka.
Nikamuuliza ni kwa nn, akanambia hiyo ni "NATURE/ASILI" Imeumbwa Hivyo. Ila akanipa tahadhari kuwa, Unapokutana na tukio kama Hilo ghafla Bin Vuu, Hutakiwi kupiga Kelele. Ukifanya hivyo basi hukasirika na Kumgonga Mtoto.

Akanambia kuwa vivyo hivyo nikimuona Nyoka akila Chakula kilichoachwa wazi au nikimuona Nyoka amekwea PiPa la Mbege huku akinywa Mvinyo ndani ya Pipa Basi Usije ukamshtua, kwani ukimshtua,hukasirika na kutemea huko Sumu.

Kwa yoyte mwenye uelewa Mpana naomba atupe elimu kuhusiana na jambo hili la kushangaza inakuwaje Nyoka amheshimu mtoto kiasi cha kucheza naye tu na kutokumdhuru!??

Nawakilisha kwenu wana Jf kwa ajili ya Upembuzi yakinifu.

Hili Swali Linawafaa Sana Wasukuma ambao Jadi Yao Ni Kuishi na Mijoka na Sitasahau Miaka Yangu 3 Chuoni Mwanza ilikuwa Kukutana na Nyoka Chumbani au ktk Kitanda Chako au Bafuni na Chooni Ni Kitu Cha Kawaida Sana. Jamani Kanda Ya Ziwa Kuna Mijoka Acheni Masihara!!!!!!!!!!!!!! Wasukuma Humu JF hebu Tusaidieni basi na Majibu Ya Jamaa huyo Japo Tunajua Nyoka Wenu Mnafuga Kwa Imani Zenu Zileeeeeeee.......................!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hallo Wana JF, Naomba kujua kutoka kwa yeyote yule Mwenye kujua kwa nn Nyoka hawadhuru Watoto.

Kutia ndani chatu?

Akanambia kuwa vivyo hivyo nikimuona Nyoka akila Chakula kilichoachwa wazi au nikimuona Nyoka amekwea PiPa la Mbege huku akinywa Mvinyo ndani ya Pipa Basi Usije ukamshtua, kwani ukimshtua,hukasirika na kutemea huko Sumu.

Do, hii sikuijua. Nyoka wa Moshi wanakunywa mbege?

Hapo kwenye ''chatu'' wakati wote napitia comments za watu (ambazo nyingi nimezikubali kwa sababu ya maelezo ya kisayansi yaliyotolewa) nilikua najiuliza hilo swali. Hawa nyoka wengine wanagonga au kutema sumu kwa maana ya kujihami na hatari iliyo mbele yao!!! sababu si njaa. Lakini kwa chatu yeye humkamata mnyama kwa maana ya chakula. Sasa kama chatu ana njaa, ''atacheza'' na mtoto? Wale wenye kujua haya watujuze zaidi.
 
mtoto anavyoomuona nyoka wala hashtuki kabisaaaaa tofaut na mtu mzma ambaye akimuona tu lazma ata react either kwa kukimbia or lazma atatafuta kitu cha kujihami nacho hapo ndo tatizo linapoanza kutokea. Bt kwa mtoto yy hawez kushtuka wala akaanza kupga kelele coz hajui ni kitu kipi kizur wala kibaya!!!matokea yake anaweza kutabasam na kuanza kushangaaaaa hiki ni kitu gan
 
mimi nakubaliana na wachangiaji wote kwa hoja zao,lakini kwenye local believes za kwetu sisi hasa upande wamama kwa mtu aliyefatana na mapacha au mapacha na mzazi wa mapacha inasemekana hawezi dhuriwa na nyoka sababu wao nyoka huzaa mapacha pia..Nakumbuka tukio nilisha lishuhudia toka kwa mamangu nyoka aliingia ndani akakutana na mama njiani nyoka akatulia kabisa,na kila mama alipokunja ngumi basi nayeye nyoka nalijikunja bila kumdhuru mpaka alipo kuja mzee kutoa yule nyoka..Lakini naungana kabisa na waliotoa ufafanuzi kibiologia zaidi
 
Inategemea,hta mimi binafsi nishawa kuelekezewa kichwa na nyoka maeneo ya kifuani,na hakunidhuru sababu yeye aliniona ila mimi sikuoma,nilpokuja kustuka nikakimbia,nyoka aina ya swila,nyoka naye ndo akaanza kujihami,
 
Hili Swali Linawafaa Sana Wasukuma ambao Jadi Yao Ni Kuishi na Mijoka na Sitasahau Miaka Yangu 3 Chuoni Mwanza ilikuwa Kukutana na Nyoka Chumbani au ktk Kitanda Chako au Bafuni na Chooni Ni Kitu Cha Kawaida Sana. Jamani Kanda Ya Ziwa Kuna Mijoka Acheni Masihara!!!!!!!!!!!!!! Wasukuma Humu JF hebu Tusaidieni basi na Majibu Ya Jamaa huyo Japo Tunajua Nyoka Wenu Mnafuga Kwa Imani Zenu Zileeeeeeee.......................!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Maneno iko India. Kule si mchezo. Na hao wtt wanacheza nao kweli.

Si uneona hata picha ya tayta?
 
Last edited by a moderator:
Na kwa mama mjamzito jee? Hii pia nimewahi kuskia kuwa nyoka napenda kuwa karibu na mama mjamzito na wala hamdhuru
 
Katavi mimi nimtalamu wa wanyama pori wadudu na mimea. Ulichokisema mwanzo upo sahihi
 
sijajua kama ni kweli ila nadhani ni bahati 2 ya mtt kuto kundurika maana tuxha wahi kumuona mtt kang'atwa lakini sijajua kwa upana lakini 2kio hilo lilitokea

Kwawatoto i bahati ndiyo lakini inaweza pia ikaw ni zaidi ya hapo. Je, ulishawahi kusikia pia kuwa mtoto asiyeweza kuongea ana uwezo wa kuona vitu visivyoweza kuonekana na mtu mzima, sambamba na wanyam wa kufuga kama mbwa, paka, ng'ombe, kondoo, nk. Sina proof ila huwa nasikia hivyo.
 
Mmm nakubaliana na wadau wengi kuhusu kutokuwa na taharuki ukimuona nyoka. Kila kiumbe hai kina njia zake za kujilinda, Binadu (mtu mzima mwenye ufahamu) anajilindakwa njia mbalimbali(Mishale, bunduki, Ngumi, n.k), kuna aina ya miti ambayo ina miba mikali na mtu/wanyama wengine hawawezi kuupanda ila ukipita kawaida hauna madhara, Nyoka pia anapona kunahatari anajihami ndo kumgonga mtu. Kwa ishu ya motto hana madhara kwa nyoka hivyo anakuwa salama. Mwaka jana ilitokea kwa motto wangu akiwa miezi 11, mama yake alimuweka sebuleni sakafuni akicheza(kutambaa) kurudi akamkuta anacheza na nyoka(mdogo) anaivuta aipeleke mdomoni inateleza. Aliduwaa na ikaondoka naye ndo akambeba mtoto, Watoto wanabaraka zao za ulinzi wa Mungu
 
Back
Top Bottom