Umesoma shule ya bweni wewe?

Hiyo mm niliikuta Kibasila Hostel Lakini zaidi ni ile ya JKT Makutupora ni Mustin la bati na Sembe lisilokobiolewa huo ugali kwa sahani la plastic mbona mzuri? Ulizia mabinti wa JKT Operation ................. walivyokuwa wakitupiga vikumbo maana hawapangi foleni ya Wanawake wanawaita Mabint wao wanapambana na wanaume tu tena kuRUDIA KULA (BUST)
 

Mkuu nimecheka mpaka watu wakanishangaa! Nimekumbuka kukatwa ubao! Usiombe kiranja wa kugawa awe ni adui yako siku hiyo utakatwa ubao yaani unawekewa slice ya sembe na maharage kumi! Yaani kumi hile moja mbili tatu... hadi kumi tu! Ukinusurika hilo basi unapigwa deshi na wataalamu wa midabo! Yaani mtu anakuwahi anamimina sahani yako kwenye yake unaambulia patupu. Sisi mesi ilikuwa ya kugawia chakula ikipigwa kengere mnaingia kuchukua na kulia popote unakotaka, kisa viti na meza hakuna mesini!!
 
Napakumbuka Iringa girls high school a.k.a Zoo ladies camp
 
Malangali boyz daaaaaaaaa ilikuwa kiama yan,hiyo menu iliniuma sn sn
 
Ajabu watu walikua wananenepa balaa. Form 1 anakuja mdogoo mpe miezi sita tu utaona dona litakavyomfutua
 
mambo ya kiunga Tanga Tech. siku ya wali nyama ndiyo siku ya madogo wa o-level kugegedana.
 
Dah! sisi tulikuwa tunaliita dongo, lilikuwa dongo kweli kwa sababu ilikuwa ni dona na sio sembe kama hii
 
Duh, longtime kishenzi. Nilipigaga buku pale Tosa.
 
 

Bagamoyo Secondary School (BSS)
 
Aisee, na ule ugali wa unga wa njano!!!! Halafu na maharage yote ni wadudu weupe wanaelea juu!!!! Yet tulijitahidi tukasoma kwa bidii na kupasua vikali!!!!!! Hawa wajukuu zetu shule mpaka na TV, wali kuku, chips kuku, eti sijui chai mkate, eti sijui ni kitu gani!!!!! Kwa nini wasifeli na madaraja waanze kuyapangua???? Tena ugali ulikuwa ni dona, hakuna cha kukoboa wala nini!!! Uji wa dona, wali ni mara moja kwa wiki au mwezi!!! Na wakati mwingine hali ikiwa ngumu kama Wizara haikutoa fungu la kutosha basi wali ni mpaka graduation tu!!! Hapo ni kupigana za uso kabisa maana kila mtu anagombania wali na top layer!!! Tumetoka mbali sana.
 
Hayo maharage nilikutana nayo pale Mara Sekondari tangu mwaka 1993 hadi 1996. Tulilishwa maharage na mwalimu Magesa (Dingi) kidogo yaote tumboni. Nilipoenda Mkwawa kwa mwalimu Mgohamwenda ndipo rate ya maharage ikapungua.
 
JF patamu sana. hii ngoma Minaki enzi za marehemu Mjare mkuu wa shale.. ukileta fujo kinarukia na ng'wenzi kilikuwa kifupi kinavizia wanaofanya fujo kugombania NGUNA.
 
maharage ya pale salute!juu lazima ukutane na wadudu weupe na weusi...

Wadudu unawatoa kwa Spoon.... ukiwa na blueband unaenjoy sana kwenye maharagwe... Watu waliokuwa wanafaidi wale wa Diet... Unawakuta wanapukuchua maganda ya maharagwe na kuchanganya na Makande yao Meupe yasiyo na maharagwe....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…