nilikuwa nafanya kazi mahali sasa kulikuwa na mwenzangu tunafanya nae kazi lakini ilitokea akawa anachukiwa sana na mke wa boss kutokana tu na sababu za wivu wa kike. sasa nilikuwa namuhurumia sana kutokana na jinsi alivyokuwa ananyanyaswa, ikatokea mimi nikapata kazi mahali pengine ambapo kwenye hiyo ofice nikapewa kuwa supervisor wa wafanyakazi wengine, yani akitoka boss ndio mimi, kwa huruma zangu nikamfanyia mpango yule mwenzangu aliyekuwa ananyanyasika kule akaja akapata kazi pale nilipokuwa, nikamfundisha kazi mpaka akaiva haswaa, aisee alianza kuyapika majungu ya hatari kuanzia kwa boss mpaka wafanyakazi wengine, nilichukiwa na kila mtu bila kosa, nikashangaa tu napewa likizo,na boss mpaka hapo nitakapoitwa, huwezi amini ndio ilikuwa mwisho wa kibarua changu na yeye akachukua nafasi yangu. sitasahau hili jambo mpaka nakufa