Umafia, ubabe na ujasusi wa biashara za Kariakoo

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,789
Kikiwa ndio kitovu kikubwa cha biashara nyingi za nchi kwa mizigo inayotoka nje hasa China.. Kuna wababe na mafioso ndio wamezikamata biashara za huo mji na wengine wote ni wapagazi na wajakazi kulingana na makundi yao lakini mwisho wa siku kila mtu anapata kulingana na urefu wa kamba yake!

Hawa ma godfather ndio wamiliki wa mabohari makubwa na utitiri wa mafremu.. .. Wakiuza jumla na rejareja kupitia mtandao wa wachuuzi wao waliotapakaa kwenye fremu, barabara na kila aina ya upenyo..hawa wao kuingiza miliom mia moja kwa siku ni jambo la kawaida

Hawa mabwanyenye wenye hela wao hawangaiki juani bali ni wapanga mipango na wachora racket.. Wanachoangalia wao kupitia mawakala wao ni biashara gani imeshika soko na mwanzilishi ni nani...na ana bei gani.

Ni kipindi ukiwa umeshaitangaza biashara yako mpya sokoni na kujaza wateja.. Mafioso hao huwatuma vijana mawakala wao na kukununuza baaadhi ya bidhaa zako... Hizo hurushwa China na kutafuta chimbo lake...

Wewe huku bila habari umeshapelelezwa mzigo wako unaisha na kuwahi China kuchukua mzigo mkubwa zaidi... Pengine container moja au mbili.. Wakati unatua China wenzako washafungasha container kumi za mzigo kama wako.. Na kwa wachina jinsi unavyochukua mzigo mkubwa ndivyo bei inavyopungua

Ukija kurudi bongo na mzigo wako wa container 2 unakuta sokoni bidhaa imetapakaa tena kwa bei ya chini zaidi kuliko yako!
Hapo utafanyaje?

Huna jinsi bali kupunguza bei ama kuwauzia mafioso hao mzigo wako wote...!! Kuna umafia mwingi sana Kariakoo usijaribu kujifanya mjanja kama huna nguvu za kutosha...! Biashara nyingi ni mali kauli na kuaminiana.. Ole wako ulete usela pori uchukue mzigo halafu usirejeshe pesa.. Wanakufuturu kimya kimya...

Biashara nyingi za Kariakoo ni kukopana pesa na kurejesha kwa siku, wiki na mwezi.. Ole wako uingie mitini usirejeshe.. Kesi zao hawapeleki mahakamani wanamaliza wenyewe kwa namna ya kuogofya na kutisha sana lakini kimya kimya
Kariakoo mtaondoka wote kwenda China kufunga mzigo lakini mkifika huko kila mtu anaingia chimbo lake.. Hakuna kuaminiana

Kwa upande wa nguvu za giza ndio usiseme kuna makafara ya kutosha kuliko sehemu nyingine yoyote nchini...kuna misukule ya kutosha kuliko sehemu nyingine yoyote Tanzania Kuna milango ya kuzimu

Kuna uchawi wa kutosha.. Kila mtu anakinga yake! Kila mtu anatafuta mvuto... Vita ya kiroho Kariakoo huwezi kuipata popote nchini
Kuna viumbe na wanyama wa kutisha lakini wote wako kwenye maumbo ya kibinadamu

Kuna vyumba vya mateso, kuna jela za siri, kuna utumwa wa kuanzia, kwenye biashara, nyumbani na sehemu za starehe.. Kuna watumwa wa ngono Kariakoo.. Ombaomba na watoto wa mitaani si wote ni halisi . .. Ni biashara za watu zile.. Tena zenye kipato kizuri tuu...

Soko kuu la Kariakoo limeungua(zwa) limeteketeza vingi lakini si vyote.. Vilinge bado viko hai na ule mlango wa kuzimu kule shimoni bado uko wazi... Ukitaka kupajua Kariakoo vizuri ingia pale shimoni usiku
 
Leo umeandika kitu kikubwa sana mshana,Kariakoo vita ukivipigana utajiri huu hapa.

Kariakoo Inataka ubabe haswaaa watu wanaoanza kusaka utajiri,Huku unaweza uziwa kitu bei mara 50 ya bei halisi na ukasogea mbele unakuta hicho kitu mara 100 cheap ya bei halisi afu unabaki kusonya tu, Watu Wana fanya biashara za kutisha sanaaa,Jamaa angu alinambia kama unataka utajiri upo kariakoo,muhimu kazaa roho haswaaa na ujifanye una serikali yako mwenyewe inayoratibu mambo yako,yani hata reset hyo wanaita ya EFD hata ya 20million utapata KWA kutoa elfu10 tu unatafutiwa,Watu wa procurement WANAPIGA sana pesa wakienda kkoo na kufoji reset.

Bado najiuliza,jamaa kaunguliwa maduka Zaid ya manne yalikua yamejaa mali zai ya 300mill.

Within a week kafungua duka la Zaid ya million800,Huyu 10years ago alikua mzururaji tu kkoo,tena kibarua wa sokoni ndani hapo.Now anamiliki utajiri wa kufuru.
 
Leo umeandika kitu kikubwa sana mshana,Kariakoo vita ukivipigana utajiri huu hapa.

Kariakoo Inataka ubabe haswaaa watu wanaoanza kusaka utajiri,Huku unaweza uziwa kitu bei mara 50 ya bei halisi na ukasogea mbele unakuta hicho kitu mara 100 cheap ya bei halisi afu unabaki kusonya tu,Watu Wana fanya biashara za kutisha sanaaa,Jamaa angu alinambia kama unataka utajiri upo kariakoo,muhimu kazaa roho haswaaa na ujifanye una serikali y'all mwenyewe inayoratibu mambo yako,yani hata reset hyo wanaita ya EFD hata ya 20million utapata KWA kutoa elfu10 tu unatafutiwa,Watu wa procurement WANAPIGA sana pesa wakienda kkoo na kufoji reset.

Bado najiuliza,jamaa kaunguliwa maduka Zaid ya manne yalikua yamejaa mali zai ya 300mill.

Within a week kafungua duka la Zaid ya million800,Huyu 10years ago alikua mzururaji tu kkoo,tena kibarua wa sokoni ndani hapo.Now anamiliki utajiri wa kufuru.
Bado najiuliza,jamaa kaunguliwa maduka Zaid ya manne yalikua yamejaa mali zai ya 300mill.

Within a week kafungua duka la Zaid ya million800,Huyu 10years ago alikua mzururaji tu kkoo,tena kibarua wa sokoni ndani hapo.Now anamiliki utajiri wa kufuru.
 
Ila kwel kuna kitabu nilikisoma mwaka Jana kinasimuliwa na mtu mmoja alienusurika kutoka kwny msukule alidumu kwa mwez km sio wik akafanikiwa kutoroka,lakin alisimulia maisha ya umsukule japo yy alibahatika hakukatwa ulim,anasema walikua wakipelekwa kariakoo wanakodiwa na matajir kupakua mizigo , sasa yy nguvu zilikua zinamuishia coz alisahaulika kukatwa ulim hivo alikua anakoswa ile nguvu ya asil ya umsukule wenzake walikua wanapiga mzigo balaa,yy gunia mbil anachecheme lakin alijikaza hivohivo asigundulike ,lakin mwishon walipelekwa Zanzibar kuna mchaw mmoja akamgundua akataka kumharibia hivyo akatoroka kwa kukimbia (walikodiwa uko Zanzibar na wachaw wakalime mashamba)yaan alisimlia mambo meng ya kustaajabisha ,dunia hii ukitaka kuichunguza ina mambo meng ya kustaajabisha na kutisha sana
 
Ila kwel kuna kitabu nilikisoma mwaka Jana kinasimuliwa na mtu mmoja alienusurika kutoka kwny msukule alidumu kwa mwez km sio wik akafanikiwa kutoroka,lakin alisimulia maisha ya umsukule japo yy alibahatika hakukatwa ulim,anasema walikua wakipelekwa kariakoo wanakodiwa na matajir kupakua mizigo , sasa yy nguvu zilikua zinamuishia coz alisahaulika kukatwa ulim hivo alikua anakoswa ile nguvu ya asil ya umsukule wenzake walikua wanapiga mzigo balaa,yy gunia mbil anachecheme lakin alijikaza hivohivo asigundulike ,lakin mwishon walipelekwa Zanzibar kuna mchaw mmoja akamgundua akataka kumharibia hivyo akatoroka kwa kukimbia (walikodiwa uko Zanzibar na wachaw wakalime mashamba)yaan alisimlia mambo meng ya kustaajabisha ,dunia hii ukitaka kuichunguza ina mambo meng ya kustaajabisha na kutisha sana
Chai hizo
 
Kikiwa ndio kitovu kikubwa cha biashara nyingi za nchi kwa mizigo inayotoka nje hasa China.. Kuna wababe na mafioso ndio wamezikamata biashara za huo mji na wengine wote ni wapagazi na wajakazi kulingana na makundi yao lakini mwisho wa siku kila mtu anapata kulingana na urefu wa kamba yake!
Hawa ma godfather ndio wamiliki wa mabohari makubwa na utitiri wa mafremu.. .. Wakiuza jumla na rejareja kupitia mtandao wa wachuuzi wao
Kariakoo ni habari nyingine.

Najiuliza wale Wachina wanapawezaje pale?
 
Back
Top Bottom