Ulokole wa facebook

Ulokole wa facebook

kwanini mambo yanapoenda sivo ndo unaokoka? Okoka mapema,wengine ni wafiki tu me nawaonaga unamtokea anakubali unajigia na kisha unamtema
 
Nashangaa na wewe...! Nini tatizo mtu kuandika kilichoujaza moyo wake? Hata kama anaanguka katika dhambi kila dakika, nani asiyefanya dhambi?

By the way, imani ya mtu ipo kwenye nafsi yake. Wale wanaobeza na kuponda naona ndio wanafiki. Hata hivyo, tunafanya dhambi na inafikia wakati tunabadilika, iwe kwa sababu ya umri, maradhi, matstizo ya dunia, nk.

#totalCrap ..
Nakubaliana na wewe kabisaa, aliyenadhambi ndio anayemwitaji mwokozi, hata Yesu mwenyewe alisema amekuja kwa walio na dhambi.
 
wamekukosea nini wana wa mungu? si kweli kwamba ulokole ni mbaya lahasha ni mzuri sana tena sana. na pia kwenye msafara wa mamba kenge pia wamo. hata kanisani wachawi na wazinzi pia wamo na dini bado zipo. kimsingi uokovu ni wamtu sio wa watu. ikiwa umempokea yesu na kufuata yale neno la mungu lisemalo basi wewe umeokoka tena watenda vema.na ikiwa hutendi sawa na neno la mungu basi wewe ujiesabu ni kupoteza muda2 na wokovu au ulokole utabaki pale pale kwani alie uleta uokovu au ulokole ni yesu mwenyewe. kimsingi na kushauri kama hujampokea yesu kama bwana na mwokozi wa maisha yako ni fursa ya kuokoka ni vema ukawakosoa ukiwa ndani ya uokovu ili ujue ukweli.je wokovu ukoje?
amen ubarikiwe mkuu.
 
asante umeongea vyema, tatizo watu wengine hawana maisha yao kutwa kufuatilia ya wengine.

Wala sio kufwatilia maisha...wewe km in rafiki yangu was Facebook automatically nikilog in au nikiwa online lazima nione kwenye new feed
 
Yani kila mtu anashusha mistari mpaka inakuwa ngumu kumaliza feeds zote...mi kuna watu nashindwa kujua wameokoka, fashion, au frustration maana ni washikaji na ni watu wa kawaida tu all of a sudden siku hizi kila uchao ni full mistari...isije kuwa wana frustration wanahitaji counselling...maana mistari yenyewe ni ile ya mafumbo mafumbo wanachomoa toka kwenye baibo...

imagine mtu anaandika...'Bwana ndiye mchungaji wangu nimuogope nani'...kuna tofauti gani na ile 'karibu mgeni, utakalolikuta nyumba hii liache humu humu'...au na mimi niamue kuandike 'si kila anayeita bwana bwana atauona ufalme wa mbinguni' hapo itakuwa vipi...mipasho tu...

Maana hata kama ni mahubiri uangalie na audience yenyewe...

Wala sio kufwatilia maisha...wewe km in rafiki yangu was Facebook automatically nikilog in au nikiwa online lazima nione kwenye new feed
 
haaaa we Viol usintafutie balaa mie..,

halafu kwani hujaona mambo yangu mtaa wa pili.
nimeona si ndo hivo una maringo nikuambia dada vipi,unasonya huku sehemu za nyuma ukitingisha,haya bhana tesa tu we ngoma ghali
 
Yani kila mtu anashusha mistari mpaka inakuwa ngumu kumaliza feeds zote...mi kuna watu nashindwa kujua wameokoka, fashion, au frustration maana ni washikaji na ni watu wa kawaida tu all of a sudden siku hizi kila uchao ni full mistari...isije kuwa wana frustration wanahitaji counselling...maana mistari yenyewe ni ile ya mafumbo mafumbo wanachomoa toka kwenye baibo...

imagine mtu anaandika...'Bwana ndiye mchungaji wangu nimuogope nani'...kuna tofauti gani na ile 'karibu mgeni, utakalolikuta nyumba hii liache humu humu'...au na mimi niamue kuandike 'si kila anayeita bwana bwana atauona ufalme wa mbinguni' hapo itakuwa vipi...mipasho tu...

Maana hata kama ni mahubiri uangalie na audience yenyewe...
hao wa bwana asifiwe watoswe sasa na malengo yao kukwama,utaona wanaporomosha matusi
 
nimeona si ndo hivo una maringo nikuambia dada vipi,unasonya huku sehemu za nyuma ukitingisha,haya bhana tesa tu we ngoma ghali

hahaaaaaaa nimechekaje ..
halafu nakumbukia ile ngoma ya prof Jay zali la mentali..
 
Back
Top Bottom