Ulokole wa facebook

Ulokole wa facebook

We Kama mlokole pita kuleeeee na ufake wenu. Wakati mnagalagazwa majanini aaaagg ila mkija hapa mnajifanya Kama sio wale...kwendreeeeeni
 
Mrembo unapiga usoni tu duh...sehemu zingine huzioni au we ni specialist wa za uso tu! Wahurumie kidogo.
 
Ukiona mtu anaingia kwenye Ulokole ujue jua lishazama hasa 30+yrs


Sent from my iPad Air using JamiiForums
 
Nimeipenda sana facebook kwa hilo. Zamani watu walikuwa wanaona kama kumpokea Yesu na kumkiri hadharani ni kama ushamba flani hivi. Sasa wengine wanapoona sisi wajanja tunamkiri Yesu hadharani hasa kwenye fb, nao wanahamasika. Kwa kweli sasa hivi Yesu ana wafuasi wengin sana ambao wanamkiri hadharani tofauti na miaka minne hivi iliyopita. Fb ina mchango mkubwa kwenye hilo...
 
alafu kuna watu wengne wanaichukulia fb very serious,mtu umepost kitu fb wanakutafuta kwenye simu.
 
Sio ulokole wa dizaini hiyo ulokole unazungumziwa hapa ni mwingine
mfano wewe khantwe useme umechoshwa na mmeo unataka kuchepuka
heeee tutakurushia maneno hadi ukomeeee
mi mwenyewe ntakusema wakati muda huo naandika nipo juu ya kifua cha mchepuko wangu na mie

this is very true!
 
Salamu kwenu waungwana wa jukwaa hili.

Salamu pia ziwaendee wale walokole wa mitandaoni wakati nje ya mitandao wanajijua wenyewe vile waishivyo.

Binafsi ni mdau mzuri wa facebook (hasa kipande ya usomaji zaidi wa kile wadau wengine wanachopost). Kwa ufupi kule watu walio wengi ni wema sana, full kuposti mistari ya biblia na kukemea uovu yani kule unaweza kujiona wewe ndio shetani peke yako duniani. Wnawake wengi walio single (hasa wale walioko kwenye 30's na hakijaeleweka) ndio usiseme kwa injili. Yani ni kama dozi (asubuhi mchana na jioni). Wakati mwingine hata inakuwa ngumu kwetu sie kuishi maisha yetu ya ukweli manake wahukumu ni wengi sana.
Sasa mie nilishangaa mmoja wa walokole hao maarufu kwa kuposti mistari ambae awali alikuwa anaishi kinyumba na njemba moja alipokuwa na mimba siku ya ndoa yake (na njemba nyingine).Sasa ulokole na mimba kabla ya ndoa wapi na wapi?

Wanawake wengi wameamua kuutumia ulokole km gia ya kuwanasa wakaka wengi wa karne ya 21 ambao wanaziogopa ndoa
km ukoma. Ule ulokole kwa asilimia kubwa ni fake (Sio kwa wote lakini). Mtu amekula dunia wee hadi dunia imemchoka, mtaani alishachakaza sasa anaona usiku unakaribia suluhisho ni mwendo wa kuposti verse tu ili awanase walio wengi. Zinduka but that is none of my business
Mrembo by Nature ushapata mchumba au mme?
 
Last edited by a moderator:
Hii tabia unadhani iko kwa single tu...mbona hata walioolewa naona ni full kurusha mistari...mimi wala sisomagi naona wanaboa tu...yani unaonekana kama huko kwenye matatizo fulani vile...tena wala si walokole wala wacha Mungu kivile...naona ni fashion...
wenye ndoa ndo zaidi,huwa kwenye profile wameandika married na unaona kaweka pics za familia yake yote ila inbox atasema tuna mgongoro
 
Back
Top Bottom