Uliza lolote kuhusu mgogoro ndani ya DRC hasa mapigano kati ya M23 na FARDC

Ukigusia madini ya DRC napenda kukushakikishia kuwa naijua vizuri sana maana ndiyoinayoniweka mjini. Ni kweli Rwanda wananufaika sana na madini ya RDC. Sina uhakika na uhusika wa USA moja kwa moja na madini ya DRC ila wana urafiki wa damu na RWANDA. Ninachokiona mimi ni kuwa jamaa hawana interest tena na Rwanda (Kumbuka they have only permanet interest but not permanent friend).

Kwani si inasemekana marekani anashiriki kwa kiasi kikubwa sana kufanya wizi wa madini congo,kimetokea nini mpaka akaamua kumbadilikia m23(rwanda) aliyeko on ground kupiga mzigo?
 
Karibu kaka. Huku yaani tupo wengi kiasi kwamba masuala ya SUPU, CHAPATI, UGALI ni kama bongo. Uliza madereva hasa wa Azam wanaokuja mara kwa mara. Always sehemu yenye problems, there are opportunity.

Mkuu Flash Hider umenifurahisha sana.Ila ntakusumbua wakati mwingine kuhusu biashara ya madini huko.Nafikira kuja huko hali ikitulia.
 
Kwanza hongera kwa kazi nzuri ingawa ninajiuliza kama ni mfanyabiashara wa kawaida kwa sababu ya uelewa waku upo juu. Ninaomba kujua katika hali hiyo ya mgogoro kuna ndege za abiria zinazotua Goma kutoka miji au nchi nyingine? Na kwanini DRC historia ya mapinduzi na mauji ya viongozi tangu miaka hiyo ya kina Lumumba kama sikosei?
 
nimepitia mkuu na nashukuru kwa majibu yako
nasikia nkunda alipandikizwa na kinamseveni na kagame kwa ajili ya kupora mali ya drc kulipia ahadi walizopeana na kabila, na kunatetesi hawa ndo walimuua huyu mzee?

Uki-link chanzo cha mgogoro ambao ulipelekea mauaji ya Kabila baba, ni wazi kuwa Rwanda na hata Uganda wanahusika. Hebu jaribu kusoma historia ya Nkunda utagundua kuwa ni Mnyarwanda aliyezaliwa DRC. Kuapnikizwa kupo wazi kabisa hakuihitaji research ni logical thinking tu.
 
Uki-link chanzo cha mgogoro ambao ulipelekea mauaji ya Kabila baba, ni wazi kuwa Rwanda na hata Uganda wanahusika. Hebu jaribu kusoma historia ya Nkunda utagundua kuwa ni Mnyarwanda aliyezaliwa DRC. Kuapnikizwa kupo wazi kabisa hakuihitaji research ni logical thinking tu.
hii vita haiiishi labda DRC waishiwe madini mkuu!
 
Kaka msiwe na shaka kabisa na uelewa wangu. Sina elimu kubwa, nilimaliza pale mazengo na kusoma masuala ya madini kidogo. Ninafuatilia hali ya dunia inavyoenda nia ni kuhakikisha nakwenda na upepo wa fursa. Hapa GOMA ndege zinatua sana tu. Hata Rwanda Air pia inatua hapa.

Kama nilivyosema mtazamo wangu ni kuwa matatizo haya huenda yasiishe leo wala kesho. FRANCOPHONE zote zinatabia ya kuwa na matatizo yasiyoisha. Inasemekana watawala hao walikuwa na tabia ya kutofundisha au kutoacha good political infrustructure wanapoondoka. Hebu cheki Mali, CAR, yaani west Africa yote ni migogoro isiyoisha.

Kwanza hongera kwa kazi nzuri ingawa ninajiuliza kama ni mfanyabiashara wa kawaida kwa sababu ya uelewa waku upo juu. Ninaomba kujua katika hali hiyo ya mgogoro kuna ndege za abiria zinazotua Goma kutoka miji au nchi nyingine? Na kwanini DRC historia ya mapinduzi na mauji ya viongozi tangu miaka hiyo ya kina Lumumba kama sikosei?
 
Karibu sana na ninawaomba ndugu zang, kwa haya ninayoyaona huku na kwa jinsi jamaa wanavyohangaika, tuitunze vyema amani tuliyonayo bila kujali mitazamo yetu kisiasa. Kuna siku nitawawekea baadhi ya picha muone jinsi watu wanavyopata tabu.

Tanzania yangu haijaishiwa wazalendo hongera mkuu FLASH HIDER kwa taarifa hizi binafsi nimenufaika..
 
Karibu kaka. Huku yaani tupo wengi kiasi kwamba masuala ya SUPU, CHAPATI, UGALI ni kama bongo. Uliza madereva hasa wa Azam wanaokuja mara kwa mara. Always sehemu yenye problems, there are opportunity.

Ofcourse wanasema "Penye Mwamba Mgumu ndio Penye mafuta" Ni PM namba yako na e-mail tutakuwa tunachat mara mojamoja.
 
Bwana Sixgates,

Suala moja ambalo ningependa watu wote waelewe ni kuwa ukweli DRC ina matatizo mengi kuanzia Political, Economical and Security. M23 ni sehemu ndogo sana ya tatizo la DRC. Mengi yanatakiwa yafanyike.

Mkuu, kwa nyongeza tu historia ya DRC tokea uhuru wao pia ni sehemu ya tatizo. Swali langu ni kuwa DRC haijawahi kutulia tokea ilipopata uhuru, migogoro na mapigano yamekuwapo kwa miaka. Je kikosi cha UN cha wakati huu kina nini kipya cha kutoa matumaini kuwa sasa hatimaye DRC itatulia kimoja?
 
Nkunda kwa sasa yupo under house arrest huko Rwanda. Ana uhusiano mkubwa na M23 kwani yeye andiyo mwanzilishi wa CNDP(The National Congress for the Defence of the People (kwa kifaransa Congrès national pour la défense du peuple) ambalo ndiyo chumbuko la M23. Hebu pitia uzi huu kwa ujumla nimejaribu kuelezea uhusiano wa M23 na NKUNDA LAURENT
Nkunda ana uhusiano mkubwa na M23, na muda huo inasemekana Kagame anawasaidia M23; imekuwaje tena Nkunda awe under arrest huko Rwanda?
 
Kaka kama nilivyoeleza awali sina habari nyingi. Hya uliyonipa kama inasemekana nitajaribu na mimi kufuatilia kuelewa ukweli upo wapi. Kwa mtazamo wangu, Mgogoro wa DRC ni complex pengine kuliko migogoro mingi katika dunia hii. Unahusisha Ecomonic, Political, security, socialogy nk.

Suala la USA kupoteza radha kwa Rwanda lipo wazi, ingawa sikuwa nafahamu kikubwa ninini. Tanzania kama nchi hapa DRC inatajwa kama mkombozi wa nchi za Maziwa Makuu ambapo endapo kuna kikao chochote na TZ isishiriki, basi kikao hakifanyiki. Ukweli watake wasitake geographical location ya nchi yetu, na historia yetu vinatupa fursa nzuri ya kupendwa na kutegemewa.

Mdau hebu elezea ushiriki wa marekani katika mgogoro huu upoje? habari zilizopo ni kuwa kuna uhusika mkubwa wa mataifa ya kigeni hasa marekani. Interest kuu ni rasilimali zilizopo Congo (zaidi madini).Walimtumia Kagame akishirikiana na Mu7 kuharibu hali ya amani consistently ili waendelee kutimiza interest zao, lakini pia ushiriki wa tanzania katika kipindi hiki una mgongo wa Marekani.(Kwa kifupi Tanzania imetumiwa na Marekani)
Kagame hajatenda kadiri ya maelekezo ya marekani kwani naye amekuwa akichota rasilimali na kuijenga Rwanda na kufaidikia kuliko anayemtuma (hii pia inasemekana ndo chachu ya maendeleo ya haraka ya Rwanda). Hivyo Marekani anatumia JWTZ kuimaliza M23 yenye ufadhili wa Kagame na Mu7 kama njia ya kumshikisha adabu Rwanda. Inasemekana ziara ya juzi iliyowakutanisha kwa pamoja Obama na Bush hapa Tanzania ina nyayo za huu mgogoro. Hebu endelea kufunguka kuhusu hizi nilizoziita "inasemekana, inasemekana, inasemekana....."
 
Nasikia kulikuwa na deal kati ya DRC an Rwanda kuhusu kukamatwa kwake. Pia UN walilazimisha Nkunda akamatwe. Ujue yupo under house arrest lakini nasikia ni kama protection maana akiachiwa tu atakamatwa na DRC maana kimsingi ni raia wa DRC.

Nkunda ana uhusiano mkubwa na M23, na muda huo inasemekana Kagame anawasaidia M23; imekuwaje tena Nkunda awe under arrest huko Rwanda?
 
Habari hiyo ipo na ndiyo political agenda ya M23 na jamaa zao wa Rwanda.

Kuna tetesi kuwa banyamulenge wakishirikiana na m23 wanataka kuimega DRC vipande viwili ili watangaze taifa jipya la republic of kivu ili iwe kama ilivyo tokea kwa sudani hili liko vip?
 
Nimeeleza awali kuwa commitment ni kubwa zaidi kwani kikosi hiki kinatoka Africa. African problems can best be solved by africans themselves. Unadhani wahindi, Pakistan, Bangradeshi wana uchungu na waafrika? Pili nasikia UN imewaongezea uwezo wa kisheria wa kuapambana na waasi hawa.

Mkuu, kwa nyongeza tu historia ya DRC tokea uhuru wao pia ni sehemu ya tatizo. Swali langu ni kuwa DRC haijawahi kutulia tokea ilipopata uhuru, migogoro na mapigano yamekuwapo kwa miaka. Je kikosi cha UN cha wakati huu kina nini kipya cha kutoa matumaini kuwa sasa hatimaye DRC itatulia kimoja?
 
Back
Top Bottom