Uliza lolote kuhusu mgogoro ndani ya DRC hasa mapigano kati ya M23 na FARDC

Flash hider hivi rwanda kuwasaidia m23 wanasaidiwa na nani? Na ni kwa nini congo toka miaka hiyo ya 1960
mpaka leo wanashindwa kuituliza nchi yao?
 
umenena vyema kuwa wewe ni mtanzania ambaye umelowea goma. Inaonekana huna habari na amri ya jwtz kuwa sisi wananchi haturuhusiwi kuongelea masuala ya vita ya huko congo mpaka kwa kibali chao. Angalia usije ukaingia matatizoni na jeshi letu kwa kuongelea vita ambayo tayari kuna katazo la chombo chetu cha ulinzi na usalama.

ninafanya hivi kwa nia njema na nadhani sijaharibu hali ya hewa
 
Nkunda kwa sasa yupo under house arrest huko Rwanda. Ana uhusiano mkubwa na M23 kwani yeye andiyo mwanzilishi wa CNDP(The National Congress for the Defence of the People (kwa kifaransa Congrès national pour la défense du peuple) ambalo ndiyo chumbuko la M23. Hebu pitia uzi huu kwa ujumla nimejaribu kuelezea uhusiano wa M23 na NKUNDA LAURENT

mkuu Nkunda ninani na yuko wapi kwa sasa?
anauhusiano na m23?
 
Kuna fununu kuwa wakati wa nyuma majeshi ya U.N yalituhumiwa kufanya biashara ya silaha na madini kwa waasi hasa Nkunda.Pia kuna fununu kuwa Nkunda alikuwa supported na belgium through Rwanda.Ni kweli mambo hayo yalikuwepo?ni nini kimeleta tofauti ya utendaji kati ya majeshi ya UN yaliyopita na haya ya sasa yaliyosheheni wabongo?
 
Sijakuelewa unavyozungumzia wasaidizi wa karibu! kama una maanisha washauri wake ukweli siwezi kujua uwezo wao zaidi ya kupima output ya uongozi wake. Nionavyo mimi wanajitahidi kwasababu DRC ni nchi kubwa imepitia matatizo mengi lakini pamoja na hayo amejaribu kuiweka sawa na kuwepo madarakani mpaka muda huu.

Sula la uraia wa Joseph Kabila ukweli sielewi kiundani. Ninachofahamu ni kuwa yeye anatokea Katanga (Ilipo timu ya TP Mazembe). Kule watu wengi wanazungumza kiswahili. Kwa vile yeye alikulia na kusomea TZ hivyo kuna challenge ya kutoelewa ipasavyo kifaransa na kilingala, lungha zinazotumika sana hapa DRC. Hiyo ni challenge kwake kisiasa ingawa to me is nothing, awe anajua au hajui si issue, tunataka rais anayeweza kazi yake.

Mm kaka napenda kuuliza maswali machache...wasaidizi wa karibu wa rais kabila ni watu wenye uwezo kiasi gani? Wa kumshauri na pia suala la kwamba rais kabila sio mkongo je linainfluence chochote kwenye governance ya raisi kabila
 
Hivyi ninvyoandika ninaangalia TV hapa, miji yote ambayo ilikuwa imekaliwa na M23 imekwishachukuliwa na FARDC. Kanzia Kiwanja, Rumangabo, Katale, Kibati (ulichukuliwa siku nyingi) yote ipo chini ya FARDC. Wamebakiza mji wa BUNAGANA ambapo ni mpakani kabisa na Uganda. Bila shaka kufikia Kesho mtasikia M23 imekwisha. Tuombe yasitokee tena mauaji kwa JWTZ maana naambiwa wanafanya kweli huko front.

Mkuu unataka kusema wanajeshi wa tanzania wapo frontline wakipambana na m23? mbona naskia wanajeshi wetu kazi yao ni kulinda raia wa goma wasishambuliwe?. naomba ufafanuzi. Mia
 
Kimsingi kwa andiko hili, sasa umejibu ombi langu la awali la kusema japo kwa kifupi kuhusu unachokijua kuhusu mgogoro huu. Asante kwa historia hii.

ok, ngoja niwape hili ingawa kwa ufupi

Mgogoro katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (Democratic Republic of Congo "DRC") una historia ndefu. Tokea nchi hiyo ipate uhuru wake kutoka kwa Ubeligiji hapo tarehe 30 Juni 1960, haijawahi kushuhudia hali ya kiusalama ya muda mrefu. Migogoro isiyopata ufumbuzi w kudumu ilianza mara tu baada ya uchanguzi wa kwanza nchini humo uliomweka Patrice Lumumba kuwa Waziri Mkuu na Joseph Kazavubu kuwa Rais. Kutokana na matatizo mbalimbali ya kimtazamo baina ya Rais na Waziri Mkuu, Serikali hiyo mpya ilijikuta ikipinduliwa na Kanali Jopeph Mobutu hapo tarehe 14 Septemba 1960 ambapo wiki chache baadaye, Kanali Joseph Mobutu alimuua Patrice Lumbumba. Mara baada ya mapinduzi na kifo cha Lumumba, nchi hiyo ilishuhudia machafuko kwa vipindi mbalimbali kuanzia mwaka 1960-1964 ambapo mara zote majeshi ya Serikali yakisaidiwa na yale ya Marekani pamoja na askari wa kukodiwa kutoka Ulaya yalikuwa wakidhibiti machafuko hayo. Mwaka 1965, Mobutu ambaye alijipandisha cheo na kuwa Luteni Jenerali, alijitangaza kuwa ni rais rasmi. Tokea mwaka 1965-1977 nchi hiyo ilishuhudia hali ya utulivu kiasi ingawa ilikuwa inaendeshwa kimabavu katika utawala wa kidikteta chini ya Rais Mobutu. Mwishoni mwa mwaka 1990, Serikali ya rais Mobutu iliandamwa na upinzani mkubwa kutoka ndani na nje ya nchi ikilalamikiwa kwa kutofuata haki za binadamu, rushwa, matumizi mabaya ya mali za serikali nk. Mwaka 1991 hali ya kiuchumi nchini Zaire ilizidi kuwa mbaya ambapo ilifikia wakati wanajeshi waligoma kutokana na kutolipwa mishahara.....

Mimi siyo mwandishi wa habari lakini bila shaka mmenipata ninachotaka kusema.
 
ninafanya hivi kwa nia njema na nadhani sijaharibu hali ya hewa

Kaka asante sana. Naiona nia njema yako kujujuza kinachoendelea huko Congo DRC. Binafsi nimejua mengine kiasi zaidi ya mwanzo.

Ila bado nina mashaka na amani ya kuduma Congo DRC, Kuanzia wananchi wa Congo DRC na hata serikali kuna haja ya kubadilisha mambo mengi sana.
Niliona baadhi ya clip za video zikionesha wanajeshi wa Congo DRC walevi, na matendo yao kipindi cha mapigano yanaonesha ni moja ya jeshi lisilokuwa na nidhamu kabisa.
Kama JWTZ wakiwasaidia WaCongoman kuwaondoa M23 bado tatizo litakuwepo kama hatutawasaidia kujenga jeshi lao. Tulifanya Uganda baada ya kumtoa Amin Dada, nadhani inahaja na Congo kusaidiwa.

Asante sana FLASH HIDER.
 
Hapo Goma,kuna mahusiano mazuri kati yenu wabongo na wanyarwanda hivi sasa?ukiwa mji wa mashariki mwa Congo,idadi ya raia wenye asili ya Rwanda ikoje hapo?Kuna kabila lolote la hapo lenye uhusiano wa damu na wanyarwanda au wote walioko hapo ni wahamiaji?
 
Karibu sana, hivi ninavyoandika hapa, Helikopta za FARDC zinapita hapa GOMA kuelekea eneo la mapigano, bila shaka M23 wanaadabishwa.

Du! Mkuu sijui kwa nini imetokea nikamkumbuka yule waziri wa habari wailiyokuwa iraq ya saadam hussein maarufu kama komedi/comic ally.

Swali langu la msingi vipi kuhusu zana za kivita walizo nazo hawa wapiganaji wetu? Maana kuna siku wameonekana kwenye tv wamejazana kwenye p/up double cabin la UN. Je hii haiwezi hatarisha maisha yao zaidi?
 
Karibu sana, hivi ninavyoandika hapa, Helikopta za FARDC zinapita hapa GOMA kuelekea eneo la mapigano, bila shaka M23 wanaadabishwa.

M23 Wanashikilia miji mingapi na ipi hadi sasa? idadi ya jeshi la waasi ni kama wangapi?
 
Kuna fununu kuwa wakati wa nyuma majeshi ya U.N yalituhumiwa kufanya biashara ya silaha na madini kwa waasi hasa Nkunda.Pia kuna fununu kuwa Nkunda alikuwa supported na belgium through Rwanda.Ni kweli mambo hayo yalikuwepo?ni nini kimeleta tofauti ya utendaji kati ya majeshi ya UN yaliyopita na haya ya sasa yaliyosheheni wabongo?

Hizo fununu na mimi nimezisikia sana. Unajua DRC ni nchi kubwa kiasi kwamba kuna maeneo hayajawahi kabisa kukaliwa na mtu. Majeshi ya UN yamekuwa wakiweka kambi zao katika maeneo hayo. Kuna uwezekano mkubwa hayo yanafanyika au yalikuwa yanafanyika.

Ni wazi kuwa Rwanda walikuwa wanam-support Nkunda. CNDP (kikundi cha NKUNDA)kilikuwa kinadai kuwa kinalinda maslahi ya Watusi (Wanyamulenge) waliokimbia Rwanda miaka ya 60. Hivyo ajenda hiyo ndiyo ilichukuliwa na Rwanda katika kuhalalisha support yao kwa Nkunda. Ukisoma uzi huu, kuna sehemu nimeeleza kwa kirefu mgogoro huu.


Kilicholeta utofauti wa utendaji wa Majeshi ya UN ya awali na haya ya sasa kwanza ni uzalenda na nia ya dhati ya kutaka kumaliza matatizo ya wa cONGO waliyonayo hawa wanajeshi wa sasa (JWTZ). Inasemekana hapo awali unaweza kusikia watu wanabakwa, badala ya kuchukua hatua hao jamaa wanakuja na kuanza kuchukua video kwa ajili ya kuonyesha kwao. Wacongo hawawapendi kabisa jamaa hao.Pili nimeambiwa kuwa hawa wamepewa nguvu zaidi ya kisheria na UN kuweza kushambulia. Yaani kaka kuna tofauti kubwa sana.
 
JWTZ na majeshi mengine ya SA na Malawi yote yapo front. Tofauti ni kuwa JWTZ ndiyo lead army kwa kutoa kamanda wa majeshi ya FIB na viongozi. Hawajatulia kaka. Habari zilizopo ni kuwa Miji iliyokaliwa kiukamilfu mpaka sasa ni Kiwanja, Rumangabo, Kitale, Kibumba, Kibati, Munigi, Rwaza na Kalengele.
Du!
JWTZ noma sana!
Najua hawapo mitaani ,lakini ukiwaona waambie sisi huku tunawapa kidole gumba- big up!
Lakini yote ni lile zoezi la karibia miaka 50 ua ukombozi wa Afrika?
 
Ni wazi kuwa M23 wanasaidiwa na Rwanda. Hilo liko wazi kabisa. Hii ni kutokana na historia ya nchi hizi mbili. Mgogoro wa DRC ni complex sana wengine wanafikia hata kueleza kuwa huenda hiyo ni tabia za nchi za FRANCOPHONE (Sorry for spelling). Zote hazijawahikuwa na amani ya kudumu. Fanya simple research utagundua hili.

Flash hider hivi rwanda kuwasaidia m23 wanasaidiwa na nani? Na ni kwa nini congo toka miaka hiyo ya 1960
mpaka leo wanashindwa kuituliza nchi yao?
 
Hapa mtaani hawapo kwa sasa ingwa huwa wanarudi. Kambi yao ipo hapa hapa GOMA. Wanafanya kazi nzuri sana kaka believe me. Ukitaka mwulize Mkongo yoyote aliyepo hapa GOMA.

Du!
JWTZ noma sana!
Najua hawapo mitaani ,lakini ukiwaona waambie sisi huku tunawapa kidole gumba- big up!
Lakini yote ni lile zoezi la karibia miaka 50 ua ukombozi wa Afrika?
 
Ulichozungumza Kilio changu ni kweli kabisa. Kwa mtazamo wangun(ambao unaweza pia kuwa challenged), matatizo ya DRC is more than M23. Kuna vikundi vingine veye silaha zaidi ya 25. Rushwa, unskilled workforce, patriotism ni sifuri kabisa. Wanahtaji reform ya maana kabisa. Sisi tulibahatika kutembelea nchi mbalimbali kibiashara tunaona wazi kazi iliyopo. Usitegemee kwenda polisi kushitaki jambo, rusha kwa traffic ni vitu vya kawaida sana. Sijui lakini wazo lako ni sawa mkuu kabisa mkuu.

Kaka asante sana. Naiona nia njema yako kujujuza kinachoendelea huko Congo DRC. Binafsi nimejua mengine kiasi zaidi ya mwanzo.

Ila bado nina mashaka na amani ya kuduma Congo DRC, Kuanzia wananchi wa Congo DRC na hata serikali kuna haja ya kubadilisha mambo mengi sana.
Niliona baadhi ya clip za video zikionesha wanajeshi wa Congo DRC walevi, na matendo yao kipindi cha mapigano yanaonesha ni moja ya jeshi lisilokuwa na nidhamu kabisa.
Kama JWTZ wakiwasaidia WaCongoman kuwaondoa M23 bado tatizo litakuwepo kama hatutawasaidia kujenga jeshi lao. Tulifanya Uganda baada ya kumtoa Amin Dada, nadhani inahaja na Congo kusaidiwa.

Asante sana FLASH HIDER.
 
Back
Top Bottom