Uliza chochote kuhusu wakurya.

Uliza chochote kuhusu wakurya.

Kwa nini mna makovu sana ya visu na mapanga?
Kichuri ni mchanganyiko wa nini na nini?

Je hakuna kabila linatoitwa wakurya kwa sababu ninyi kila ukoo una lugha yake? Mfano wanaoishi pale Ikoma wanaitwa 'waikoma', wanaoishi pale isenye wanaitwa 'waisenye' na kuendelea hivyo kwa kila kijiji na kufanya neno mkurya kuwa useless ukiw huko

Kuna aina mbili za wakurya kuna wale Wa asili ambao lugha yao ni moja tunawaita wakurya Wa nyanda za juu mfano wairegi,wakira,wanyabasi,watimbaru nyamongo nk,na wapo wakurya Wa nyanda za chini ambao lugha zinafanana ila matamshi tunatofautiana kama wakenye ,wasuba waikoma na wengineo .
 
Je hakuna kabila linatoitwa wakurya kwa sababu ninyi kila ukoo una lugha yake? Mfano wanaoishi pale Ikoma wanaitwa 'waikoma', wanaoishi pale isenye wanaitwa 'waisenye' na kuendelea hivyo kwa kila kijiji na kufanya neno mkurya kuwa useless ukiw huko.

Wewe huwajui wakurya badala ya kuuliza unajitahidi kupotosha watu.
Katika nchi hii nani asiyelifahamu kabila la wakurya? au unataka kufananisha wakurya na jamaa zangu wachaga?

Waikoma na Wanata ni makabila mawili tofauti na wakurya, angalau wao wenyewe wawili wanasikilizana kidogo.

Tunapozungumzia wakurya tunamaanisha kabila la wakurya ambao tumetapakaa kutoka Tanzania hadi Kenya. Wakurya tuna koo mbalimbali kama vile watimbaru, wanyabasi, wakira, walenchoka, waanchari, wairege, wasweta, wakenye, wahunyaga, wasimbete, watobori, wangoreme, wanyamongo n.k

Na wote hao tunaongea lugha moja tu ya kikurya.
 
Sikiliza nikwambie nanii, nani.. Eeer, unaitwa nani vile !?
Sample uliyoitumia haikuwa sahihi!

Uliyemdhania ndiye, kumbe.....!

Sifa pekee aliyojaliwa mkurya kwanza ni mkarimu endapo utakuwa mstaraabu na mwenye nidhamu!

Sifa nyingine ni hasira!

Hasira za mkurya ni mdomo na ulimi, na ili zitulie, lazima atende! Labda tu itokee incident akusamehe!

Mambo ya majigambo, waachie akina nshomile (au sio Ruttashobolwa? Nimeishi sana kahororo kwa akina KOKUTONA, nawafahamu sana wahaya, kila jumapili.... Bukoba inahamia beach bana! Teh teh)

Ha ha ha haaaaa yaani weweee.

Afu unakesi na mimi ya kujibu, usisahau
 
Wewe huwajui wakurya badala ya kuuliza unajitahidi kupotosha watu.
Katika nchi hii nani asiyelifahamu kabila la wakurya? au unataka kufananisha wakurya na jamaa zangu wachaga?

Waikoma na Wanata ni makabila mawili tofauti na wakurya, angalau wao wenyewe wawili wanasikilizana kidogo.

Tunapozungumzia wakurya tunamaanisha kabila la wakurya ambao tumetapakaa kutoka Tanzania hadi Kenya. Wakurya tuna koo mbalimbali kama vile watimbaru, wanyabasi, wakira, walenchoka, waanchari, wairege, wasweta, wakenye, wahunyaga, wasimbete, watobori, wangoreme, wanyamongo n.k

Na wote hao tunaongea lugha moja tu ya kikurya.

Mkuu Mwita Maranya bahati nzuri nimewahi kufanya shughuli mbalimbali huko Tarime na nina kauzoefu ka makabila hayo. Ninanchojua ni kwamba kuna koo mbalimbali kama ulivyosema lakini hizo koo zinatofautiana kwa lugha kiasi fulani. Kadri unavyotoka Tarime kuelekea Musoma ndivyo unavyokutana na tofauti hizo. Mfano kuna tofauti ya matamshi kati ya Wasimbete na Wakira/Wanyabasi na pia kuna tofauti ya kimatamshi kati ya Wasimbete na Wangoreme na pia Wangoreme na Wanyabasi; hapo pamekaaje?

Pia nina swali moja: Kuna majina ya kiume ya wakurya kama vile Chacha, Mwita, Wambura, Marwa na Magessa: Niliambiwa kwamba Magessa ni mtoto aliyezaliwa wakati wa mavuno; Wambura - Wakati wa mvua na Marwa - Wakati wazee wakipata pombe. Ila cha ajabu ni kwamba hata wakurya wenyewe hawajui maana ya majina Mwita na Chacha; mkuu naomba unisaidie maana ya majina Mwita na Chacha ukiachilia mbali kwamba ni majina wanayopewa mara nyingi watoto wa kwanza wa kiume.

 
Last edited by a moderator:
ugari kwa kikurya inaitwa bukima . je umewahi kuomba ugari kwa mwanamke wakisukuma naukataja kwa kikurya na kama ndivyo nini kilifuata..?? ni hilo tu
 
ugari kwa kikurya inaitwa bukima . je umewahi kuomba ugari kwa mwanamke wakisukuma naukataja kwa kikurya na kama ndivyo nini kilifuata..?? ni hilo tu

hahahaaaa!!!!

mkuu umenikumbusha mbali sana ujue!

nakumbuka nilikuwa hungumalwa, usukumani hukooo!!

basi kulikuwa na mama mmoja hivi alikuwa anauza chakula maeneo fulani hivi ya senta ya kijiji!

sasa kwa vile alikuwa mwenyeji wa mkoa wangu, nikamuongelesha kikwetu huku nikitamka hilo neno kwa kujiamini kabisa!

nakwambia watu woooote walinyamaza kimyaaaaa!!!! mimi huku sina hili wala lile!!

baadae kakaangu kaja niambia manke nini!!

dah, nilichoka! nguvu ziliisha ghafla hasa nikikumbuka niliongea mbele ya watu wazima, wanawake kwa watoto!
 
Ni kweli kuwa mwanaume aliyezaliwa na mwanamke asiyekeketwa hana heshima mbeleza wanaume wenzie?? na anajulikana kama "omona wa msaghane??"
kuna msemo wao wanasema okontema ontemele ila..... naleye.
 
Wewe huwajui wakurya badala ya kuuliza unajitahidi kupotosha watu.
Katika nchi hii nani asiyelifahamu kabila la wakurya? au unataka kufananisha wakurya na jamaa zangu wachaga?

Waikoma na Wanata ni makabila mawili tofauti na wakurya, angalau wao wenyewe wawili wanasikilizana kidogo.

Tunapozungumzia wakurya tunamaanisha kabila la wakurya ambao tumetapakaa kutoka Tanzania hadi Kenya. Wakurya tuna koo mbalimbali kama vile watimbaru, wanyabasi, wakira, walenchoka, waanchari, wairege, wasweta, wakenye, wahunyaga, wasimbete, watobori, wangoreme, wanyamongo n.k

Na wote hao tunaongea lugha moja tu ya kikurya.

Umeeleza vizuri ila hapo kwenye red nina mashaka ukiwauliza wangoreme wenyewe hawatakubali kuwa wao ni wakurya na hata matamshi ni tofauti sana japo majina ni sawa pia mila zote ni sawa wangoreme wana shabihiana sana na waikoma na waisenye.
 
Umeeleza vizuri ila hapo kwenye red nina mashaka ukiwauliza wangoreme wenyewe hawatakubali kuwa wao ni wakurya na hata matamshi ni tofauti sana japo majina ni sawa pia mila zote ni sawa wangoreme wana shabihiana sana na waikoma na waisenye.

ni kweli mkuu. mungurimi hakubali kuwa yeye ni mkurya. matamshi hayafanani kabisa

kwa mfano,

'' mimi ni mungulimi'
' eni nomongoleme neni; but mkurya atasema, ' uni nomokolinde nde' (nadhani nimepatia kwa upande wakurya. correction if needed)
 
Back
Top Bottom