Ulishawahi kusingiziwa kitu?

Ulishawahi kusingiziwa kitu?

Daaah
Pumzika kwa amani!!!! Sijawahi singiziwa jambo kubwa kama lile mimi jamani, umri wa miaka kumi na sita mama mtu mzima mwenye uwezo wa kunizaa... Inaniuma mpaka Kesho lakinii Mungu ndo ajua yote.

Pumzika tu mama kwa amani... Ulinifanya nione dunia chungu, kipigo nilichopata ndo hicho ulichokipata mpaka umauti ukakufika na mtu huyo huyo alonipiga mie!!!!

Pumzika kwa amani, kisa tu barua aloandika nduguyo wa kikee akimsaidia mwanao kuniandikia mimi ili tu nimkubali kwa hand writing nzuri!!!! Loooh mumewe alinipiga si kawaida!!!!, kwa kuaminishwa tuu namrubuni mwanae. Mamangu nae hakutaka kunielewa mama ukaniongezea kipigo tena!!!! Mama najua hakuwa na lengo baya mama, Nilikusamehe na Nakupenda mnooo Mamangu!!!
 
Nakumbuka kipindi fulani niko shuleni kuna demu mmoja nilikuwa na kabifu nae ka chini chini kabisa yule alikuwa rafiki angu sana,akasema mimi mjamzito na ni muathirika nina ukimwi. Nilikuwa nalia kila siku Dom watu wananicheka balaa,tena shule ya girls umbea unasambaa kama moto wa petrol kila kona unanyooshewa vidole. Nakumbuka nilimfata nikamuuliza kwanini unanizushia tuhuma hizi,mbele za watu huku akipaza sauti akasema ndio wewe una mimba na ukimwi kwani uongo? Watu walinicheka,walinizomea na kunisema vibaya juu ,Niliishiwa pozii hata ya kunyanyua mguu kutoka sikuwa na nguvu hiyo, kuna dada alikuwa anatuzidi darasa ndio akaja kunitoa. She please me mpaka nikaacha kulia lakini moyoni nilikuwa na hasira kali na yule demu. Nikaenda kwa matron nikamwambia nataka kupima ukimwi,matron alishangaa balaa akamuita mwalimu wa malezi still nika insist nataka kupimwa,wakanipeleka kufanyiwa counselling na mshauri wa wanafunzk nikagoma na kusimamia msimamo wangu ikabidi siku ile ile wanipeleke hospital wanipime,nikakutwa sina maambukizi wala mimba hapo nikaliamsha dude maana sikusema lolote kwao nilisubiri mpaka nipimwe wawe na uhakika. Ilikuwa bonge la kesi akaambiwa aniombe msamaha assemble maana alitangaza taarifa za uongo karibia shule nzima ilijua, watu wakaanza kumzomea alivyokuwa anajielezea kwamba kanizushia sababu ya kibifu chetu kisicho na kichwa wala miguu.
Sitasahau ile ishu aseeee.
Kumbe ndio wewe niliehadithiwa nishakujua
 
Mie nina hasira sana watu hadi leo wananisingizia eti EDWARD LOWASA "ni mtu wangu" ila basi tu, itabidi sasa nifanye kweli
Hata kama mtu unamchukia vipi huwezi mkebehi stairi hii. Fikiria kama wewe mzazi then watoto wako wakaiga tabia yako...... basi wote watakuwa ma babieiiiiiiiiiiis..
 
Kiufupi tu nilisingiziwa nimeuza mbuzi wa nyumbani, sitakaa nisaau
 
Nakumbuka kipindi fulani niko shuleni kuna demu mmoja nilikuwa na kabifu nae ka chini chini kabisa yule alikuwa rafiki angu sana,akasema mimi mjamzito na ni muathirika nina ukimwi. Nilikuwa nalia kila siku Dom watu wananicheka balaa,tena shule ya girls umbea unasambaa kama moto wa petrol kila kona unanyooshewa vidole. Nakumbuka nilimfata nikamuuliza kwanini unanizushia tuhuma hizi,mbele za watu huku akipaza sauti akasema ndio wewe una mimba na ukimwi kwani uongo? Watu walinicheka,walinizomea na kunisema vibaya juu ,Niliishiwa pozii hata ya kunyanyua mguu kutoka sikuwa na nguvu hiyo, kuna dada alikuwa anatuzidi darasa ndio akaja kunitoa. She please me mpaka nikaacha kulia lakini moyoni nilikuwa na hasira kali na yule demu. Nikaenda kwa matron nikamwambia nataka kupima ukimwi,matron alishangaa balaa akamuita mwalimu wa malezi still nika insist nataka kupimwa,wakanipeleka kufanyiwa counselling na mshauri wa wanafunzk nikagoma na kusimamia msimamo wangu ikabidi siku ile ile wanipeleke hospital wanipime,nikakutwa sina maambukizi wala mimba hapo nikaliamsha dude maana sikusema lolote kwao nilisubiri mpaka nipimwe wawe na uhakika. Ilikuwa bonge la kesi akaambiwa aniombe msamaha assemble maana alitangaza taarifa za uongo karibia shule nzima ilijua, watu wakaanza kumzomea alivyokuwa anajielezea kwamba kanizushia sababu ya kibifu chetu kisicho na kichwa wala miguu.
Sitasahau ile ishu aseeee.
Hahaha watoto wa kike bana..
 
Daaah
Pumzika kwa amani!!!! Sijawahi singiziwa jambo kubwa kama lile mimi jamani, umri wa miaka kumi na sita mama mtu mzima mwenye uwezo wa kunizaa... Inaniuma mpaka Kesho lakinii Mungu ndo ajua yote.

Pumzika tu mama kwa amani... Ulinifanya nione dunia chungu, kipigo nilichopata ndo hicho ulichokipata mpaka umauti ukakufika na mtu huyo huyo alonipiga mie!!!!

Pumzika kwa amani, kisa tu barua aloandika nduguyo wa kikee akimsaidia mwanao kuniandikia mimi ili tu nimkubali kwa hand writing nzuri!!!! Loooh mumewe alinipiga si kawaida!!!!, kwa kuaminishwa tuu namrubuni mwanae. Mamangu nae hakutaka kunielewa mama ukaniongezea kipigo tena!!!! Mama najua hakuwa na lengo baya mama, Nilikusamehe na Nakupenda mnooo Mamangu!!!
Pole mwaya Sakayo
 
Singiziwa vyote ila sio ile unaambiwa 'mbona upo, tuliambiwa umekufa'
 
Sema ishu ya Kusingiziwa mwizi afuu mtu akapiga kabisa kelele ndo mbaya kuliko zote aisee.. Me kuna siku nlienda kumpa hi manzi flani mzee wake akaja akakuta tumesimama nje kwao pale alinipiga Beat afuu akasema au Nikuitie mwizi...!?? Daah nkikumbuka huwa najiuliza maswali mengi sana... Toka siku hiyo yule manzi hata namba yake nlifutaa...
 
  • Thanks
Reactions: THT
Shule ya msingi hiyo, ninaishi na mama wa kambo kwa muda mrefu tu. Mama yangu alinilea hadi nilipofikisha miaka mitano tu, Mungu amrehemu mama yangu.


Nakumbuka kwa jirani kulikuwa na rafiki zangu wawili ambao hadi leo hii ni marafiki zangu ukubwani pia. Hawa jamaa walianza kufuga njiwa na mimi nikawa napenda haswa kuanza nao. Siku moja naikumbuka wazi ilikuwa ni jumatatu, nilijiminya nikatoa 300 rafiki yangu akaongeza 200 ikawa 500 nikaenda kununua Njiwa. Nina furaha sana ya utotoni nimeanza kufuga njiwa, kumbe huko upande wa pili kumenuka.


Kumbe ndani kaka yangu ambaye kipindi hiko yupo form one, aliibiwa 300. Si akaja kusikia nimetoa 300 kuchanga nipate njiwa. Alinikomalia mimi ndiye nimemwibia ile hela, msala ukafika kwa mzee.


Mama yangu wa kambo ana watoto wawili wa kike wakubwa tumechangia baba, mmoja alinikomalia nimeiba. Nikaitwa mbele ya Mzee, nilishinikizwa nikubali nimeiba.


Aisee mwishowe nikakubali kosa lisilo langu, Mzee nalaumu hakuwa akitupa nafasi ya kutusikiliza. Nilipigwa mno kwa kusingiziwa huku, ninatoka hapo huko nasakamwa ni kidokozi. Hili jambo sikuwahi kulisema hata muda ambao Mzee alianza kujua muda mwingine anatuonea na akawa rafiki yetu mkubwa
 
Back
Top Bottom